Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH) aliuliza:- Baadhi ya miradi ya maji inayosimamiwa na Halmashauri imekuwa ikisuasua kutokana na uchache wa fedha pamoja na kuingia mikataba na wakandarasi wasiokuwa na uwezo wa kutosha na kusababisha miradi hiyo kutokamilika kwa wakati:- Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza tatizo la maji kwa wananchi wa vijijini?

Supplementary Question 1

RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali madogo mawili.
Kwa kuwa Wilaya ya Kilolo imezungukwa na mito ya Ruaha, Mto Rukosi; ni kwa nini Serikali isivute maji kutoka katika mito hiyo kuliko kuchimba visima ambavyo vimekuwa vikichimbwa, lakini havitoi maji?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa visima…
SPIKA: Hilo, swali la kwanza ulilouliza ni kwa niaba ya kaka au? (Kicheko)
Mheshimiwa endelea!
MHE. RITTA E. KABATI: Swali la pili, kwa kuwa visima virefu huwa havina uhakika sana wa kutoa maji na mara nyingi vimekuwa vikiharibika! Ni kwa nini Serikali isielekeze nguvu kwenye kuchimba mabwawa badala ya kutumia fedha nyingi sana katika kuchimba hivi visima ambavyo mara nyingi vimekuwa havina uhakika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKAL ZA MITAA): Mheshimiwa Spika, swali la kwanza lilikuwa ni kwa nini sasa tusitumie fursa za mito ambayo inapita katika Jimbo la Kilolo badala ya kwenda kuchimba visima virefu. Katika utekelezaji wa miradi ya maji, kwanza wataalam wanaangalia au wanafanya analysis, ni chanzo gani cha maji ambacho kitaweza kusaidia, lakini utafiti huo vilevile unaendana na bajeti.
Mheshimiwa Spika, kuna maeneo mbalimbali ambayo yamebainika kwamba kumeenda kuchimbwa visima virefu, lakini sehemu zingine kuna fursa za maji. Hili naomba nikiri hapa wazi kwamba, watu wengi mbalimbali hasa wa kutoka maeneo mbalimbali ambayo kuna mito mirefu au maziwa, kama watu wa Kanda ya Ziwa wanasema kwa nini tuchimbiwe visima badala ya kutumia vyanzo vilivyopo. Naamini katika Programu ya Maji ya Awamu ya Pili ambayo sasa inaanza, Watalaam wetu, wataangalia katika sehemu ambayo kuna fursa ya vyanzo vikubwa vya maji hasa mito viweze kutumika vizuri kutokana na bajeti iliyopo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mbunge kwamba katika Awamu ya Pili ya Mradi wa Maji, watalaam wetu wataenda mbali zaidi kuangalia fursa. Ndiyo maana tulisema pale awali kwamba maeneo yote yanayozungukwa na vyanzo vikubwa vya maji, basi watalaam itabidi wajielekeze huko kuona jinsi gani ya kufanya ilimradi kupata maji ya uhakika na kuhakikisha fedha inatumika vizuri.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni kwa nini sasa kuchimba visima virefu badala ya kuchimba mabwawa. Mara nyingi sana watalaam wanazungumza kwamba maji ya kisima kirefu, kitaaluma au kitalaam, ukiyatoa yanakuwa maji safi na bora, kwa sababu yanakuwa hayana contamination, lakini maji ya bwawa maana yake yanataka ufanye treatment.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, imeonekana wazi, sehemu zingine visima virefu kweli vimechimbwa, lakini hatukupata maji. Kwa sababu uhitaji wa maji ni mkubwa na sehemu zingine water table inasumbua sana, naamini sasa, ndiyo maana katika mkutano wetu wa pili tuliofanya tathmini pale Dar es Salaam, tulielekeza kila Halmashauri, ikiwezekana kila mwaka twende katika uelekeo wa mabwawa kwa sababu maeneo mengi mbalimbali tuliyochimba visima virefu ni kweli wakati mwingine tulikosa maji na wakati mwingine miradi hii inaharibika. Vitu hivi vyote vitakwenda sambamba kwa pamoja kuangalia engineering specifications ya maji inasemaje kwa ajili ya kuelekeza wananchi wapate maji bora na salama.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH) aliuliza:- Baadhi ya miradi ya maji inayosimamiwa na Halmashauri imekuwa ikisuasua kutokana na uchache wa fedha pamoja na kuingia mikataba na wakandarasi wasiokuwa na uwezo wa kutosha na kusababisha miradi hiyo kutokamilika kwa wakati:- Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza tatizo la maji kwa wananchi wa vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Naomba niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Waziri, Korogwe ilikuwa na mradi wa World Bank ambapo ilikamilisha miradi yake Kwa Msisi, Ngombezi na Kwa Mndolwa na ikabakiza mradi wa Rwengela Relini, Rwengela Darajani na Msambiazi. Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha miradi hiyo ambayo imebakia?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Spika, ni kweli Korogwe kuna mradi wa maji, lakini naomba nitoe maelezo kwamba si Korogwe peke yake isipokuwa kuna miradi ya maji mingi sana hivi sasa, hata Wabunge wengi wanaweza wakasimama. Miradi hii ni kwamba mingi ambayo wakandarasi walikuwa site, lakini baadaye wakafanya mpaka waka-demobilize vifaa kutokana na kushindwa kulipwa fedha. Nadhani hata mradi wa Korogwe ndiyo tulipata changamoto hiyo, lakini siyo mradi wa Korogwe peke yake isipokuwa ni miradi mingi.
Mheshimiwa Spika, ndiyo maana, tulipoanza katika Serikali ya Awamu ya Tano jukumu lake kubwa, lilikuwa ni kuangalia jinsi gani itakusanya fedha za kutosha. Wakati tunaingia tulikuwa na outstanding payment ambapo deni tunalodaiwa lilikuwa karibu bilioni 28, lakini kutoka na makusanyo mazuri yaliyofanywa hivi sasa deni lile lote limeshalipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naamini sasa hivi ukiangalia hata Waziri wa Fedha hapa atakapokuja katika bajeti yake ataeleza kwamba hivi sasa tuna uwezo hata certificate zikija watu wakaweza kulipwa. Kwa hiyo, mradi wa Korogwe sawasawa na miradi mingine ambayo imesimama. Naamini Halmashauri zingine hivi sasa watasema bado hawajapokea fedha, lakini mchakato huu sasa nawasisitiza Wakurugenzi wote na ma-engineer wote wa Wilaya, wale wakandarasi ambao certificate zao hazijapelekwa, haraka zipelekwe Wizara ya Maji ilimradi kuhakikisha kwamba, wakandarasi wanarudi site kazi ziweze kufanyika. Hii ni kutokana na umakini uliyofanyika katika ukusanyaji wa kodi. Hapa naomba niwasistize ndugu zangu Wabunge, wote tushikamane na Serikali yetu ili kodi ziweze kulipwa, miradi iweze kutekelezeka.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y. MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH) aliuliza:- Baadhi ya miradi ya maji inayosimamiwa na Halmashauri imekuwa ikisuasua kutokana na uchache wa fedha pamoja na kuingia mikataba na wakandarasi wasiokuwa na uwezo wa kutosha na kusababisha miradi hiyo kutokamilika kwa wakati:- Je, Serikali imejipanga vipi kumaliza tatizo la maji kwa wananchi wa vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Serikali ilikuwa inatekeleza mradi wa program ya maji kwa vijiji kumi kwenye Halmashauri mbalimbali nchini na kuna baadhi ya Halmashauri hawakufanikiwa kupata hata anagalau vijiji vitano. Je, Serikali iko tayari sasa kutuletea taarifa ya kina ikionesha Halmashauri moja baada ya nyingine na taarifa hiyo ikionesha ni miradi mingapi imefanikiwa kwa kila Halmashauri ili tuweze kujua?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, tulianza Programu ya Utekelezaji wa Miradi ya Maji mwaka 2006 na tumemaliza Awamu ya Kwanza mwaka 2015. Sasa hivi tumeanza Programu ya Pili ambayo imeanza mwezi Januari, 2015, kwa hiyo tunaendelea.
Mheshimiwa Spika, iko miradi ambayo hatukuikamilisha kwenye Programu ya Kwanza. Bajeti ambayo tumeitenga mwaka 2016/2017, itaanza kwanza kukamilisha ile miradi ambayo ilikuwa inaendelea, haijakamilika, lakini pili itaendelea na ile miradi ambayo imekuwa earmarked kwenye Programu ya Kwanza. Kwa hiyo, tutaingia mikataba na kuikamilisha, hiyo ndiyo Sera yetu tunaendelea namna hiyo, ikiwa ni pamoja na Jimbo la Mheshimiwa Mbunge. Pamoja na hilo ni kwamba tunayo orodha ya Wilaya zote, kwa hiyo, kama utahitaji upatiwe tutakapokuwa tumesoma bajeti Mheshimiwa Mbunge tutakupatia hiyo orodha.