Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa Barabara za lami na kufunga taa za barabarani katika Mji wa Mafinga chini ya Mpango wa Uendelezaji Miji nchini?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa niaba ya wananchi wa Mafinga, nafarijika kwamba katika zile Halmashauri 19 za Miji, Mafinga nayo itakuwemo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na jibu la msingi, naomba Serikali iweze kuwaambia wananchi wa Mafinga, mazungumzo haya na Benki ya Dunia kwa ajili ya kuanza kutekeleza program nyingine ya kuendeleza miundombinu katika hiyo Miji 26 na 18 yatakamilika lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa hali ya barabara zetu wakati huu ambapo mvua sasa zimeanza kunyesha kwa wingi, maeneo mengi nchi nzima barabara zimekatika baina ya eneo moja na nyingine: Je, Serikali kupitia TARURA iko tayari kutenga fedha za emergence na fedha hizi zikakaa kule kule Wilayani kuliko ilivyo sasa ambapo Wilaya au Mji kama Mafinga inabidi tuombe Emergence Fundkutoka TARURA Makao Makuu; sasa when it is emergence, imaanishe kweli ni emergence: Je, Serikali iko tayari kutenga Emergence Fundkwa ajili ya barabara ambazo zimeleta matatizo wakati kama huu wa mvua nyingi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafingi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika,ni kweli kwamba mazungumzo kati ya Serikali na Benki ya Dunia kuhusu miradi hii ya kuendeleza Miji inaendelea. Niseme kwamba maongezi haya yanaendelea na tunaamini kwamba mipango iliyoko na mwelekeo wa haya mazungumzo haitachukua muda mrefu kukamilisha mazungumzo haya. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira kwamba Serikali inakwenda kutekeleza suala hili kwa ufanisi iwezekanavyo mara baada ya mazungumzo haya kukamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na miundombinu ya barabara na je, kama Serikali iko tayari kupeleka fedha za dharura kupitia TARURA katika Wilaya kwa ajili ya kuhudumia barabara zilizoharibika. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali kupitia TARURA imejipanga ku-respondkwa wakati kutatua changamoto za miundombinu ambayo itatokana na uharibifu wa mvua ambazo zinaendelea kunyesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mara tu changamoto hizi zitakapoonekana katika maeneo husika, naomba nimhakikishie kwamba Serikali iko tayari na tutahakikisha tunatatua changamoto hizo kwa wakati. (Makofi)

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa Barabara za lami na kufunga taa za barabarani katika Mji wa Mafinga chini ya Mpango wa Uendelezaji Miji nchini?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Name naomba nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa miradi hii ya kimkakati ambayo tunaizungumzia imekuwa na msaada mkubwa sana kwenye Halmashauri zetu na hasa kuisaidia TARURA kwenye kuhakikisha miradi inafanikiwa zaidi, tunao mradi mwingine mkubwa wa Tacticambao Serikali imeshauanzisha ikiwemo Jiji la Mbeya pamoja na Jiji la Mwanza na Manispaa nyingine.

Je, ni nini sasa mpango wa Serikali kuhakikisha mradi huu unaanza haraka ili tuone matokeo yake makubwa kama TSCP?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya maswali ya awali. Pia naomba nimpongeze ndugu yangu, mtani wangu Mheshimiwa Stanslaus Mabula Bin Jongo wa kutoka Pwani kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Jiji ambalo tumefanya kazi kubwa sana ni Jiji la Mwanza. Kwa hili, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa waliyofanya kwa kushirikiana na TAMISEMI kubadilisha Jiji la Mwanza kuonekana katika sura iliyokuwepo. Hata hivyo, mpango wetu kama nilivyosema wakati natoa budget speech yangu katika mwaka uliopita kwa mwaka wa Fedha 2021, kwamba tumekuwa na ile miradi ya Tactic, ambapo matarajio yetu makubwa ni kwamba tutakwenda kugusa maeneo 45 zikiwepo Halmashauri za Miji, Mafinga ikiwa ni mojawapo, Nzega, Kasulu, Handeni Mjini na maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Waheshimiwa Wabunge wawe na subira tu, kazi inakwenda vizuri. Ni imani yetu kwamba mradi huu unakwenda kubadilisha kabisa nchi yetu. Katika miaka mitano ijayo, Tanzania miji yake yote itakuwa ni ya ajabu kutokana na kazi kubwa tunayokwenda kuifanya. Kwa hiyo, msihofu, kazi inafanyika vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.