Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. SIMON S. LUSENGEKILE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa katika Hospitali ya Wilaya ya Busega ili huduma bora za afya ziendelee kutolewa?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa naipongeza Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kutupatia pesa shilingi bilioni 5.4 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya ya Bariadi, Bariadi DC, Itilima na Busega. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize swali la nyongeza; kwa kuwa tuna upungufu mkubwa wa watumishi katika hospitali zetu hizo za Wilaya nilizozitaja, je, ni lini Serikali itatuletea watumishi wa kutosha hasa madaktari bingwa wa magonjwa ya wanawake? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya ujenzi wa miundombinu ya hospitali, vituo vya afya na zahanati, Serikali imeweka mkakati ambao tayari umeanza kutekelezwa wa kuajiri watumishi wa kada za afya kuanzia madaktari na wauguzi na ajira hizi zinatolewa kwa awamu. Lengo la ajira hizi ni kwenda kuhakikisha majengo yote yaliyojengwa yanatoa huduma bora za afya kama ilivyotarajiwa.

Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hilo ni kipaumbele cha Serikali na itaendelea kuajiri wataalam wa afya kadri ya upatikanaji wa fedha ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi katika Halmashauri za Mkoa wa Simiyu na nchini kote.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. SIMON S. LUSENGEKILE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa katika Hospitali ya Wilaya ya Busega ili huduma bora za afya ziendelee kutolewa?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD K. OLELEKAITA: Nakushukuru, kwa kuwa swali lililoulizwa linafanana kabisa na matatizo na changamoto tunayopata kama Wilaya ya Kiteto, hususan Hospitali ya Wilaya, tuna upungufu wa mashine ya x-ray, jenereta ni mbovu, majengo, gari la kubeba wagonjwa, vitanda na mashine ya usingizi. Ni lini sasa Serikali itapeleka vifaa hivi katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Kiteto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu ya utoaji wa huduma za afya yakiwemo majengo, vifaatiba, x-ray, ultra sound na vifaa tiba vingine ni vifaa ambavyo vimepewa kipaumbele katika vituo vyetu vya huduma ili kuweza kufikisha huduma bora kwa wananchi na ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimeeleza jinsi ambavyo Serikali imetenga fedha kiasi cha takribani bilioni 33.5 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba katika hospitali zetu 67 za Halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba azma ya Serikali ni kuhakikisha tunaendelea kuboresha upatikanaji wa vifaa tiba katika vituo vyetu vyote ikiwemo Hospitali ya Halmashauri ya Kiteto.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. SIMON S. LUSENGEKILE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa katika Hospitali ya Wilaya ya Busega ili huduma bora za afya ziendelee kutolewa?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tunapozungumzia Hospitali ya Wilaya hatuzungumzii majengo bali tunazungumzia huduma inayotolewa kulingana na level ya Wilaya. Ninapenda kujua Serikali ni lini itatuletea watumishi wa kutosha pamoja na vifaatiba katika Hospitali ya Wilaya ya Nkasi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, uboreshaji wa miundombinu na watumishi katika vituo na hospitali zetu za Halmashauri ni kipaumbele cha Serikali na utekelezaji wake unafanyika kwa awamu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha na ndiyo maana katika mipango ya Serikali ya kila mwaka Serikali inatenga fedha, kwanza, kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunaajiri watumishi ili kuondoa changamoto ya watumishi katika hospitali na vituo vyetu. Lakini pili, tunatenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunaboresha upatikanaji wa huduma bora za afya katika vituo vyetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua sana kwamba majengo ni kitu kingine na huduma bora ni kitu muhimu pia na ndiyo maana tumeendelea kuboresha miundombinu hiyo, lakini upatikanaji wa vifaa tiba pamoja na watumishi na tutaendelea kuhakikisha kwamba tunatekeleza suala hilo.