Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Hospitali ya Wilaya ya Olturumet katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kwa kuipatia jengo la OPD, Wodi ya kulaza Wagonjwa, Jengo la X-Ray na mashine ya X-Ray ili Hospitali hiyo iweze kutoa huduma kwa wananchi ipasavyo?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, na kutakuwa na maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuuliza, kwa kuwa suala la kupanuliwa kwa hospitali hiyo ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais kwa muda mrefu; je, hospitali hiyo iko kwenye idadi ya hospitali 21 zitakazokarabatiwa katika bajeti ya mwaka 2021/2022?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa, hospitali hiyo inatoa huduma kwa akina mama na watoto vijijini ambao hawana uwezo wa kupata huduma za afya kwenye hospitali binafsi ambazo ni gharama kubwa, je, Serikali sasa haioni ni wakati muafaka wa kuiweka hospitali hiyo kwenye bajeti ya mwaka 2021/2022 ili na yenyewe iweze kutoa huduma bora kwa wananchi wetu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUNGANGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Noah Mollel Mbunge wa Arumeru Magharibi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie kwamba ahadi zote za viongozi wetu wa Kitaifa ni kipaumbele katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Nimhakikishie kwamba hospitali hii ya Orturmet ni miongoni mwa hospitali ambazo zimepewa kipaumbele; na nimhakikishie kwamba katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 tumeanza na hospitali 21 awamu ya kwanza; na tutakuwa na awamu ya pili ya hospitali zile nyingine ambazo zinabaki. Nimhakikishie katika awamu hiyo ya pili hospitali hiyo ya Orturmet Arusha ni miongoni mwa hospitali ambazo zitaingizwa ili ziweze kufanyiwa upanuzi na ukarabati.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba hospitali hii inatoa huduma kwa wananchi vijijini na wengi wao ambao hawana uwezo na ndiyo maana Serikali imeendelea kuhakikisha kwamba inaingiza kwenye orodha hospitali ambazo zinapewa kipaumbele kwaajili ya ukarabati ili iendelee kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi katika maeneo hayo. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Noah kwamba jambo hilo linafanyiwa kazi na mara fedha zikipatikana hospitali hii itakarabatiwa ili iweze kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Hospitali ya Wilaya ya Olturumet katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kwa kuipatia jengo la OPD, Wodi ya kulaza Wagonjwa, Jengo la X-Ray na mashine ya X-Ray ili Hospitali hiyo iweze kutoa huduma kwa wananchi ipasavyo?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa, Kata ya Iyumbu ipo pembezoni na haina kituo cha afya wala zahanati katika vijiji vyake vyote, je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kituo cha afya katika Kata ya Iyumbu iliyopo Jimbo la Singida Magharibi ili kuwawezesha wananchi wake kupata huduma bora za afya na kuokoa vifo vya akina mama na Watoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUNGANGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aysharose Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tunafahamu pamoja na jitihada kubwa na kazi kubwa sana iliyofanywa na Serikali ya kujenga vituo vya afya, ambapo katika miaka mitano iliyopita zaidi ya vituo vya afya 490 vimejengwa bado kuna uhitaji wa vituo vya afya katika kata zetu mbalimbali kote nchini. Kwa hiyo katika eneo hilo Kata hii ya Iyumbu katika Mkoa wa Singida ni miongoni mwa kata ambazo kimsingi zina uhitaji wa kituo cha afya.

Mheshimiwa Naibu Spika na Mpango wa Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo ya Afya Msingi ni kuendelea kujenga vituo vya afya kwa awamu katika kata zetu kadri ya upatikanaji wa fedha. Mimi naomba nimhakikishie Mheshimiwa Aysharose kwamba tunachukua hoja hiyo, na kadri ya upatikanaji wa fedha tutaendelea kutoa kipaumbele katika Kata hii ili tuweze kujenga kituo cha afya na kuweza kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Hospitali ya Wilaya ya Olturumet katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kwa kuipatia jengo la OPD, Wodi ya kulaza Wagonjwa, Jengo la X-Ray na mashine ya X-Ray ili Hospitali hiyo iweze kutoa huduma kwa wananchi ipasavyo?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa hospitali ya Makandana wilaya ya Rungwe imeshajengewa wodi ya wanawake. Serikali ina mpango gani wa kutuongezea madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake katika hospitali ile?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUNGANGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeboresha miundombinu katika hospitali ya Wilaya ya Rungwe, hospitali ya Makandana kwa kujenga wodi ya wanawake ili kuendelea kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto katika Halmashauri ya Rungwe. Ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba bado Serikali ina mipango ya kuendelea kuboresha miundombinu hiyo ikiwemo kuongeza vifaatiba lakini pia kuongeza madaktari.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimhakikishie kwamba kwa sera na miongozo kwa sasa hospitali zetu za Halmashauri bado hazijawa na mwongozo wa moja kwa moja wa kuwa na waganga mabingwa, kwa maana ya madaktari bingwa katika hospitali hizo, kwa sababu kwa ngazi ile madaktari wa ngazi wanaopatikana bado wana uwezo mzuri wa kutibu na tuna mfumo mzuri wa rufaa pale ambapo kuna kesi ambazo zinashindikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Sophia Mwakagenda kwamba Serikali itaendelea kuboresha ikama ya madaktari katika hospitali ya Makandana ili waendelee kuhudumia vizuri wananchi wetu wakiwepo wanawake katika wodi hizo na kwenda kuboresha huduma za afya kadri ya matarajio ya wananchi.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Hospitali ya Wilaya ya Olturumet katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kwa kuipatia jengo la OPD, Wodi ya kulaza Wagonjwa, Jengo la X-Ray na mashine ya X-Ray ili Hospitali hiyo iweze kutoa huduma kwa wananchi ipasavyo?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Jimbo letu la Mkinga lina vituo vya afya viwili tu. Kituo cha kwanza ni Kitomanga na kituo cha pili ni Rutamba. Kituo cha Rutamba kipo katika hali mbaya sana. Hakikidhi haja za kutoa huduma za afya kama kituo.

Je, ni lini Serikali itatutengea pesa kwa ajili ya ukarabati wa kituo hicho? Kama itampendeza Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri naomba nifuatane nae akaone hicho kituo. Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUNGANGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa mama Salma Kikwete Mbunge wa Mkinga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Jimbo la Mkinga kuna upungufu mkubwa wa vituo vya afya na vituo vya afya vilivyopo ni chakavu ikiwepo Kituo cha Afya hiki cha Mtamba. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mama Salma Kikwete kwamba Serikali inatambua kwamba kuna uhitaji mkubwa sana wa vituo vya afya katika Jimbo la Mkinga na ninatambua kwamba kuna kila sababu ya kuweka jitihada za maksudi kuhakikisha tunakarabati Kituo cha Afya cha Mtamba ili kiweze kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nichukue nafasi hii kumhakikishia kwamba tutachukua hoja hii na kuiwekea kipaumbele katika awamu inayokuja ya ukarabati wa vituo vya afya ili kituo hiki pia kiweze kuwekewa fedha kwa ajili ya ukarabati na upanuzi ili kitoe huduma bora za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa mama Salma Kikwete kwamba tutaendelea kushirikiana kwa karibu sana, na Ofisi ya Rais TAMISEMI tuko tayari wakati wowote kushirikiana na kufuatana na Mheshimiwa mama Salma Kikwete. Baada ya kikao hiki tutapanga kuona uwezekano wa kupata fursa hiyo ili twende kushirikiana pale muda ambapo utaturuhusu.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaboresha Hospitali ya Wilaya ya Olturumet katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kwa kuipatia jengo la OPD, Wodi ya kulaza Wagonjwa, Jengo la X-Ray na mashine ya X-Ray ili Hospitali hiyo iweze kutoa huduma kwa wananchi ipasavyo?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Hospitali ya Kyela jengo la mama na mtoto liliungua. Je, ni lini Serikali sasa itamalizia pesa zilizobaki kwa ajili ya jengo la mama na mtoto katika hospitali ya Kyela?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUNGANGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mlaghila Jumbe Mbunge wa Kyela kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Jumbe kwamba hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ni moja ya hospitali ambazo nazifahamu sana kwa sababu nimekuwa mganga mkuu wa Kyela kwa zaidi ya miaka tis ana nimekuwa sehemu ya uendelezaji wa miundombinu katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela. Ninafahamu kwamba ni kweli wodi ilipata ajali ya moto na Serikali imesha peleka fedha na kazi za ukarabati wa wodi ile zinaendela.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimhakikishie kwamba katika Mpango ujao tumetenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunakamilisha ukarabati wa wodi ile iliyopata ajali ya moto ili iweze kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi. Kwa hiyo naomba nimhakikishie Mheshimiwa Jumbe kwamba jambo hilo linafanyiwa kazi na mara fedha zitakapopatikana basi ukamilishaji wa wodi ile utafanyika ili tuendelee kutoa huduma kama ambavyo tunatarajia.