Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Katika Jimbo la Segerea kuna zahanati kumi lakini hakuna zahanati moja iliyopandishwa hadhi kuwa kituo kikubwa cha afya chenye uwezo wa kulaza wagonjwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuipandisha hadhi Zahanati ya Tabata „A‟ kuwa Kituo cha Afya kwa sababu ina miundombinu yote inayofaa kwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 1

Vinguguti ina wakazi wengi na mpaka sasa hivi Kata ya Vinguguti haina zahanati yoyote.
Swali la Pili, kwa kuwa Kata ya Kipawa, Kata ya Minazi mirefu, Kata ya Kiwalani pamoja na Kata ya Kisukuru na Kimanga zina matatizo kama haya haya. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inashirikiana na Manispaa ya Ilala ili Kata hizi ziweze kuwa na zahanati lakini pia tuweze kuwa na vituo vya afya ili kuondoa msongamano katika Hospitali ya Amana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, Vinguguti kweli ni eneo ambalo lina wakazi wengi sana na kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge ni kweli kwamba eneo hili lazima lipatiwe kipaumbele. Lakini naomba nimwombe Mheshimiwa Mbunge japokuwa juhudi kubwa zinafanyika needs assessment wakati mwingine zinaanza katika Mabaraza yetu ya Madiwani.
Kwa hiyo, kwa sababu nia yako ni njema na Serikali tutakuunga mkono katika eneo hilo. Lakini kikubwa zaidi tutaweka nguvu zaidi katika lile eneo letu la Kituo cha Afya cha Mnyamani, kwa sababu ni eneo ambalo wenzetu wa Plan International walifanya juhudi kubwa sana kujenga kituo kile, jukumu letu kubwa ni kwamba kwanza kuwekeza vya kutosha kituo kile angalau kiweze kua-accommodate hii demand iliyokuwepo hivi sasa, wakati huo tukiangalia mtazamo wa mbali jinsi gani tutafanya, eneo lile la Vinguguti tuwe na sehemu ya kujenga zahanati kubwa na siyo zahanati kwa hadhi ya Vingunguti, kujenga moja kwa moja kituo cha afya kutokana na mahitaji ya idadi ya watu waliokuwa katika maeneo yale.
Mheshimwa Spika, eneo la Kipawa, Kiwalani na maeneo haya ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyasema ni kweli, ukiangalia yana sifa zinazofanana na maeneo ya Vingunguti kwamba watu ni wengi.
Mheshimiwa Spika, naomba nisema kwamba mimi nipo radhi kabisa kukutana na Mheshimiwa Mbunge kubadilishane mawazo, kwamba tutafanya vipi na kwa sababu nikijua Halmashauri ya Manispaa ya Ilala wana mikakati mikubwa sana ya ujenzi wa sekta afya ukiangalia demand ya sasa hivi iliyokuwepo hivi sasa hospitali yetu ya Amana inazidiwa, hata Hospitali ya Taifa ya Muhimbili idadi ya wagonjwa imekuwa wengi, ni kwa sababu katika ngazi ya chini tunakosa facilities za kuwasaidai wananchi kiasi kwamba kila mngojwa anaona kwanza aende Hospitali ya Taifa.
Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI jukumu letu kubwa ni kwamba katika mpango unaokuja tuhakikishe tufanye kila liwezekanalo. Huduma ya afya tuipeleke chini zaidi kupunguza ile referral system inayoenda juu ili kuhakikisha hospitali zetu za ngazi za juu ziweze kupata fursa nzuri zaidi.
Mheshimiwa Spika, hili kwa sababu Waziri wa Afya kesho ata-table bajeti yake hapa, tutaona mipango mipana katika Wizara Afya ambayo ina lenga moja kwa moja kutatua tatizo la suala la afya katika jamii yetu.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONNAH M. KALUWA aliuliza:- Katika Jimbo la Segerea kuna zahanati kumi lakini hakuna zahanati moja iliyopandishwa hadhi kuwa kituo kikubwa cha afya chenye uwezo wa kulaza wagonjwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuipandisha hadhi Zahanati ya Tabata „A‟ kuwa Kituo cha Afya kwa sababu ina miundombinu yote inayofaa kwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 2

changamoto kubwa ya zahanati hizi katika Jimbo la Segerea na Manispaa ya Ilala ni maeneo lakini wapo watu wanaoishi jirani na maeneo hayo, wapo tayari kutoa maeneo yao kwa ajili upanuzi wa maeneo ya zahanati hizi.
Je, Serikali ipo tayari kusaidiana na Halmashauri ya Ilala kulipa fidia kwa ajili ya kuongeza ukubwa wa maeneo ili kupata zahanati na vituo vikubwa vya afya katika maeneo ya Jimbo la Segerea na Manispaa ya Ilala kwa ujumla?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kama nilivyosema katika jibu letu la awali, mahitaji ya afya hapa yamekuwa ni changamoto kubwa sana, nilipofanya reference tulipokuwa na Mbunge wa Segerea kipindi kilichopita, alipokuwa na timu iliyoenda eneo la Vingunguti katika machinjio yale, vilevile akaja katika ofisi yangu kuona jinsi gani tutafanya, licha ya suala la machinjio lakini wananchi wana changamoto ya afya.
Mheshimiwa Spika, mimi naamini hayo mawazo ni mazuri, tutakaa vizuri kubadilishana mawazo ili tuone ni jinsi gani tutafanya ujenzi wa zahanati au kituo cha afya maeneo yaweze kupatikana. Lengo kubwa ni kwamba kina mama na watoto wa maeneo yale waweze kupata huduma kama wengine.
Mheshimiwa Spika, ajenda yetu kubwa ni kuhakikisha kwamba hospitali zetu za rufaa sasa tupunguze idadi ya wagonjwa siyo mtu anaumwa mguu mpaka aende Muhimibili au Amana haiwezekani hata kidogo. Lazima tuhakikishe mfumo mzuri unatengenezwa katika sekta ya afya katika ngazi za chini kusaidia sekta za juu ziweze kufanya huduma kubwa zinazohitajika.