Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano ya ujenzi wa barabara za lami katika Mji wa Bunda kwa kuwa mpaka sasa hauna barabara za lami?

Supplementary Question 1

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ahadi ambazo Hayati Dkt. Magufuli aliahidi wakati wa kampeni ilikuwa ni pamoja na kujenga soko kuu la Mji wa Bunda pamoja na stendi mpya.

Je, kati ya stendi na soko kuu, ahadi hii yenyewe itatekelezwa lini? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKO ANA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Robert Chacha Maboto, Mbunge wa Bunda Mji kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba hapa nimeelezea kwa chini kwamba Serikali inaendelea na mazungumzo na Benki ya Dunia kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa TACTIC, uendelezwaji wa miundombinu katika miji yetu. Na ule uendelezaji wa miundombinu kwenye TACTIC haihusu barabara peke yake, ni pamoja na masoko, stendi, madampo ya taka yaani tunatengeneza mji kuwa wa kisasa. Kwa hiyo, hata hiki anachokizungumza kuhusu soko kuu pamoja na stendi mpya katika Mji wa Bunda nafikiri itakuwa ndani ya package katika mradi huu wa TACTIC ambao mara utakapotekelezeka ni sehemu ya huo mradi, ahsante sana.

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano ya ujenzi wa barabara za lami katika Mji wa Bunda kwa kuwa mpaka sasa hauna barabara za lami?

Supplementary Question 2

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, sambamba na hilo swali la Mheshimiwa Robert Maboto nauliza je, ni lini Serikali itakamilisha lami kutoka Kinesi yaani Wilaya ya Rorya inayounganisha kutoka Rorya mpaka Tarime ambayo pia ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa wetu Hayati Magufuli? (Makofi)

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi za viongozi wetu wakuu tutaendelea kuzitekeleza kulingana na fedha itakavyopatikana ikiwa ni pamoja na hiyo barabara ya kutoka Rorya hadi Kinesi, ahsante.