Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Niishukuru Serikali kwa majibu mazuri ambayo Naibu Waziri amewasilisha, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; wananchi wa Kata hii ya Imalamate yenye vijiji vitatu, kwa maana ya Mahwenge, Imalamate pamoja na Jisesa, wamejitolea sana kwa kujenga maboma ya kisasa ya zahanati. Je, Serikali haioni sasa umuhimu wa kuifanya kata hii kuwa moja ya kata za mfano ambazo wananchi wamejitolea kwa kujenga maboma haya ili waipatie kipaumbele cha kukamilisha maboma haya?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, Naibu Waziri yuko tayari sasa baada ya Bunge baada ya Bunge hili la Bajeti kuambatana pamoja nami ili kwenda kuwatembelea wananchi wa Kata ya Imalamate kuona kazi kubwa ambayo wameifanya ambayo itakuwa ya kuigwa katika nchi yetu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, kwa kazi kubwa sana anayoifanya ya kuhakikisha anawasemea wananchi wake na kufuatilia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miradi ya huduma za afya. Pia niwapongeze sana wananchi wa Kata hii ya Imalamate na wananchi wa Busega kwa ujumla kwa kuendelea kuchangia nguvu zao katika ujenzi wa miundombinu ya kutoa huduma za afya kwa maana ya zahanati na vtuo vya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua na inathamini kwamba wananchi hawa wameendelea kutoa nguvu zao. Na ni kweli, ni moja ya kata ambazo zimefanya vizuri katika ujenzi wa vituo vya afya na hivyo katika mwaka ujao wa fedha, tumetenga shilingi milioni 150 kwa ajili ya maboma matatu katika Jimbo la Busega. Kwa hiyo bila shaka fedha hizi zitakwenda kukamilisha majengo haya katika Kata ya Imalamate.

Mheshimiwa Naibu Spika, niko tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kushirikiana naye kuwahudumia wananchi wa Busega, lakini pia kutambua michango yao. Hivyo baada ya kikao hiki, tutapanga na Mheshimiwa Simon Songe tuweze kuona lini muda muafaka tutaambatana kwenda Jimboni kwake Busega.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Wananchi wa Jimbo la Meatu wapo wanaotembea hadi kilometa 40 kwenda tu kufuata huduma za afya katika zahanati. Je, ni lini Halmashauri ya Wilaya ya Meatu italetewa fedha za kukamilisha maboma katika ule utaratibu wa kukamilisha maboma matatu kwa mwaka 2020/ 2021?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Leah Komanya kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwasemea wananchi wa Meatu, lakini pia kuhakikisha miradi ya huduma za afya inakamilishwa na kusogeza huduma za afya karibu zaidi na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Jimbo la Meatu ni jimbo kubwa na wananchi wanafuata huduma za afya mbali kutoka kwenye makazi yao. Ndiyo maana Serikali imeweka mpango wa maendeleo ya afya msingi kuhakikisha tunajenga zahanati katika kila kijiji, vituo vya afya katika kata ili kusogeza huduma hizi kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba katika mwaka huu wa fedha 2020/2021, Serikali ilitenga shilingi bilioni 27.75 na tayari imekwishatoa shilingi bilioni 23 katika majimbo na wilaya zipatazo 133 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma matatu kwa kila halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimhakikishie kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha, Juni 30, Jimbo la Meatu pia litakuwa limepata fedha zile shilingi milioni 150 kwa ajili ya kukamilisha maboma hayo. Hili ni sambamba na majimbo na halmashauri zote ambazo bado hazijapata milioni 150, shughuli hiyo inaendelea kutekelezwa na kabla ya Juni 30, fedha hizo zitakuwa zimefikishwa katika majimbo hayo.

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo?

Supplementary Question 3

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo lililoko Busega linafanana kabisa na tatizo lililoko katika Jimbo la Magu. Jimbo la Magu lina vijiji 82, vijiji 40 vina zahanati, vijiji 42 havina zahanati. Tunavyo vijiji 21 ambavyo vimekamilisha maboma ya zahanati. Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia maboma hayo 21 ambayo yanahitaji bilioni moja na milioni 50 ili wananchi waweze kupata huduma kama inavyosema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwamba kila kijiji kiwe na zahanati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali inaendelea kujenga vituo vya afya na zahanati katika vijiji na kazi kubwa imekwishafanyika nchini kote ikiwepo katika Jimbo la Magu. Hata hivyo, ni kweli kwamba bado kazi ni kubwa, bado kuna vijiji vingi na kata nyingi ambazo bado zinahitaji kujenga vituo vya afya na zahanati. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kiswaga kwamba Serikali itaendelea kutenga fedha kila mwaka wa fedha kuhakikisha tunaendelea kujenga vituo vya afya na zahanati nchini kote, lakini pia katika Jimbo hili la Magu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitambue kwamba katika mwaka huu wa fedha, tayari Jimbo la Magu limeshapelekewa milioni 150 kwa ajili ya kuchangia nguvu za wananchi kujenga na kukamilisha maboma matatu na katika mwaka ujao wa fedha pia imekwishatengewa shilingi milioni 150 kwa ajili ya kukamilisha maboma matatu ya zahanati. Kwa hiyo maboma haya yote yaliyobakia pamoja na nguvu za mapato ya ndani ya halmashauri, Serikali itaendelea kutenga fedha kuhakikisha maboma haya yanakamilika na kusogeza huduma za afya karibu zaidi na wananchi.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo?

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa hali ilivyo katika Jimbo la Busega inafanana kabisa na hali ilivyo katika Jimbo la Sumve. Katika Kata ya Mwabomba wananchi wamejenga maboma katika Vijiji vya Mwambomba, Mulula na Ngogo na mpaka sasa maboma haya hayajamaliziwa, ni maboma ya zahanati. Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa Serikali itamalizia maboma haya ili wananchi wa Kata ya Mwabomba na wenyewe wapate huduma ya afya kama yalivyo maeneo mengine?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasalali, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kata hii ya Mwabomba katika Jimbo hili la Sumve, ni kweli kwamba wananchi wameendelea kuchanga nguvu zao kwa ajili ya ujenzi wa maboma ya zahanati na katika vijiji hivi vitatu, kwanza niwapongeze sana kwa kutoa nguvu zao na kujenga maboma haya kuonesha kwamba kimsingi wana uhitaji mkubwa wa huduma za afya. Ndiyo maana Serikali imeendelea kutambua na kuthamini sana nguvu za wananchi kwa kutenga fedha kwa ajili ya kila jimbo kupelekewa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma haya ya zahanati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo katika Jimbo la Sumve pia, nimhakikishie Mheshimiwa Kasalali kwamba fedha zimetengwa kwa mwaka ujao wa fedha, maboma matatu, ambayo yanahitaji kwenda kukamilishwa yatakwenda kukamilishwa. Nimweleze Mbunge, kwa kuwa vipaumbele ni haya maboma matatu na tayari milioni 150 zimetengwa kwa ajili ya maboma hayo, kwa hiyo tatizo hilo limeshapatiwa majawabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili ni endelevu. Katika kila mwaka wa fedha tutaendelea kuhakikisha tunatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma yote yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuendelea kuimarisha huduma za afya kwa wananchi wetu.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Imalamate Wilayani Busega wamejenga zahanati na kumaliza maboma manne kwa maana ya zahanati moja kila kijiji:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hao kuezeka maboma hayo ili waweze kupata huduma za afya kwenye zahanati hizo?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Changamoto zilizopo kule Busega zinafanana sana na changamoto ambazo tunazo Arumeru Mashariki. Wananchi Kata za Kikatiti, King’ori, Majengo, Gabobo na Kikwe, wanahangaika kila leo kujenga zahanati wenyewe lakini hatujaona Serikali ikija kutusaidia. Je, Serikali ina mpango gani wa kuja kutupa msaada na sisi tuweze kupata huduma za afya kikamilifu?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba wananchi wa Arumeru Mashariki wameendelea kuchangia nguvu zao kujenga maboma ya zahanati na vituo vya afya. Serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wananchi wale wanaungwa mkono kwa juhudi zao ambazo wanazionesha katika kuwekeza katika miundombinu hii ya huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo pamoja na maboma hayo mengine ambayo Mheshimiwa Dkt. Pallangyo ameyasema, nimhakikishie kwamba, kwanza katika mwaka huu wa fedha ambao tunaendelea, 2020/2021, shilingi milioni 150 kwa ajili ya maboma matatu, kuhakikisha kwamba yanakamilishwa, zimetengwa na zitafikishwa kabala ya tarehe 30, Juni, mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka ujao wa fedha, 2021/21, Serikali pia imetenga shilingi milioni 150 kwa ajili ya maboma matatu katika Jimbo hili la Arumeru Mashariki. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Pallangyo kwamba tutahakikisha tunaendelea kutenga fedha za kuchangia nguvu za wananchi kukamilisha maboma ya zahanati na vituo vya afya ili tuendelee kusogeza huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, amekuwa mfuatiliaji wa karibu sana kwa ajili ya wananchi wa Arumeru Mashariki, amehakikisha anasimamia miradi mbalimbali ikiwemo miradi hii ya huduma za afya. Na sisi tumhakikishie kwamba tutaendelea kushirikiana kwa karibu sana na wananchi wa Jimbo la Arumeru Mashariki, lakini pia na Mheshimiwa Dkt. Pallangyo kuhakikisha kwamba tunahudumia wananchi wetu kwa karibu zaidi.