Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Hungumalwa - Ngudu hadi Magu kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, mbali na majibu mazuri ya Serikali, kwa kuwa swali hili limeulizwa kwa muda mrefu, kuanzia katika Mkutano wa Tatu, ambapo Mheshimiwa Kiswaga na mimi Mbunge wa Sumve tuliuliza na tukapata majibu ya namna hii hii.

Je, Serikali haioni sasa umefika wakati wa kulifanyia kazi jambo hili na kuanza taratibu za manunuzi ili barabara hii ijengwe? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa ujenzi wa barabara hii unaendana sambamba/unaathiriana na ujenzi wa reli ya kiwango cha standard gauge kutokea Isaka kwenda Mwanza kwa sababu, barabara hii kwa usanifu mpya inapita eneo tofauti na barabara iliyopo inapita na reli hii ikishajengwa, ina maana hakutakuwa na njia tena ya kupita kutoka Kwimba kwenda Magu.

Je, Serikali haioni sasa umefika wakati iharakishe ujenzi wa barabara hii, ili kuepuka kufunga njia ya kutoka Kwimba kwenda Magu? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasalali Mageni, Mbunge wa Sumve kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, Serikali imetenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa barabara hii tuliyoitaja kwa kiwango cha lami. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii itajengwa na sisi kwa upande wa Wizara tayari tumeshakamilisha taratibu zote ili fedha itakapopatikana basi tuanze utaratibu wa kuanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa suala la barabara hii aliyoitaja kuingiliana na reli hii ya kisasa ya SGR, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, yote hayo yalizingatiwa kwenye usanifu na kwa hiyo, tumuhakikishie kwamba, hakutatokea hiyo changamoto anayoisema kati ya muingiliano wa hizo barabara na hiyo reli. Cha msingi tu avute subira kwamba wakati reli imeshaanza kujengwa hiyo ya SGR kati ya Isaka na Mwanza, lakini fedha ikipatikana mara moja pia barabara hii itajengwa ili basi hii miundombinu yote iende sambamba kuyafungua hayo maeneo. Ahsante. (Makofi)