Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Kasi ya utekelezaji wa miradi ya REA III Jimboni Bagamoro ni ndogo:- Je, ni lini miradi hiyo itakamilishwa katika Jimbo la Bagamoyo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Pia nichukue fursa hii kuwapa hongera sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa juhudi kubwa wanayoweka katika utekelezaji wa miradi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nina swali moja la nyongeza. Kijiji cha Kondo katika Kata ya Zinga ambacho kilikuwa kwenye mradi wa REA II, mpaka kufikia Juni 2016 kijiji hicho hakikutekelezewa mradi wake na Mheshimiwa Waziri akaahidi vijiji vyote ambavyo havikutekelezewa miradi yao katika REA II basi vitapewa kipaumbele katika REA III. Huu ni mwaka 2019 kijiji hicho ambacho kiko katika Kata ya Zinga na humo ndani kuna Shule ya Msingi ya Kondo na jirani kuna Shule ya Sekondari ya Zinga, sehemu zote hizo hazina umeme mpaka hivi sasa. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana kauli gani kuhusu kukipatia umeme Kijiji hiki cha Kondo na miundombinu ya Shule ya Sekondari Zinga na Shule ya Msingi Kondo mapema iwezekanavyo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya kwenye swali la msingi la Mheshimiwa Mbunge. Nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Kawambwa kwa kazi nzuri anayofanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabla sijajibu swali, Mheshimiwa Mbunge katika Jimbo lake vijiji vyote sasa vimeshapata umeme kwa sababu ya kazi anayoifanya anavyofuatilia, kilichobaki ni vitongoji. Kwa hiyo nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, kati ya wilaya ambazo sasa hivi vijiji vyake ambavyo vimeshapata umeme ni pamoja na Jimbo la Bagamoyo, kwa hiyo Mheshimiwa hongera sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, alishughulika sana na Shule ya Sekondari ya Fukayosi mwaka jana, ilikuwa na changamoto ya umeme na imejengwa na Korea Kusini, tunampongeza sana ina umeme sasa hivi na inakwenda vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna vitongoji 169 katika Jimbo la Mheshimwa Mbunge; vitongoji 161, vitongoji 100 vyote vina umeme bado vitongoji 69 na Kati ya vitongoji 69 ambavyo havina umeme ni pamoja na Kitongoji cha Kondo. Kwenye Kijiji cha Kondo kuna vitongoji vitatu; vitongoji viwili tayari vina umeme isipokuwa Kondo Kati anayozungumza Mheshimiwa Mbunge.

Kwa hiyo nimpe tu imani Mheshimiwa Mbunge kwamba nimeshawaelekeza wakandarasi kwa kushirikiana na TANESCO wameshaanza kupeleka umeme kwenye Kitongoji cha Kondo na watakamilisha tarehe 12 mwezi ujao. Wanapeleka kwenye Kitongoji cha Kondo pamoja na Shule ya Msingi ya Kondo, lakini pamoja na Shule ya Sekondari ya Zinga. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge wala asiwe na wasiwasi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niongeze kidogo kwa Jimbo la Bagamoyo na Chalinze, mkandarasi aliyeko kule anapeleka umeme kwenye vitongoji vyote na Peri urban inaanza tarehe Mosi mwezi ujao kujumuisha vitongoji vyote vya Bagamoyo pamoja na Chalinze. Chalinze kuna kijiji kirefu sana cha Msigi pamoja na Magurumatare cha kilomita 28 na chenyewe kinapelekewa umeme. Ahsante sana. (Makofi)