Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya ujenzi wa barabara ya urefu wa kilomita tano kwa kiwango cha lami Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa majibu ambayo yanaeleza zaidi barabara za kawaida kwa sababu milioni 900 haina uwezo wa kujenga kilometa ya lami hata moja. Kwa hiyo naomba sasa kujua kwa sababu Mji wa Ikungi ni mpya kwa maana ya wilaya ni mpya na kwa sababu Makao Makuu ya Wilaya tunategemea yawe na lami. Sasa naomba nijue kwa sababu Mheshimiwa Waziri Mkuu alituhakikishia tangu 2019 na leo ni 2021; je, ni lini hasa Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kujenga hizo kilometa tano ya lami ili wananchi wa Ikungi nao waweze kupata lami na kufaidi matunda ya uhuru? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ametaka kufahamu ni lini sasa Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kujenga kilometa tano za lami katika Makao Makuu ya Wilaya yake katika eneo la Ikungi. Ni kwamba, kama katika jibu letu la msingi tumeainisha hapa kwamba katika mwaka huu wa fedha 2021/2022, tumepanga kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini kwa maana ya TARURA kutenga fedha kwa ajili ya kufanya usanifu na tathmini za gharama ya ujenzi kwa kiwango cha lami katika eneo hilo. Kwa hiyo mara baada ya usanifu na tathmini ya kina ambayo itakwenda kufanyika katika mwaka huu wa fedha maana yake katika mwaka wa fedha unaofuatia tutaanza kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa lami katika eneo la Ikungi. Nimhakikishie, Serikali ya Rais wa Sita, mama Samia Suluhu Hassan iko tayari kukamilisha ahadi hiyo kwa vitendo. Ahsante sana.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya ujenzi wa barabara ya urefu wa kilomita tano kwa kiwango cha lami Wilayani Ikungi?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, naomba kufahamu kwamba, ni lini barabara ya kutoka Mlowo kwenda Kamsamba ujenzi wake utaanza, ikizingatiwa kwamba, suala zima la upembuzi pamoja na usanifu limeshakamilika, lakini pia ni barabara ambayo ipo kwenye Ilani ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na ni ahadi ya Mheshimiwa Rais ya Awamu ya Tano pamoja na Awamu ya Sita, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alipokuja kwenye kampeni. Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA – MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, barabara hii naifahamu vizuri ni barabara ambayo inasimamiwa na TANROADS. Ni kutoka Mloo mpaka Kamsamba ambapo ni nyumbani kwetu kabisa ni kilometa 166.6 na miaka yote imekuwa ikihudumiwa na TANROADS. Bahati nzuri kwasababu Serikali ni moja na ndio maana iko katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ninaamini mimi na yeye tukishirikiana kwa pamoja ile barabara itajengwa kwa kiwango cha lami na ninajua Serikali imeipangia fedha kwa ajili ya ujenzi utakaoanza hivi karibuni. Ahsante sana.