Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI Aliuliza:- Kutokana na changamoto za vyanzo vya mapato hususan katika Halmashauri zilizo nje ya miji kumekuwa na uwiano usio sawa wa utoaji wa mikopo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta njia ya kuweka uwiano sawa wa mikopo hiyo bila kujali mapato ya Halmashauri husika?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, natambua kwamba Serikali inafanya jitihada kubwa sana kupunguza umaskini vijijini; na kwenye vijiji vyetu vingi vyanzo vya mapato ni vidogo na hivyo kusababisha mikopo ya halmashauri kuwa midogo vijijini ukilinganisha na mijini. Je, Serikali haioni kama kuna haja ya kutafuta njia sahihi ya kugawa mikopo hii ili basi kutimiza dhima hii ya Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; akina mama wa Arusha Mjini wamenituma, sasa hivi kuna sintofahamu ya kugawa mikopo katika Wilaya ya Arusha Mjini. Wanalazimishwa waanzishe viwanda vidogo vidogo ndipo wapate mikopo ya Halmashauri. Akinamama wa Arusha Mjini ni akinamama hodari sana na wanajishughulisha na shughuli nyingi zikiwemo kilimo, ufugaji na hata utalii, wanauza vinyago na shanga na shughuli zingine kadhalika. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu jambo hili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba halmashauri zetu zinatofautiana uwezo wa ukusanyaji wa mapato na hasa Halmashauri za mijini ikilinganishwa na Halmashauri za vijijini. Ni lengo la Serikali kuwawezesha wajasiriamali wa vikundi tajwa kwa maana ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni jambo ambalo linahitaji tafakari ya karibu zaidi kuona uwezekano wa kuweka kiwango sawa kwa Halmashauri zote kwa sababu pia halmashauri hizi idadi ya wananchi inatofautiana. Unaweza ukatafakari kwa mfano tukisema tuweke kiasi sawa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kwa mfano kwa idadi ya wananchi waliopo na Halmashauri ya Wilaya ya Ileje kwa mfano kwa idadi ya wananchi waliopo. Ni dhahiri kwamba Manispaa na Majiji na Miji zina idadi kubwa zaidi ya wananchi na hivyo ni rahisi kuwa na vikundi vingi zaidi kuliko vijijini.

Kwa hiyo, mgawanyo unaotolewa kwa asilimia 10 ya mapato ni equitable inategemeana pia na makusanyo, lakini pia hata idadi ya wananchi katika maeneo hayo inatofautiana. Lakini ni jambo muhimu, tunalichukua na tutaendelea kulifanyia kazi kuona namna bora zaidi ya kuboresha ili wananchi hawa waweze kupata faida ambayo imekusudiwa na Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na sintofahamu ya mikopo Arusha Mjini, ninaomba nitoe ufafanuzi kwamba lengo la mikopo ya asilimia 10 ni kuwawezesha makundi hayo katika shughuli zao za ujasiriamali na maelekezo yaliyotolewa ni wao kuunda vikundi hivyo, lakini pia kutafuta shughuli za ujasiriamali ambazo zinawaingizia mapato na kusajiliwa ili waweze kupata mikopo hii.

Kwa hiyo, hakuna utaratibu wa kulazimisha vikundi vya wanawake, vijana au watu wenye ulemavu kufanya shughuli maalum ili waweze kupata mikopo na ninaomba niendelee kusisitiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuzingatia utaratibu na kanuni za utoaji wa mikopo bila kulazimisha wajasiriamali. (Makofi)

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI Aliuliza:- Kutokana na changamoto za vyanzo vya mapato hususan katika Halmashauri zilizo nje ya miji kumekuwa na uwiano usio sawa wa utoaji wa mikopo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta njia ya kuweka uwiano sawa wa mikopo hiyo bila kujali mapato ya Halmashauri husika?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa majibu ya Serikali yameeleza bayana kwamba uwiano wa mapato katika kila Halmashauri ni tofauti na hata wingi wa watu ni tofauti; na kwa kuwa shida hii ya mikopo ya akinamama bado inaonekana ni kubwa; je, ni lini Serikali itakuwa tayari sasa kuongeza asilimia ya mikopo kwa akinamama kutoka asilimia nne kwenda asilimia 10? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna uwiano tofauti wa mapato ya ndani ya Halmashauri, lakini hoja ya kuongeza kiwango cha ukopeshaji kutoka asilimia 10 kwenda juu zaidi ni jambo ambalo linahitaji kufanyiwa tathmini na kuona uwezekano wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majukumu haya ya asilimia 10, ikumbukwe pia mapato ya Halmashauri yanahitajika pia kuboresha miundombinu mbalimbali kama ujenzi wa vituo, ukarabati wa madarasa, ujenzi wa madarasa na huduma mbalimbali za wananchi. Kwa hiyo, ni jambo ambalo linahitaji pia kufanyiwa tathmini kuweza kuona faida zake na kuweza uona namna gani litaboresha huduma kwa ujumla katika halmashauri na katika vikundi hivi husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba niseme tunachukua wazo la Mheshimiwa Mbunge, tutalifanyia tafakuri na kuona njia bora zaidi ya kuboresha mfumo huu wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10. (Makofi)

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI Aliuliza:- Kutokana na changamoto za vyanzo vya mapato hususan katika Halmashauri zilizo nje ya miji kumekuwa na uwiano usio sawa wa utoaji wa mikopo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta njia ya kuweka uwiano sawa wa mikopo hiyo bila kujali mapato ya Halmashauri husika?

Supplementary Question 3

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nia ya mfuko huo ni kujaribu kusaidia vijana na akina mama na watu wenye ulemavu katika kukuza ajira, hawaoni sasa ni muda mwafaka wa kuongeza muda kutoka miaka 18 hadi 45 badala ya 18 mpaka 35 ambayo hiyo inawazuia wananchi walio wengi kupata mikopo hiyo na kufanya biashara? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Noah kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la mikopo hii kwa vijana ni kuhakikisha kwamba pia inawawezesha kiuchumi, na hasa vijana wa umri wa miaka 18 hadi 35 kwa maana ya definition ya kijana. Kwa hiyo, wazo lake la kuongeza wigo kutoka miaka 18 hadi 45 linahitaji pia kulifanyia tathmini na kuona kama miaka 45 iko ndani ya umri wa ujana au kama maana yenyewe ya vijana inahitaji kuboreshwa ili kuongeza wigo huo. Kwa hiyo, ni wazo zuri, lengo ni kuboresha na sisi Serikali tunaomba tulichukue hilo tukalitafakari na kuona uwezekano wa kulitekeleza kwa manufaa ya jamii yetu. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI Aliuliza:- Kutokana na changamoto za vyanzo vya mapato hususan katika Halmashauri zilizo nje ya miji kumekuwa na uwiano usio sawa wa utoaji wa mikopo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta njia ya kuweka uwiano sawa wa mikopo hiyo bila kujali mapato ya Halmashauri husika?

Supplementary Question 4

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ukweli Halmashauri za Tanzania hazilingani upande wa vyanzo vya mapato, na kwa kuwa Halmashauri kama ya Wilaya ya Same vyanzo vya mapato ni vya chini mno, kwa hiyo, inasababisha wananchi wa Wilaya yetu wa Same kuwa maskini ukilinganisha na kwenye Wilaya nyingine ambazo wana vyanzo vikubwa vya mapato.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta taratibu nzuri ya kufanya zile Halmashauri ambazo vyanzo vya mapato viko chini mno nao wakaongezewa ili wananchi wa Tanzania wawe katika uwiano unaolingana? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tofauti ya kiwango cha mapato katika Halmashauri inatokana na wigo wa ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri husika na kimsingi asilimia kumi kama ambavyo jibu la msingi limeeleza, linatokana na mapato ya ndani baada ya kutolewa vyanzo lindwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali inaona umuhimu wa kuona namna gani tunaweka mazingira mazuri zaidi kwa Halmashauri zile ambazo zina mapato ya chini zaidi, lakini jambo hili linahitaji kulifanyia tathmini, kulipitia na kuona njia nzuri zaidi ya kuendelea kuboresha.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue wazo la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, kuweza kuona ni namna gani tunafanya ili tuweze kuboresha huduma hizi za mikopo ya asilimia 10. (Makofi)