Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU (K.n.y MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:- Mkandarasi wa REA anayefunga umeme katika Jimbo la Geita Vijijini amemaliza tatizo na yule anayeunganisha kutoka Sengerema yupo pole pole sana. Je, ni lini sasa Serikali itamsimamia kikamilifu mkandarasi huyo ili aweze kumaliza kazi hiyo na umeme uweze kuwashwa?

Supplementary Question 1

MHE. COSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninaomba nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika REA Second Phase ambayo ilikuwa inaendelea ni robo tu ya vijiji vya Jimbo la Geita na Geita Mjini ambavyo vimepata umeme, vijiji kama Nyawilimilwa, Kagu, Senga, Bulela bado havijafikiwa; naomba kujua ananipa uhakika gani kwamba Vijiji hivi ambavyo bado havijapata umeme vitapata umeme kwenye Awamu ya Tatu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Mji wa Geita tumekuwa na tatizo la umeme kukatika katika kila siku kutokana na umeme mdogo ambao tunatoka Mwanza. Hata mji wenyewe wa Geita pale Mjini umeme unakuta upo lakini sehemu nyingine hauwaki. Ni lini Mheshimiwa Waziri atahakikisha Geita inapata umeme wa uhakika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza kuhusu kujumuisha vijiji vya Nyawilie na Bulila nimhakikishie kwamba vijiji hivyo vyote vitaingia kwenye REA Awamu ya Tatu inayoanza Julai mwaka huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kukatika katika kwa umeme nichukue fursa hii kuwataarifu kwamba ni kweli kabisa karibu nchi nzima siyo Geita tu umeme bado unakatika katika na suluhisho la kukatika kwa umeme kama tulivyosema miji ya Geita na maeneo ya Kanda ya Ziwa pamoja na maeneo mengine, itapata sasa umeme wenye kilovoti 400 unaotoka North West Grid unaotoka Mbeya unaopita Sumbawanga, unaopita Mpanda, unaokuja Kigoma unakwenda mpaka Nyakanazi na baadaye Geita na umeme huo utatoka Geita kwenda Bulyanhulu na utatoka Bulyanhulu kwenda maeneo ya Biharamulo. Umeme huu utakuwa na nguvu kubwa ya kilovolt 400 na unatembezwa kwa takribani ya kilometa 1148.

Name

Joshua Samwel Nassari

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU (K.n.y MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:- Mkandarasi wa REA anayefunga umeme katika Jimbo la Geita Vijijini amemaliza tatizo na yule anayeunganisha kutoka Sengerema yupo pole pole sana. Je, ni lini sasa Serikali itamsimamia kikamilifu mkandarasi huyo ili aweze kumaliza kazi hiyo na umeme uweze kuwashwa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu linafanana sana na swali la muuliza swali Mbunge wa Geita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua jitihada ambazo zilifanywa na Serikali hapo nyuma kwa baadhi ya maeneo na vijiji kupata umeme kupitia Wakala wa Umeme vijijini kwa maana ya REA, lakini pia tunatambua mapungufu makubwa ambayo yameonekana kwenye miradi hii. Vipo baadhi ya vijiji ambavyo wananchi walipitiwa, ramani ikapitishwa, Serikali ikawaagiza wakakata mazao yao, wakakata kahawa…
MHE. JOSHUA S. NASSARI: Wakachimba mashimo na mashimo yakachimbwa na Serikali kupitia Wakandarasi waliopewa kazi kwa ajili ya kuwapa umeme, lakini badala yake Wakandarasi wameondoka watu hawajapata umeme, mashimo yamebaki, mazao yao yameanguka, ng‟ombe wanaanguka kwenye mashimo. Sasa ningetaka kauli ya Serikali kwamba ni kwa nini unamnawisha mtu unamuweka mezani halafu kama huwezi kumpa chakula, kwa hivyo ni lini wananchi hawa ambao tayari ramani zimeshapita kwao na mashimo yakachimbwa halafu yakaachwa na mazao yao yakakatwa, ni lini wanakwenda kufungiwa umeme? Vijiji hivyo ikiwa ni pamoja na Mulala, Kilinga pamoja na baadhi ya maeneo mengine?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kuna maeneo mengine mkandarasi ameendelea kuchimba mashimo na kuweka nguzo.
Sasa ni lini maeneo haya yatapatiwa umeme, jibu la uhakika kabisa ambapo Waheshimiwa Wabunge tumekuwa tukiwaambia kwamba REA Awamu ya Tatu inakuja kusambaza umeme kwenye vijiji vyote, REA Awamu ya Tatu inaanza mwezi Julai baada ya bajeti yetu kupita mwaka huu. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge ni kuanzia mwezi Julai miezi inayofuata maeneo yenye mashimo yatapatiwa umeme kuanzia mwezi wa saba mwaka huu mara baada ya bajeti yetu kupita.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. COSTANTINE J. KANYASU (K.n.y MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:- Mkandarasi wa REA anayefunga umeme katika Jimbo la Geita Vijijini amemaliza tatizo na yule anayeunganisha kutoka Sengerema yupo pole pole sana. Je, ni lini sasa Serikali itamsimamia kikamilifu mkandarasi huyo ili aweze kumaliza kazi hiyo na umeme uweze kuwashwa?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa dhumuni la REA Phase One ilikuwa ni kupekeka umeme kwenye kila makao makuu ya kata na kwa kuwa Kata ya Hemtoye, Mbaramo, Mbaru pamoja na kata ya Shagayu bado hazina umeme.
Je, ni lini Serikali itapelekea umeme katika maeneo hayo? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa napenda nisahihishe kidogo, siyo kweli kama Phase One ya REA ilikuwa inapeleka kata zote ni Kata chache. REA II pia ilichagua Mikoa na Kata na maeneo ya kati. Jibu la uhakika sasa kama alivyosema ni lini sasa atapewa, REA ya Awamu ya Tatu inayoanza mwezi wa saba ndiyo itakayopeleka umeme kwenye Vijiji vyote pamoja na vya Mheshimiwa Mbunge ambavyo havijapata umeme hadi sasa.