Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI Aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kuwa na Mtaala mmoja kuanzia Kidato cha Kwanza hadi cha Nne kati ya Tanzania Bara na Zanzibar? (Makofi)

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, nina swali moja dogo la nyongeza:

Mheshimiwa Spika, kwa vile sasa Wizara ipo kwenye mchakato wa kukusanya maoni ya kurekebisha mtaala. Je, Serikali haioni sasa kuwa ipo haja ya kuweka mtaala mmoja wa elimu ya msingi kati ya Tanzania Bara na Zanzibar? (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Maryam nakupa nafasi tena, sasa uulize swali lako ukiniangalia, usipige chabo. (Kicheko)

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kwa vile Serikali sasa ipo kwenye mchakato wa marekebisho ya mtaala. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja sasa ya kuweka mtaala mmoja wa elimu kati ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Bara? (Makofi/ Kicheko)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwa upande wa Elimu ya Msingi kuna tofauti ya mitaala kati ya Tanzania Bara na Visiwani. Kwa sababu kwa upande wa Tanzania Bara tunawapeleka watoto shule miaka saba kwa upande wa shule za msingi, lakini kwa wenzetu wa Tanzania Zanzibar wao wanakwenda kwa kipindi cha miaka sita. Kwa hiyo kuna utofauti wa namna hiyo.

Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na nilitaarifu tu Bunge lako Tukufu kwamba, Taasisi yetu ya Elimu Tanzania (TET) na ile ya Zanzibar (ZIE) zinafanya kazi kwa karibu sana kuhakikisha kwamba utekelezaji wa mitaala unakwenda sawasawa lakini na majadiliano ya karibu kuhakikisha kwamba changamoto zote zinazotokea kwenye utekelezaji wa mitaala zinapatiwa ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, ni kweli pasipokuwa na shaka kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeanza sasa kufanya mapitio ya Sera ile ya Elimu ya Zanzibar ya mwaka 2016 na wataangalia sasa namna gani tunaweza kuhusianisha miaka hii ya Elimu ya Msingi kuhakikisha kwamba tunakwenda sawasawa.

Mheshimiwa Spika, kama tunavyofahamu kwamba tuna mjadala mpana wa kitaifa kuhakikisha kwamba mwenendo au mfumo wa elimu yetu uwe vipi.

Kwa hiyo, katika majadiliano haya tunaamini changamoto hizi zote anazozungumza Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge humu ndani zinaenda kupata ufumbuzi ikiwemo na hili la kuwa na mtaala mmoja kuanzia Elimu ya Msingi.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)