Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Urambo ilijengwa mwaka 1975. (a) Je, Serikali iko tayari kuifanyia ukarabati wa majengo na miundombinu yake yote? (b) Je, ni lini Serikali itabadilisha mashine ya X-ray ya Hospitali hiyo ambayo imepitwa na wakati?

Supplementary Question 1

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, bado hali ya Urambo ni mbaya kuhusu upimaji wa afya ya akinamama na watoto kwa kuwa X- ray ni mbaya. Na wakati huohuo, pamoja na jitihada nzuri ya kupata ultrasound mbili, bado ultrasound hizo hazina watumishi, zimekaa bure. Kwa hiyo, sasa kwa kuwa hakuna X-ray kama alivyojibu Mheshimiwa Waziri, ultrasound tumejitahidi tumepata mbili, hazina watumishi. Je, lini Serikali italeta watumishi wawili angalau zile ultrasound zianze kupima akinamama na watoto? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na nia nzuri ya Serikali yetu ya kutujengea kituo cha afya Mlimani katika Kata ya Uyumbu, jengo la akinamama na watoto linakaribia kuisha lakini limepungukiwa milioni 100. Suala hili tulizungumzia Mheshimiwa Waziri mhusika alipokuja kutembelea, Mheshimiwa Dkt. Festo, bado ile hospitali inahitaji kumaliziwa jengo. Je, lini Serikali itatuletea milioni 100 ambazo tumekisiwa zimalize ili wodi ya akinamama ianze kutumika badala ya sasa wanakwenda mbali kwa lengo la kujifungua? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameuliza na ameomba hapa kwamba walau wapelekewe watumishi wawili katika maeneo ambayo tumepeleka ultrasound na X-ray katika Wilaya yake ya Urambo. Nimhakikishie kabisa kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto tumekubaliana kwamba Waziri husika anaendelea kufanya utafiti na kuhakikisha ndani ya kipindi hiki kifupi wanapeleka mtaalam katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, commitment ya fedha ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya kumalizia jengo lililoko katika Jimbo la Urambo ambayo inahitajika kuhakikisha hilo jengo linaanza kutumika kwa wakati. Nimhakikishie kabisa kwamba nimewasiliana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ameniagiza kwamba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutapeleka wataalam wetu wakaangalie hiyo tathmini na baada ya hapo tutatoa majibu ya msingi kuhakikisha hilo jengo linakwisha na linaanza kutumika. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Urambo ilijengwa mwaka 1975. (a) Je, Serikali iko tayari kuifanyia ukarabati wa majengo na miundombinu yake yote? (b) Je, ni lini Serikali itabadilisha mashine ya X-ray ya Hospitali hiyo ambayo imepitwa na wakati?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi, japokuwa ntaendelea kubakia kuwa mwananchi mtiifu wa Jangwani, na chini ya GSM naamini kwamba tutavuka salama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja katika Jimbo la Kilombero na Mheshimiwa Job Ndugai akiwa Mjumbe wa Kamati Kuu alipokuja katika Jimbo la Kilombero, waliwaahidi wananchi wa Jimbo la Kilombero juu ya ujenzi wa Hospitali ya Jimbo la Kilombero. Namshukuru Mheshimiwa Waziri, dada yangu, Mheshimiwa Ummy, ametuahidi kwamba tutapata milioni 500 za kuanza ujenzi huu.

Mheshimiwa Spika, swali langu; je, ni lini ujenzi huu utaanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kabisa katika bajeti inayokuja ya mwaka 2021/ 2022, Serikali imehakikisha kuanza hospitali mpya katika halmashauri zote nchini ambazo hazina hospitali za wilaya.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Urambo ilijengwa mwaka 1975. (a) Je, Serikali iko tayari kuifanyia ukarabati wa majengo na miundombinu yake yote? (b) Je, ni lini Serikali itabadilisha mashine ya X-ray ya Hospitali hiyo ambayo imepitwa na wakati?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, natambua mchango wa Serikali kwa kupeleka fedha kwenye ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Nkasi lakini kilio cha Wanankasi ilikuwa ni kupata huduma kwa level ya Wilaya. Mpaka sasa jengo lipo lakini huduma inayotolewa hailingani na huduma inayotakiwa kutolewa katika Hospitali ya wilaya.

Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba pamoja na madaktari kulingana na level ya Wilaya?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa katika eneo lake kuna jengo ambalo bado kutumika kwasababu ya vifaa tiba. Na hilo nimwambie tu kabisa kwamba mimi kabla sijafika hapa nilikuwa nazungumza na Waziri anayehusika na Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, na katika bajeti yake ambayo tutakwenda kuipitisha, kuna fungu ambalo tumetenga kwa ajili ya kununua vifaa na vifaa tiba kwa ajili ya hospitali zote ambazo majengo yake yako tayari lakini hayajakamilika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tukishapitisha bajeti, ninaamini kabisa kwamba mara baada ya Bunge hili na mara baada ya bajeti kupita, basi hivyo vifaa na vifaa tiba vitatengwa na kupelekwa. Suala la watumishi basi tutaendelea kutenga kulingana na vibali vya ajira ambavyo tunapatiwa na Serikali. Ahsante.