Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya maji katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. MARTHA F. MARIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nampongeza Naibu Waziri wa Maji kwa kutoa majibu mazuri, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imekuwa ikitenga pesa nyingi sana kwenda katika miradi mbalimbali katika Mkoa wetu wa Katavi na miradi hiyo huonekana kwamba haikidhi kutokana na ongezeko kubwa la watu katika Mkoa wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda. Je, ni lini Serikali itatoa maji kutoka chanzo cha uhakika cha Ziwa Tanganyika ili kukidhi mahitaji ya maji ya watu katika Mkoa wetu wa Katavi hususan Mji wa Mpanda ambao unaongezeko kubwa sana la wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kutokana na Serikali ilitenga fedha nyingi sana kwenda katika Mradi wa Mamba katika Wilaya ya Mlele, Jimbo la Kavu na mradi huo umekamilika, lakini mradi huo umekamilika kwa kuacha baadhi ya vijiji vingi sana kupata maji. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari sasa kuja kufanya ziara katika Mkoa wetu wa Katavi, kujionea jinsi gani Serikali imetenga pesa nyingi, lakini mradi huo umeonekana uko chini ya kiwango kwa baadhi ya vijiji vingi sana kutokupata maji? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martha Lugangira, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Swali lake la kwanza, lini Serikali itatumia Ziwa Tanganyika kupelekeka maji katika Mji wa Mpanda na Mkoa wa Katavi? Wizara imeshakamilisha usanifu wa miradi yote mikubwa ambayo itatokana na maziwa yetu makuu, ikiwemo Ziwa Tanganyika. Hivyo, kwa mwaka ujao wa fedha tunatarajiwa kuanza kazi hizi endapo kadri namna ambavyo tutakuwa tunapata fedha ndivyo namna ambavyo miradi hii ya Maziwa Makuu itakuwa inatekelezwa. Hivyo, hata kwa Mkoa wa Katavi nao tutauangalia kwa jicho la kipekee kabisa kwa umuhimu wake na niendelee kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge kutoka Mkoa wa Katavi hasa Mheshimiwa Martha akiwa Mbunge wa Viti Maalum ameweza kuwajibika mara nyingi sana kufuatilia suala hili na sisi kama Wizara hatutamwangusha Mheshimiwa Martha pamoja na Wabunge wote wanaotoka ukanda ule.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili anasema mradi umekamilika lakini baadhi ya maeneo maji hayatoki, anatamani mimi niweze kufika huko. Nimwahidi Mheshimiwa Mbunge mara baada ya Bunge hili la Bajeti, tutapanga pamoja ratiba ambayo itakuwa rafiki kwetu sote ili niweze kufika Mpanda nijionee na kabla ya mimi kusubiri hadi Mwezi Julai huko, nitaagiza wahusika pale tuna Managing Director wa Mamlaka ya Maji.

Mheshimiwa Spika, lakini vilevile tuna RM wa pale, nitawaagiza waanze kufuatilia ili mpaka mimi nitakapokuwa naelekea huko kwa ajili ya ziara ikiwezekana wawe wameshafanya marekebisho na maji yaweze kutoka. (Makofi)