Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Kijiographia Tanzania ipo kwenye ukanda wenye mvua za kutosha:- Je, Serikali imejizatiti vipi kuhamasisha zoezi la uvunaji wa maji ya mvua kwa matumizi ya wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ambayo kwa kweli yanatia Faraja, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ukurasa wa 150 Ibara ya 100 imeweka bayana kwamba, tunataka tupeleke maji vijijini kwa asilimia 85 lakini mijini kwa asilimia 95. Na kinachoonekana hapa kinakosekana ni elimu kwa wananchi, je. Wizara iko tayari sasa kuja na mpango Madhubuti wa kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi ili wawe na utaratibu huu mzuri wa kuvuna maji? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa, maji yanapotiririka yanaharibu miundombinu kwa kiasi kikubwa na mara nyingi ni miundombinu ya barabara, reli lakini pia wakati mwingine na mabwawa na scheme za umwagiliaji. Na kwa mfano, katika eneo la Kongwa mara kadhaa tumeona kwamba, barabara inasombwa na maji lakini pia, kule katika Mto Mkondoa eneo la Kilosa, reli mara kadhaa inasombwa na maji. Sasa kwa nini Serikali isije na mkakati mahsusi wa kuhakikisha kwamba, tunakuwa si tu, na mabwawa machache lakini tutafute mabwawa mengi nchi nzima ambayo yatakuwa yanazuia maji ambapo maji haya yatatumika kwa matumizi ya kunywa lakini pia, kwa ajili ya matumizi ya kilimo? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Ilani inatutaka kufika mwaka 2025 vijijini kote maji yawe yamefika kwa asilimia 85 na maeneo ya Miji kwa asilimia 95. Wizara inaendelea kutekeleza Ilani kwa ufasaha sana na maelekezo ya Mheshimiwa Waziri wetu wa Maji ni kwamba, maji haya ya mvua kwetu sisi tunayachukulia kuwa ni fursa na sio laana. Hivyo, nipende kumwambia Mheshimiwa Shangazi kwa umahiri alionao, Wabunge wote humu ndani tunafahamu umahiri wa Mheshimiwa Shangazi vile ni Mwenyekiti wa Simba Sports Club humu Bungeni. Lakini vile vile, ni Katibu wetu sisi Wabunge tunaotokana na Chama Cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ninafahamu tutaendelea kushirikiana lakini Wizara tutaendelea kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi namna bora ya uvunaji wa maji katika makazi yetu na kama Wizara ya Maji, tutaendelea kushirikiana na Wizara ya TAMISEMI, ili tuweze kuunganisha nguvu ya pamoja kuona wananchi tunawapa elimu, namna bora ya kufanya design, namna pale wanapojenga makazi yao. Kwasababu, mvua hizi tukiweza kufanya ni zoezi la shirikishi, maji yatakuwa ni mengi.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hata kwenye mashule yetu kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi tutahakikisha na wao tunaendelea kutoa elimu kwa wakuu wa shule, ili kuona hata kwenye mashule yetu, watoto wasiendelee kuteseka. Maji hayana sababu ya kwenda kuharibu miundombinu mingine ambayo tunahitaji katika maisha yetu ya kila siku na maji haya tuweze kwenda kuyatumia vyema. Lakini vile vile, tutaendelea kuona namna bora ya kupata matenki ya bei nafuu kwa maeneo ya vijijini, ili ikiwezekana basi maji haya yaweze yakavuliwa kwa ushiriki wa pamoja na isije ikapelekea tena kuwa ni gharama kwa mwananchi mmoja mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, na katika swali lake la pili, kama Wizara nipende tu kusema nimepokea ushauri huu tutaendelea kuufanyia kazi Mheshimiwa Shangazi tutaonana, ili tuweze kuendelea kushauriana vema na Wizara tutakwenda kutekeleza vema. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Kijiographia Tanzania ipo kwenye ukanda wenye mvua za kutosha:- Je, Serikali imejizatiti vipi kuhamasisha zoezi la uvunaji wa maji ya mvua kwa matumizi ya wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, katika Wilaya ya Ngorongoro, Mkoa wa Arusha kuna mradi mkubwa wa maji wa vijiji (8) maarufu kama Mradi wa Magehe, mradi huu unagharimu bilioni 8, upembuzi yakinifu umeshafanyika kilichobaki ni utekelezaji tu. Nilitaka kufahamu ni lini Serikali itatekeleza mradi huu mkubwa kwa wananchi wa Ngorongoro?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara imezingatia mradi huu wa maji wa Magehe kwa umuhimu wake na tunaona kabisa ni mradi mkubwa ambao utakwenda kugharimu Serikali shilingi bilioni 8. Nikutoe hofu Mheshimiwa Catherine namna ambavyo umeweza ukafatilia suala hili muda mrefu na umekuwa ukiliuliza mara kwa mara kwangu pamoja na kwa Mheshimiwa Waziri, tutatekeleza mradi huu kwa awamu katika mwaka wa fedha ujao.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Kijiographia Tanzania ipo kwenye ukanda wenye mvua za kutosha:- Je, Serikali imejizatiti vipi kuhamasisha zoezi la uvunaji wa maji ya mvua kwa matumizi ya wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini liko juu ya Bonde la Ufa na vijiji vingi sana havina maji, ni kwasababu ya Bonde la Ufa. Na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, alifika wakati wa kampeni na kuahidi vijiji vile vitapata maji kutoka kwenye Ziwa la Madunga, Je. Mheshimiwa Waziri, lini ahadi ya Mheshimiwa Rais itatimizwa kwa wananchi hawa kupata maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge suala hili kama tulivyokubaliana, tunaliingiza kwenye mpango mkakati wetu wa mwaka wa fedha 2021/2022 na mradi huu utaaanza utekelezaji wake mara moja mara baada ya Mwaka wa Fedha mpya kuanza.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Kijiographia Tanzania ipo kwenye ukanda wenye mvua za kutosha:- Je, Serikali imejizatiti vipi kuhamasisha zoezi la uvunaji wa maji ya mvua kwa matumizi ya wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Kwanza kabisa, nimshukuru Waziri na Naibu Waziri wake kwa namna ya kipekee kabisa, kwa namna ambavyo wananipa ushirikiano. Mheshimiwa Rais, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli alipokuja kwenye ziara ya kuomba kura, alisema atahakikisha anachagua Waziri ambaye anawaza nje ya box na hakika watu hawa wanafanya hivyo. Sasa swali langu, nawashukuruni pamoja na kunipa mabwawa manne, lakini nataka kujua sasa, ni lini ujenzi huo wa hayo mabwawa utaanza? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, mabwawa haya manne yatajengwa kwa nyakati tofauti kulingana na fedha tutakavyokuwa tunazipata, ninaamini Mheshimiwa Mbunge wewe ni shahidi mzuri pale Chemba tumepatendea haki sana, hivi majuzi tu tumetoka kuchimba visima na hata haya mabwawa tunakuja kujenga mwaka ujao wa fedha lakini tutaanza kwa awamu taratibu mpaka kuhakikisha mabwawa yote yanakamilika. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Kijiographia Tanzania ipo kwenye ukanda wenye mvua za kutosha:- Je, Serikali imejizatiti vipi kuhamasisha zoezi la uvunaji wa maji ya mvua kwa matumizi ya wananchi?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa swali niulize swali dogo la nyongeza. Natambua Wizara imetupa mradi mkubwa wa maji kutoka Nkome kwenda Nzela Rwezela lakini nilitaka kuuliza swali dogo. Tunayo Kata ya Rubanga haina kabisa mfumo wa maji na kina mama wanatembea umbali wa kilometa 10 kupata maji katika Kijiji cha Mwamitilwa, Mtakuja, Ludenge, Je. Serikali haioni umuhimu wa kunipatia angalau visima viwili viwili katika vijiji hivyo vitano? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Kata ya Rubanda, Serikali inafahamu umuhimu wa kuleta visima na kama nilivyoongea na wewe Mheshimiwa Musukuma, wewe ni Mbunge ambaye umefatilia suala hili kwa karibu, tayari tumekutengea visima viwili vya kuanzia katika mwaka wetu wa fedha ujao. (Makofi)