Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara za Kata ya Katumba?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika mimi nasikitika sana, kata hii ina vijiji 16 hakuna mawasiliano kati ya kijiji hiki na kijiji kingine. Madaraja yote yamekwenda na maji, mito na barabara zote zimeunganika. Wananchi wa Kata ya Katumba wanapata shida sana. Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara za wananchi wa Kata ya Katumba? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Naibu Waziri yuko tayari kwenda na mimi tukimaliza tu Bunge tukatembelee Kata ya Katumba yenye vijiji 16 ili aone uhalisia wake? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Nsimbo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna changamoto ya barabara katika Halmashauri ya Nsimbo na katika kata hii husika, lakini Serikali katika bajeti ya Wilaya ya Nsimbo kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ya shilingi milioni
556 tayari shilingi milioni 148 sawa na asilimia 27 zimekwishapelekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa ajili ya kutekeleza miundombinu ya barabara ambazo zinaunganisha vijiji husika.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza Serikali inatambua changamoto hiyo na ndio maana imepeleka fedha kiasi hiki kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo na madaraja hayo na nimhakikishie kwamba utaratibu wa kuendelea kupeleka fedha nyingine kwa ajili ya kuimarisha miundombinu katika Halmashauri ya Nsimbo na katika vijiji hivi vya kata hiyo unakwenda kutekelezwa.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba, niko tayari baada ya shughuli za Bunge kwenda naye katika Halmashauri hiyo kupitia vijiji hivyo ambavyo vinahitaji matengenezo ili tuweze kuongeza nguvu pamoja na kuondoa changamoto za wananchi. (Makofi)