Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ K.n.y. MHE. MOHAMED L. MONNI Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga stendi katika Mji wa Chemba ambao unakuwa kwa kasi?

Supplementary Question 1

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake, lakini kwa kuwa Mheshimiwa Rais alishatoa ahadi wakati wa kampeni mwaka 2020 na Mheshimiwa Naibu Waziri amezungumza kwamba ni mradi wa kimkakati.

Je, kwa kuwa ilikuwa ni ahadi ya Rais, Serikali inatoa tamko gani kuhusiana na jambo hili? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi stendi ya Chema ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na ahadi zote za viongozi zinatekelezwa kwa kadri ya upatikanaji wa fedha na mipango inavyoandaliwa. Na katika jibu langu la msingi nimewaelekeza Halmashauri ya Chemba waandae andiko rasmi ambalo litawezesha sasa Serikali kuanza kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo wa kimkakati, lakini pia ambao pia ni ahadi ya viongozi wetu wa Kitaifa.

Kwa hiyo, niombe watekeleze utaratibu huo na Serikali iweze kuona namna ya kuanza kutekeleza mradi huu. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ K.n.y. MHE. MOHAMED L. MONNI Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kujenga stendi katika Mji wa Chemba ambao unakuwa kwa kasi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Bunda ni Halmashauri inayokua lakini pia ina route nyingi za usafiri ikiwepo kwenda Arusha, Mwanza na maeneo mengine, lakini stendi yake ni mbaya sana.

Ni lini sasa Serikali mtatusaidia hasa Halmashauri yetu changa kutujengea stendi ya kisasa na hasa ukizingatia Mji wa Bunda unakua? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Bunda ni Mji ambao unakua, una muingiliano mkubwa wa kibiashara, lakini pia una muingiliano wa magari yanayokwenda katika Mikoa mbalimbali, kwa hiyo, una kila sifa ya kupata stendi ya kisasa na mimi nichukue nafasi hii kwanza kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inalitambua hilo, lakini Serikali inalitambua hilo lakini Serikali ya Halmashauri kwa maana ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Halmashauri ya Bunda waanzishe utaratibu wa kufanya tathmini ya gharama ambazo zinahitajika kujenga stendi ile ili wawasilishe Serikalini na sisi tutafanya tathmini na kuona uwezekano wa kupata fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi ya Bunda. Nakushukuru. (Makofi)