Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itaongeza Vituo vya Afya katika Kata za Jimbo la Segerea Pamoja na kupandisha hadhi Zahanati za Kinyerezi, Segerea, Kipawa na Yombo Kiwalani ili kuondoa adha kwa wananchi wa Kata 13 wanaotegemea Kituo kimoja cha Afya? (b) Je, ni lini Kata za Minazi Mirefu, Buguruni, Kimanga na Kisukuru zitapatiwa Zahanati?

Supplementary Question 1

MHE. BONNAH L. KAMOLI: Ahsante. Pamoja na majibu mazuri ambayo ameyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili nyongeza. Swali la kwanza: Je, ni lini Serikali itaanza kupanga vituo vya afya kutokana na wingi wa watu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Sera ya Serikali ni kila Kata kuwa na Kituo cha Afya na Kila Mtaa uwe na Zahanati: Je, ni lini Serikali italeta vituo vya afya katika Kata ya Kimanga, Kisukuru, Buguruni pamoja na Minazi Mirefu ili hawa wananchi waweze kuondokana na matatizo hayo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Ni kweli kwamba tunajenga Vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali za Halmashauri katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuzingatia: kwanza, ukubwa wa kijiografia wa maeneo hayo; na pili, idadi ya wananchi katika maeneo husika ili kuhakikisha vituo vile vinasogeza huduma za afya karibu zaidi na wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Bonnah kwamba Serikali imeendelea kujenga vituo vya afya kwa kuzingatia vigezo hivyo viwili; kigezo cha ukubwa wa jimbo au halmashauri na pia kigezo cha idadi ya wananchi. Kwa mfano, katika Jiji la Dar es Salaam, miaka miaka mitano iliyopita, zaidi ya vituo vya afya 12 vimeendelea kujengwa na Hospitali za Wilaya zimeendelea kujengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha ujao wa 2021/2022 katika Manispaa ya Ilala kwa maana ya Jiji la Dar es Salaam peke yake, kuna vituo vya afya vipatavyo sita vitakwenda kujengwa, pamoja na Hospitali ya Halmashauri na katika Halmashauri zote za Jiji la Dar es Salaam zitakwenda kujenga angalau vituo vya afya vitatu. Kwa hiyo, tunaona Serikali imeendelea kuhakikisha inaongeza idadi ya vituo vya afya katika Manispaa na Jiji la Dar es Salaam kwa kuzingatia idadi ya wananchi; na suala hili linafanyika kwa utaratibu huu nchini kote.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, Sera ya Serikali ya Mpango wa Maendeleo ya Msingi ni kuhakikisha kila Kata inakuwa na Kituo cha Afya na Zahanati katika Vijiji. Sera hii imeendelea kutekelezwa kwa vitendo na Waheshimiwa Wabunge wamekuwa mashahidi kwamba Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa sana katika ujenzi wa zahani na vituo vya afya katika kata zetu. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi kwa vituo vya afya ambavyo tayari Serikali imeanza kujenga na katika kata hizo ambazo Mheshimiwa Kamoli amezitaja. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itaongeza Vituo vya Afya katika Kata za Jimbo la Segerea Pamoja na kupandisha hadhi Zahanati za Kinyerezi, Segerea, Kipawa na Yombo Kiwalani ili kuondoa adha kwa wananchi wa Kata 13 wanaotegemea Kituo kimoja cha Afya? (b) Je, ni lini Kata za Minazi Mirefu, Buguruni, Kimanga na Kisukuru zitapatiwa Zahanati?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Jitihada za kujitolea ambazo wananchi wa Jimbo la Segerea wamezionesha, zinafanana sana na jitihada ambazo wananchi wa Jimbo la Nkasi Kaskazini wamezionesha katika kata 17 tunavituo vya afya viwili lakini kuna vituo ambavyo tayari vimeanzishwa kwa nguvu za wananchi. Ni lini Serikali itapeleka fedha kwenye Kata ya Kabwe ili kuheshimu na kuendelea kuhamasisha wananchi kujitolea? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini pamoja na wananchi wa Nkasi Kaskazini kwa kazi kubwa ambayo wameendelea kuifanya kuhakikisha wanachangia nguvu zao katika ujenzi wa miradi ya maendeleo vikiwemo vituo vya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua na inathamini sana nguvu za wananchi na tutaendelea kuhakikisha tunatenga fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma ambayo wananchi wameanza kuyajenga kwa nguvu zao na mfano mzuri katika bajeti ya mwaka ujao maboma zaidi ya 108 kwa maana ya vituo vya afya vitakwenda kujengwa kwa mapato ya ndani ya halmashauri na vituo vya afya 18 vitakwenda kujengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna vile zahanati maboma 578 yatakwenda kujengwa.

Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba katika mpango huu ujao pia katika Jimbo hili la Nkasi Kaskazini tutakwenda kulipa kipaumbele kuhakikisha kwamba wananchi wanaona matunda ya Serikali yao katika kujali nguvu ambazo wameziweka katika maboma yale.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itaongeza Vituo vya Afya katika Kata za Jimbo la Segerea Pamoja na kupandisha hadhi Zahanati za Kinyerezi, Segerea, Kipawa na Yombo Kiwalani ili kuondoa adha kwa wananchi wa Kata 13 wanaotegemea Kituo kimoja cha Afya? (b) Je, ni lini Kata za Minazi Mirefu, Buguruni, Kimanga na Kisukuru zitapatiwa Zahanati?

Supplementary Question 3

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imeendelea kutenga fedha na kupeleka fedha kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kivule na tayari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepokea shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa wodi na shilingi milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Afya ya Kinywa na Meno.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutenga fedha na kupeleka kwenye Kituo cha Afya cha Mama na Mtoto, Chanika ili kiweze kujengewa wodi na kuweza kupanda hadhi kuwa hospitali kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya wananchi wa Kata za Chanika, Zingiziwa, Msongola, Majohe na Buyuni?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Jerry Silaa kwa kusimamia kwa karibu sana miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Ukonga. Kwa kweli Serikali imeendelea kushirikiana sana kwa karibu na wananchi pamoja na Mbunge wa Ukonga kuhakikisha vituo vya afya hivyo alivyovitaja Kivule na pia kuhakikisha fedha zaidi ya shilingi milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali zimepelekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Chanika kwa sasa kinatoa huduma kwa akina mama wajawazito, lakini Serikali inaona kuna kila sababu ya kutenga fedha ili kuongeza miundombinu ya huduma za afya katika Kituo cha Afya cha Chanika ili pamoja na huduma za Afya ya Mama na Mtoto kianze kutoa huduma nyingine kwa wagonjwa ili kusogeza huduma za afya kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba katika mipango ya Serikali, tutakipa kipaumbele Kituo cha Afya cha Chanika ili kiweze kupata fedha kwa ajili ya kujenga miundombinu hiyo na kuhakikisha kwamba huduma zote za afya zinasogezwa kwa wananchi.