Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudia zoezi la kuweka alama za mipaka kwa kuwashirikisha wananchi ili kumaliza mgogoro uliopo wa mipaka kati ya Hifadhi ya Kitulo na wananchi wa Vijiji vya Misiwa, Makwalanga, Igofi na Nkondo?

Supplementary Question 1

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Majibu ya Serikali hayajaniridhisha kwa sababu wananchi wetu kwenye zoezi hili la kuweka beacon walishirikishwa kuweka beacon tu, hawakushirikishwa kwenye mipaka itawekwa maeneo gani.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari baada ya Bunge hili tuongozane kwenda Makete tukawape majibu wananchi wetu na kurudia zoezi la kuweka beacon? Kwa sababu zoezi hili limesababisha wananchi wangu wengi saa hizi wako ndani lakini sehemu ya shule zimewekwa beacon…

SPIKA: Mheshimiwa Festo…

MHE. FESTO R. SANGA: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari twende wote?

SPIKA: Nisikilize kwanza; swali lako halijaeleweka kabisa, kwamba wananchi wako wlaishirikishwa kuweka beacon lakini hawakushirikishwa mahali pa kuweka, sasa…

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, kilichotokea wananchi wamefika wamekuta watu wa kutoka Serikalini wanaweka beacon, hawajaambiwa kwamba ni eneo hili la mpaka au wapi. Kilichotokea nyumba nyingi za wananchi ziko ndani ya hifadhi, kitu ambacho hakikuwepo, siku za nyuma mipaka ilikuwa mbali. Leo hii wananchi wangu wengi wako ndani ni kwa sababu ya hilo jambo. Sasa ninachomuomba Naibu Waziri tuongozane baada ya hili Bunge twende Makete akawape wajibu wananchi wetu turudie zoezi; hicho ndicho ninachomwomba. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Richard Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara iko tayari kuhudumia wateja wa aina yoyote akiwemo Mheshimiwa Sanga, hivyo naahidi baada ya Bunge lako Tukufu nitaongozana naye nikiwa na wataalam kwenda kuonesha hiyo mipaka ili wananchi watambue mipaka ya hifadhi ni ipi na iendelee kuheshimiwa. (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarudia zoezi la kuweka alama za mipaka kwa kuwashirikisha wananchi ili kumaliza mgogoro uliopo wa mipaka kati ya Hifadhi ya Kitulo na wananchi wa Vijiji vya Misiwa, Makwalanga, Igofi na Nkondo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza na linakwenda kabisa sambamba na tatizo alilonalo Mheshimiwa Sanga kule Kitulo. Zoezi la uwekaji mipaka ya Hifadhi za Taifa na maeneo ya jamii halikuwa shirikishi kabisa katika Jimbo langu la Longido katika eneo linalotutenga na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro. Kuna eneo la buffer zone la hekta 5,000 ambazo lilitengwa tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza kwamba liwe ni eneo la buffer zone lakini matumizi yaliyoruhusiwa ni kuchunga tu. Hivi leo baada ya beacon kuwekwa bila kuwashirikisha wananchi wanaanza kupelekeshwa kuchungia katika buffer zone. Naomba kuiuliza Wizara, je, wako tayari kutoa tamko kwamba eneo la buffer zone katika ukanda wa msitu wa Mlima Kilimanjaro na Hifadhi ya Taifa zina access ya wachunga mifugo wa Longido na Siha kuchungia?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo ya buffer zone yana miongozo yake na Wizara itaangalia kama inaruhusu kutumika kwa shughuli zingine. Hata hivyo, kwa sababu Kamati ya Mawaziri ilishafanya maamuzi ikapitia baadhi ya maeneo ambayo yalikuwa na migogoro na maamuzi hayo tunatarajia kwamba yataanza kutekelezwa baada ya Bunge lako hili Tukufu, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba awe na subira tumalize Bunge, tuangalie sasa kama yale maeneo anayoyasema yeye yatakuwa ndani ya maamuzi ya Kamati ya Mawaziri ambavyo vijiji 920 tayari vitakuwa vimefaidika na maeneo hayo. Kama kitakuwa hakimo basi Wizara itaendelea kushirikiana naye kuangalia ni kitu gani ambacho tunaweza kufanya ili tusiweze kuathiri maeneo ya machunga (malisho) na kwenye maeneo ya hifadhi.

Mheshimiwa Spika, ahsante.