Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Tingi – Kipatimu yenye urefu wa kilometa 50 kwa kiwango cha lami hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inapita katika maeneo yenye kumbukumbu za Vita vya Majimaji na vivutio muhimu vya Utalii?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza. Kwa sasa Barabara ya Tingi – Kipatimu ina maeneo mengi ambayo hayapitiki na mengine yanapitika kwa shida sambamba na Barabara ya Nangurukuru – Liwale.

Je, Serikali ina mpango gani wa dharura wa kuweza kurekebisha barabara hizo mbili ili ziweze kutengenezwa na hatimaye wananchi waweze kuendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, barabara hizi mbili za Nangurukuru – Liwale kilometa 258 na hiyo ya Tingi – Kipatimu katika miaka ya karibuni zilipanuliwa upana wake, lile eneo la hifadhi ya barabara kutoka mita 30 hadi kufikia mita 45. Na hii Hali ilisababisha wananchi kuweza kuvunjiwa nyumba zao na kuondolewa mazao yao. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa wananchi ambao hawajalipwa hadi sasa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Tingi – Kipatimu ina vilima, na katika swali lake la msingi nimejibu kwamba, tayari TANROADS Mkoa wa Lindi umeainisha maeneo yote korofi ambayo yana vilima na yatawekewa lami. Na hivi tunavyoongea mwaka huu itawekwa walao mita 500 na mwaka wa fedha kama bajeti itapita pia, maeneo yameainishwa ambayo tunategemea kuongeza kiwango cha lami maeneo ambayo barabara inakuwa ina milima na inateleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Barabara ya Nangurukuru – Liwale, yako maeneo ambayo inapita kwenye bonde na maji huwa yanajaa. Na tunategemea kwenye bajeti ya mwaka huu tunayoiendea kama itapitishwa litajengwa tuta kubwa ambapo maji sasa yatakuwa hayana uwezo wa kufurika na kuziba njia hiyo ya Barabara ya Nangurukuru – Liwale.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu fidia, ni kweli kwamba, baada ya sheria kupitishwa barabara zetu zimetanuliwa kutoka mita 30 hadi 45, lakini 45 hadi 60. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, mita hizi ambazo zimeongezeka saba na nusu, sab ana nusu kwa upande, pale ambapo ujenzi utaanza basi wananchi hawa ambao watakuwa ni wathirika watapata fidia wakati mradi huu utakapoanza kutekelezwa kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Tingi – Kipatimu yenye urefu wa kilometa 50 kwa kiwango cha lami hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inapita katika maeneo yenye kumbukumbu za Vita vya Majimaji na vivutio muhimu vya Utalii?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali iliahidi kwa muda mrefu sana Barabara ya Karatu – Mbulu – Singida na mpaka sasa hamna dalili yoyote ya kujenga kwa kiwango cha lami. Je, ni lini Serikali itatenga hela kwa ajili ya Barabara ya Karatu – Mbulu – Singida?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Karatu – Mbulu – Singida ni kati ya barabara ambazo zimeainishwa kwenye ilani na ambazo zinategemea kujengwa kwa kiwango cha lami katika kipindi hiki cha miaka mitano. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Karatu na wananchi wa Karatu na wote watakaonufaika na barabara hizi kwamba, kadiri Serikali itakavyopata hela na katika kipindi hiki cha miaka mitano barabara hizi zitajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Tingi – Kipatimu yenye urefu wa kilometa 50 kwa kiwango cha lami hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inapita katika maeneo yenye kumbukumbu za Vita vya Majimaji na vivutio muhimu vya Utalii?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali inaendelea kukamilisha ahadi za viongozi waliotangulia. Mheshimiwa wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Jakaya Kikwete alitembelea Wilaya ya Nyan’ghwale na kuahidi ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kahama – Nyan’ghwale kwenda Sengerema, lakini mwaka 2015 Hayati Dkt. John Pombe Magufuli naye aliahidi hivyohivyo kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Swali, ni lini Serikali itatenga fedha za upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo la lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye majibu mengine, Barabara ya Kahama
– Nyn’ghwale – Sengerema pale Busisi ni barabara ambazo zimeahidiwa na viongozi wetu na ni barabara muhimu sana kwa kuunganisha maeneo haya. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Nyan’ghwale kwamba, barabara hii itafanyiwa upembuzi yakinifu mara bajeti tunayoiendea itakapokuwa imepitishwa. Kwa hiyo, baada ya kufanya hivyo taratibu nyingine kwa maana ya usanifu wa kina utafanyika, ikiwa ni hatua za awali kuelekea ujenzi wa lami wenyewe. Ahsante.