Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Makazi ya askari yamekuwa ya zamani pia mengine yamekuwa mabovu sana, mfano nyumba za Ziwani Zanzibar, Wete, Pemba na Chakechake Pemba hazikaliki kabisa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia marekebisho nyumba hizo? (b) Je, ni gharama gani Serikali itatumia kwa marekebisho ya nyumba hizo?

Supplementary Question 1

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri Mheshimiwa Masauni, nina maswali mawili ya nyongeza.
Je, ni lini Serikali au Wizara yake itaanza kufanya ukarabati wa nyumba hizo?
Swali la pili, nafahamu Wizara ina mpango mzuri wa kulinda raia na mali zake, kuna kituo cha Shaurimoyo, kuna kituo kidogo cha Mwembeladu lakini vituo hivi vimefungwa kwa muda mrefu sasa.
Je, ni lini Wizara yake itavifungua vituo hivi na kuendelea na kazi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, anauliza ni lini ukarabati huo utaanza. Kama ambavyo nimejibu katika jibu la msingi kwamba pale tu ambapo tutaweza kupata fedha tuaanza huo ukarabati. Kwa hiyo, siwezi kusema exactly ni siku gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia swali lake la pili alikuwa alitaka kujua kwa ni nini kituo cha Shaurimoyo pamoja na kituo cha Mwembeladu havitumiki. Kituo cha Shaurimoyo hakitumiki kwa sababu kwanza, takwimu zinaonyesha kwamba eneo hilo la Shaurimoyo halina uhalifu.
Lakini pili kuna vituo vingi sana ambavyo vipo karibu na kituo cha Shaurimoyo ikiwemo kituo cha Ng‟ambo, kituo cha Mwembemakumbi na Makadara ambapo imezidi maili moja kutokea kituo kilichopo kituo cha Shaurimoyo. Kwa hiyo, kwa kutilia maanani kwamba hali ya kituo hicho siyo nzuri kituo kimechakaa sana tumeamua kituo hicho kwa sasa hivi kitumike kwa ajili ya matumizi ya Polisi Jamii na wananchi wanaendelea kutumia vituo vilivyo karibu na kituo cha Shaurimoyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusiana na kituo cha Mwembeladu ambapo kipo mpakani mwa Jimbo langu vilevile, kituo hiki kilijengwa kwa ajili ya matumizi ya traffic, lakini kutokana na mkakati wa kipolisi wa matumizi ya shughuli za ki-traffic Wilaya, uratibu huo unafanyika katika kituo cha Malindi ambacho nacho hakipo mbali sana na eneo hilo. Pia miundombinu ya kituo cha Mwembeladu haikidhi haja ya kufanya shughuli za traffic kwani hata ukikamata magari siyo zaidi ya gari moja linaweza kukaa katika eneo hilo. Kwa hiyo, kwa kutilia maanani hoja hizo kwa sasa hivi tunaangalia uwezekano wa kubadilisha matumizi ya eneo ili tuweze kupata maeneo mengine ya kuweze kuimarisha shughuli za traffic badala ya kutumia kituo cha Mwembeladu.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Makazi ya askari yamekuwa ya zamani pia mengine yamekuwa mabovu sana, mfano nyumba za Ziwani Zanzibar, Wete, Pemba na Chakechake Pemba hazikaliki kabisa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia marekebisho nyumba hizo? (b) Je, ni gharama gani Serikali itatumia kwa marekebisho ya nyumba hizo?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa tatizo la makazi ya polisi yamekuwa makubwa sana haswa katika Mkoa wangu wa Arusha, polisi wamekuwa wakiishi katika nyumba mbovu na chafu na wengine kuishi uraiani. Kwa kuwa tuna ekari 30 tulizopewa na Magereza kwa ajili ya makazi haya ya polisi. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutumia zile ekari 30 tulizopewa na Magereza kwa ajili ya kujenga makazi haya ya polisi Mkoa wa Arusha?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mpango wa kujenga nyumba katika maeneo mbalimbali. Nilizungumza jana kwamba tuna mpango wa kujenga nyumba 4136 kwa awamu ya kwanza katika mikoa 17 ikiwemo Arusha. Lakini wazo lake la kutumia eneo la Magereza basi tutalichukua tuone tunalifanyia kazi kwa kiasi gani.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Makazi ya askari yamekuwa ya zamani pia mengine yamekuwa mabovu sana, mfano nyumba za Ziwani Zanzibar, Wete, Pemba na Chakechake Pemba hazikaliki kabisa. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia marekebisho nyumba hizo? (b) Je, ni gharama gani Serikali itatumia kwa marekebisho ya nyumba hizo?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, na mimi naomba kumuuliza Naibu Waziri swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa baadhi ya vituo vingi Zanzibar ni vibovu na majengo ni chakavu na askari hawana vitendea kazi wanapokamata wahalifu kama wino wa kuchapisha barua na mahitaji mengine muhimu na hata wahalifu wale hawapati hata mkate kwa sababu siyo wahalifu wote wana jamaa wa kwenda kuwaangalia kwenye vituo vya polisi wanapokuwa mahabusu.
Je, ni lini Serikali itahakikisha vituo vyote vinapatiwa huduma stahiki za kuendesha kazi zao kwa wakati muafaka.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pale ambapo Serikali itapata uwezo wa kifedha.