Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itazikarabati barabara za Jimbo la Mwibara ambazo zimeharibika sana ili kuruhusu mawasiliano kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:- Kwa kuwa barabara za Bugoma kwenda Mchigondo barabara ya Igundu kwenda Bulomba na barabara ya kutoka Mranda kwenda Mwiliruma hazipitiki kabisa kwa muda mrefu.

Je Serikali iko tayari kutengeneza barabara hizo kwa kutumia hata mfuko wa maafa?

Mheshimiwa Spika, kwa vile kuona ni kuamini yaani seeing is believing je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari baada ya kikao hiki tuongozane nae ili akajionee mwenyewe hali ilivyo katika Jimbo la Mwibara?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara hizi ambazo Mheshimiwa Kajege amezitaja katika Jimbo la Bunda zimeharibika kufuatia mvua nyingi sana ambazo zimeendelea kunyesha kote nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mpango muhususi wa kwenda kuhakikisha barabara hizi ambazo zimeharibiwa na mvua na hazipitiki zinatengenezwa mapema iwezekanavyo ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kusafirisha lakini na kusafiri katika huduma mbalimbali za kiuchumi, na kijamii. Kwa hiyo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutahakikisha katika mpango uliopo tunatoa kipaumbele cha hali ya juu katika barabara hizi zilizopo katika Jimbo la Mwibara.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais TAMISEMI tuko tayari wakati wowote kushirikiana na Waheshimiwa Wabunge na kufuatana nao katika majimbo hayo ili tuendelee kuwahudumia wananchi. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Kajege kwamba niko tayari baada ya kikao hiki tutapanga tuone ratiba nzuri ya kwenda katika Jimbo lake ili kuendelea kuwahudumia wananchi.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itazikarabati barabara za Jimbo la Mwibara ambazo zimeharibika sana ili kuruhusu mawasiliano kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika Ahsante sana kwa kuniona changamoto ya barabara katika Jimbo la Mwibara ni sawasawa kabisa na changamoto za barabara katika Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa. Kumekuwa na changamoto kubwa sana na barabara ya kutoka Iringa Mjini kuelekea Kata za Muhota na Magulilwa kutoka Kijiji cha Kitayawa kwenda Nyabula ambako kuna Hospitali ya Misheni ambako wananchi wanatibiwa barabara imekatika kabisa haipitiki imekatika daraja limekatika.

Je! Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa jimbo hili la Kalenga hususani wale wale wa…

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, taarifa kidogo.

MHE. GRACE V. TENDEGA: …Kata ya Mpota wanaweza wakapata mahitaji ya barabara.

SPIKA: Taarifa ya nini yuko wapi anayesema taarifa?

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Samahani unjuka ndio unaotusumbua Kiswaga hapa. (Kicheko/Makofi)

SPIKA: Ndio Mheshimiwa Kiswaga!

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Ni unjuka tu unatusumbua lakini kama unaniruhusu nitasema neno moja.
(Kicheko)

SPIKA: Karibu nakuruhusu.

T A A R I F A

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA, Mheshimiwa Spika, ahsante sana hiyo barabara ya kutoka Kitayao kwenda Nyabula tayari nimeshafanya mpango nimeongea na TARURA na sasa tumeshaweka mabomba hilo daraja linaanza kujengwa hivi karibuni ahsante sana tulipata fedha ya dharula nakushukuru. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Grace Victor Tendega unapokea hiyo taarifa? Halafu tuendelee na swali lako lipi sasa baada ya taarifa hiyo.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, kwa uchungu kabisa ninazungumza hapa sipokei taarifa hiyo wananchi wale wanapata shida sana hakuna chochote anachokisema kimefanyika pale barabara imekatika na wananchi awapati huduma kwa hiyo naomba swali langu lijibiwe. (Makofi)

Ni lini Serikali itahakikisha wananchi hawa wanapata huduma ya barabara waweze kupata huduma zingine na matibabu na kiuchumi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Kiswaga Mbunge wa Jimbo la Kalenga kwa juhudi kubwa sana anazozifanya kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Kalenga wanapata barabara bora na hivyo wanaendelea na shughuli za kiuchumi na kijaamii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nisema barabara hii ya kutoka Iringa Mjini kwenda Kata ya Maguliwa na maeneo haya kuna hospitali Serikali imeendelea kuhakikisha inatoa kipaumbele kwenye barabara ambazo zinapeleka huduma za jamii kwa wananchi, zikiwemo hospitali, shule na maeneo mengine yenye huduma za kijamii.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotanguliwa kusema tumepata baraka ya mvua mwaka huu, lakini tunafahamu baraka hiyo imeambatana na uharibifu wa baadhi ya madaraja, ma-calvati na barabara zetu. Naomba nimuhakikishie kwamba Serikali inaendelea kuweka mipango ya haraka ikwezekanavyo kuhakikisha barabara ile aliyoisema inakwenda kutengenezwa na hilo daraja lifanyiwa matengenezo ili wananchi waweze kupita na kupata huduma hizo za afya na huduma nyingine. Kwa hiyo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge jambo hilo linafanyiwa kazi na Serikali.