Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza. Je, ni lini mradi wa maji wa kutoka Nyamtukuza, Kakora, Kharumwa, Izunya, Kayenze hadi Bukwimba utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza nianze kuishukuru Serikali kwa kukamilisha kwenda kukamilisha mradi huu ambao ni wa kihostoria.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa sababu unaenda kukamilika mradi huu ambao utahudumia zaidi wananchi 51,500,000 mradi huu unaenda kukamilishwa mwezi Juni. Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa yupo tayari kuambatana nami kwa ajili ya kwenda kuukabidhi mradi huo na kufanya sherehe kwa sababu mradi ule ni wa kihistoria kuanzia mwaka 1975? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuendelea kusambaza maji baada ya kukamilisha vijiji hivyo 12 katika kata zifuatazo: Kata ya Nyugwa, Nyijundu, Kaboha, Shabaka, Nyangh’wale na Busolwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kusambaza maji katika kata hizo? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Amar Nassor Hussein, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nipende kupokea pongezi za shukrani kutoka kwako na pia suala la kuambatana na Mheshimiwa Mbunge, mimi na yeye tayari tulishafika pale Nyangh’wale, basi nitatoa nafasi hii kwa majimbo mengine ila nikishakamilisha nitaweza kutafuta nafasi ya kuja sasa kusheherekea.

Mheshimiwa Spika, mpango wa kusambaza maji katika kata alizozitaja Mheshimiwa Mbunge upo tayari kwenye mipango mikakati ya mwaka ujao wa fedha. Hivyo naomba tuendelee kuvuta Subira, tutakwenda mwaka ujao wa fedha kuona maji sasa yanaendelea kuwasogelea wananchi katika makazi yao.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza. Je, ni lini mradi wa maji wa kutoka Nyamtukuza, Kakora, Kharumwa, Izunya, Kayenze hadi Bukwimba utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naishukuru sana Serikali kwa kutuchimbia visima katika Jimbo la Ikungi Mashariki na Ikungi Magharibi. Hata hivyo, visima hivi havina kabisa mtandao wa maji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha visima hivi vinakuwa na mtandao wa maji ili kuwawezesha wananchi wa majimbo haya mawili la Ikungi Mashariki na Ikungi Magharibi kuweza kupata maji safi na salama? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali ya nyongeza ya Mheshimiwa Aysharose, Mbunge Viti Maalum kutoka Singida, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kutambua kazi kubwa ambayo Wizara imefanya kuchimba visima vya kutosha na kwa sasa hivi kazi inayofuata ni kuona mtandao unakwenda kuwafikia wananchi. Hivyo Serikali huwa tunaangalia kwanza kupata chanzo na uhakika wa chanzo ukishapatikana tunajenga vituo vya kuchotea maji. Sasa tupo kwenye utaratibu wa kuona kwamba mtandao huu unaendelea kuwasogelea wananchi kadri mahitaji yanavyohitajika. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza. Je, ni lini mradi wa maji wa kutoka Nyamtukuza, Kakora, Kharumwa, Izunya, Kayenze hadi Bukwimba utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Wewe ni shahidi Mradi wa Maji Bunda sasa hivi unachukua takribani miaka kumi na tatu, najua kuna awamu ya tanki imekalimilika. Awamu nyingine ilikuwa ni kuhakikisha wanasambaza mabomba na kueneza mtandao wa maji katika kata zote 14. Hivi ninavyozungumza ni kata saba tu tayari ndiyo zimeanza kusambaza mradi wa maji na wana uhakika wa kupata maji angalau kwa asilimia 50. Je, ni lini sasa Wizara itahakikisha kata zote 14 za Bunda Mjini zinapata maji na ukizingatia humu ndani mimi ndiyo nawasemea hakuna anayewasemea. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nipende kupokea pongezi kwa kuona kwamba tanki limekamilika na angalau asilimia hamsini ya usambazaji umeshakuwa katika utekelezaji. Kwa sababu tuna kata 14 na kata saba tayari utekelezaji unaendelea hiyo ndiyo kazi ya Wizara ya Maji.

Vilevile kama ambavyo umemtaja Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo kazi hii imefanyika kwa usimamizi madhubuti. Mbunge wa Jimbo amekuwa akifuatilia mara nyingi na kwa sababu Mbunge wa Jimbo amekuwa akiwasiliana na Wizara mara kwa mara ndiyo maana maji kata saba, kati ya kata 14 yameweza kutolewa. (Makofi)