Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. VEDASTUS M. MANYINYI) aliuliza:- Licha ya kazi nzuri ya waendesha bodaboda ya kurahisisha usafiri na kupunguza tatizo ya ajira bado ziko changamoto mbalimbali wanazosababisha kama ajali za mara kwa mara pamoja na wizi. (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutofautisha adhabu ya waendesha bodaboda na ile ya magari makubwa kulingana na vipato vyao?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza naipongeza Serikali kwa majibu mazuri waliyoyatoa, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa utafiti na maeneo mengi yanaonyesha kwamba bodaboda wengu katika nchi na hasa kwa Mkoa wa Mara wanafanya kazi ile bila kupata mafunzo rasmi ya kazi yao. Sasa ni lini Serikali itatoa mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu kwa vijana wote wanaoendesha bodabora katika Mkoa wa Mara?

Swali la pili, kwa jimbo langu la Bunda na hasa Wilaya ya Bunda kumekuwepo na usumbufu mkubwa wa bodaboda wakati wa siku za minada, hasa Mnada wa Mgeta, Bitalaguru na mnada wa Bulamba. Sasa je, Waziri uko tayari kuja Bunda na hasa Jimbo la Bunda kukutana na viongozi wa bodaboda na watalaam wako wa traffic katika jimbo la Bunda ilikuona namna gani ya kutatua kero hiyo hasa siku za mnada inakuwa kama inafanya operation?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeza sana Mheshimiwa Mwita Getere, nakumbuka niliwahi kufanya ziara katika jimbo lake tulishirikiana kwa karibu sana kuhakikisha kwamba changamoto ambazo zinawakabili wananchi wake zinazohusu vyombo vyetu vinavyohusu Mambo ya Ndani ya Nchi tunavikabili.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba hata katika hili suala ambalo amelizungumza la usumbufu wa wananchi wake kwenye minada na amenitaka niende basi namhakikishia kwamba nitafanya hivyo kama ambavyo nilifanya wakati ule.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusiana na mafunzo kwa Mkoa wa Mara tumekuwa na utaratibu mzuri kupitia Jeshi la Usalama barabarani kwa kutoa mafunzo watumiaji wa vyombo vya usafiri barabarani. Hata hivyo nichukue nafasi hii kumhakikishi kwamba kwa kuwa nitakwenda katika jimbo lake basi tunaweza kushauriana kuwa mpango mahususi wa jimbo lake kuhusiana na utararibu wa kutoa elimu ili kuepusha usumbufu kwa wananchi wake au hususani vijana wanaendesha bodaboda waweze kutii sheria na kuepusha usumbufu na hatimaye kupunguza ajali zinaendelea kupoteza maisha ya wananchi.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. VEDASTUS M. MANYINYI) aliuliza:- Licha ya kazi nzuri ya waendesha bodaboda ya kurahisisha usafiri na kupunguza tatizo ya ajira bado ziko changamoto mbalimbali wanazosababisha kama ajali za mara kwa mara pamoja na wizi. (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutofautisha adhabu ya waendesha bodaboda na ile ya magari makubwa kulingana na vipato vyao?

Supplementary Question 2

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, katika Wilaya ya Mbozi kumekuwa na usumbufu mkubwa sana kwa vijana wa bodaboda ambao wameamua kujiajiri ili kuweza kujikimu katika maisha na wamekuwa wakinyanganywa pikipiki hasa katika Mji Mdogo wa Mlowo pamoja na Mji wa Vwawa na maeneo mengine wamekuwa wakisumbuliwa sana na pikipiki zao zimekuwa zikichukuliwa kupelekwa Vituo vya Polisi.

Je, Serikali haioni kwamba huko ni kuwanyanyasa vijana ambao wameamua kujiajiri kupitia kazi hii ya bodaboda inayo wapatia kipato wao na wengine wameamua kuachana na maisha yao ya awali ambao hayakuwa mazuri wameamua kujiajiri. Sasa ni lini Serikali itakataza askari wasiwanyanyase vijana hao ambao wanafanya kazi hii ya bodaboda katika Wilaya Mbozi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, hatukubali kuona wala haturuhusu kuona askari wakinyanyasa wananchi. Si jukumu la askari kunyanyasa wananchi, lakini kuhusiana na suala ambalo amelizungumza kuhusiana na jimbo la Mbozi kuhusu vijana hawa ambao anadai kwamba wananyanyaswa na waendesha bodaboda nisema yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza hili tulishalitolea maelekezo hapa Bungeni kwamba kuna aina ya makosa ambayo pikipiki zikikamatwa zinakuwa katika Vituo vya Polisi kuanzia sasa na tumeshatoa waraka huo katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ili wautekeleze. Sasa sina hakika kama hawa anaowazungumzia Mheshimiwa Haonga wapo katika yale makosa ambayo tumeyaruhusu waweze kukamatwa ama katika makosa ambayo tulishakata yasikamatwe.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ninachoweza kumhakikishia ni kwamba tutafuatilia kujua kama yatakuwa makosa ambayo tulishaelekeza yasikamatwe vijana hao basi tutachukua hatua kwa kushindwa kutekeleza maelekezo ya Wizara. Lakini kama itakuwa ni makosa ambayo yanaruhusika na tumeruhusu waweze kukamatwa basi tutamuelimisha Mheshimiwa Haonga ili aweze kuelimisha wananchi wake wafahamu na waepuke kufanya makosa kama hayo.

Name

Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. VEDASTUS M. MANYINYI) aliuliza:- Licha ya kazi nzuri ya waendesha bodaboda ya kurahisisha usafiri na kupunguza tatizo ya ajira bado ziko changamoto mbalimbali wanazosababisha kama ajali za mara kwa mara pamoja na wizi. (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutofautisha adhabu ya waendesha bodaboda na ile ya magari makubwa kulingana na vipato vyao?

Supplementary Question 3

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, hao watu wa bodaboda wana tabia moja mbaya sana, na mimi wameshafanyiwa wageni wangu, wanapora simu, halafu wanakimbia na hapa juzi katika eneo la Area D ninapokaa mimi, mama mmoja alikuwa na simu wamekuja watu wa bodaboda wamepora, sasa hatua gani Mheshimiwa Rais anawapenda wanyonge watu wa bodaboda lakini tabia hii ni mbaya sana kwa kupora.

Mheshimiwa Spika, kesho watakuwa na bastora watakwenda majumbani au madukani, kwa hiyo, mimi naomba Mheshimiwa Naibu Waziri atuambie ni sheria gani hawa watu wa bodaboda wanafanya tabia hiyo mbaya kwa kupora simu pamoja na begi? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, si sahihi nadhani kuwajumuisha waendesha bodaboda na matukio ya wizi, waendesha bodaboda ni raia ambao wanafanya kazi zao, wanapaswa kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria ya kujipatia riziki ambazo zimeruhusiwa kisheria ni shughuli za kihalali.

Mheshimiwa Spika, sasa kama kuna watu ambao wanatumia pikipiki ama hiyo pikipiki ya kawaida ama iwe bodaboda kwa ajili ya uporaji hao ni wahalifu kama wahalifu wengine na kwa hiyo basi kama ambavyo ilivyo kawaida na desturi ya Jeshi letu la Polisi kuweza kukabiliana na wahalifu imekuwa ikifanya hivyo kushughulika na watu ambao wakitumia pikipiki ama bodaboda kwa ajili ya kupora wananchi na tutaendelea kufanya hivyo kuwashughulikia bila huruma wale wote ambao wanatumia pikipiki ama bodaboda kwa ajili ya kufanya uporaji.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. VEDASTUS M. MANYINYI) aliuliza:- Licha ya kazi nzuri ya waendesha bodaboda ya kurahisisha usafiri na kupunguza tatizo ya ajira bado ziko changamoto mbalimbali wanazosababisha kama ajali za mara kwa mara pamoja na wizi. (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutofautisha adhabu ya waendesha bodaboda na ile ya magari makubwa kulingana na vipato vyao?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kutokana na uhaba wa ajira na ukosefu wa mitaji, vijana wengi wanaomaliza shule sasa hivi wameiona kazi ya bodaboda kama ni kazi ambayo inawaingizia kipato. Jimboni kwangu ukienda Mamsera pale, Mengwe, Mkuu, Useri na Tarakea vijana waliomaliza chuo kikuu na form six wamejiingiza katika biashara hii na inawaletea kipato kizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambasamba na hilo, kuna vijana wengine ambao tabia zao siyo njema sana, nao wamejiingiza kufanya sasa vijana wote wa bodaboda waonekane kwamba ni vijana ambao hawafai na baadhi ya polisi wanalalamikiwa kufanya hii kazi ya bodaboda ionekane ngumu zaidi kwa kuchukua rushwa na kuwabambikia makosa.

Je, Jeshi la Polisi au Wizara hamuoni sasa kutokana na ukubwa wa kazi hii ya bodaboda kuweka polisi maalum, trafiki maalum kabisa katika kila Kituo ambaye kazi yake itakuwa ni ku-deal tu na bodaboda ili kuweza kupunguza haya matatizo yao?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, Nakubaliana kabisa na Mheshimiwa Selasini kwamba biashara ya bodaboda ni biashara ambayo ni kama biashara nyingine na ndiyo maana mara nyingi sana tumekuwa tukiwaelimisha watumiaji hasa viongozi wa vijiwe hivi vya bodaboda kwamba watusaidie kuwaelimisha wenzao ambao wanafanya kazi hii kwa pamoja ama ambao wanawaongoza ili biashara ya bodaboda isivunjiwe heshima ikaonekana kwamba ni kazi ya kihuni.

Mheshimiwa Spika, na kwa kufanya hivyo nadhani itasaidia sana kuondoa taswira mbaya iliyopo kwa baadhi ya wananchi mbele ya waendesha bodaboda ama biashara za bodaboda. Sasa kuhusiana na hoja yake kwamba tuweke askari maalum, sisi tuna Kitengo cha Usalama Barabarani ambacho kinashughulika na masuala yote yanayohusu usalama barabarani yakiwemo ya waendesha bodaboda na kazi hiyo imekuwa ikifanyika kwa ufanisi mkubwa. Kwa hiyo sioni kama kuna haja ya kusema tubague labda bodaboda iwe mbali, magari ya daladala yawe mbali, mabasi yawe mbali, nahisi kwamba utaratibu uliopo unakidhi mahitaji na tutaendelea kuboresha pale ambapo tutaona kuna mapungufu katika kusimamia Sheria za Usalama Barabarani kwa bodaboda na vyombo vingine.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. VEDASTUS M. MANYINYI) aliuliza:- Licha ya kazi nzuri ya waendesha bodaboda ya kurahisisha usafiri na kupunguza tatizo ya ajira bado ziko changamoto mbalimbali wanazosababisha kama ajali za mara kwa mara pamoja na wizi. (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutofautisha adhabu ya waendesha bodaboda na ile ya magari makubwa kulingana na vipato vyao?

Supplementary Question 5

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii.

Mheshimiwa Spika, bodaboda ni kitu chema na bodaboda imerahisisha usafiri, bodaboda imesaidia sana kuleta ajira kwa vijana wa Taifa letu la Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio hayo, lakini kuna changamoto zinazoweza kujitokeza pale inapotokea bodaboda imesababisha ajali barabarani, baadhi yao kwa muda mfupi wanajaa eneo la tukio na hatimaye kuweza kuchukua hatua za papo kwa papo na matokeo yake wanaweza kusababisha vifo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, je, Serikali inachukua hatua gani juu ya kutoa elimu kwa waendesha bodaboda kwamba wasichukue hatua za mkononi? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete, swali zuri na muhimu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli matukio kama haya yamekuwa yakitokea, na ni matukio ambayo yanasikitisha sana na hayakubaliki katika jamii iliyostaarabika kama jamii ya Watanzania na kwa hiyo, naendelea kutoa wito hapa, kwanza nichukue fursa hii nikitumia jukwaa hili la Bunge kama ni moja katika njia ya elimu kwa waendesha bodaboda wote nchini kuepuka kuchukua sheria mkononi na wale wote ambao wamekuwa wakifanya hivyo hatma yao haijawa njema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo sidhani kama kuna mwendesha bodaboda ambaye anataka hatma ya maisha yake iishie gerezani au iishie kwa kuhukumiwa hukumu ya kunyongwa kwa kusababisha mauaji yasiyokuwa na lazima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo niendee kusisitiza kwamba utaratibu wetu wa utoaji wa elimu kwa bodaboda utiliwe maanani na mkazo zaidi katika eneo la kuhakikisha kwamba waendesha bodaboda hawatumii, hawachukui sheria mkononi inapotokea matatizo ya usalama barabarani na kuacha vyombo na sheria za nchi zifuate mkondo wake. (Makofi)

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. VEDASTUS M. MANYINYI) aliuliza:- Licha ya kazi nzuri ya waendesha bodaboda ya kurahisisha usafiri na kupunguza tatizo ya ajira bado ziko changamoto mbalimbali wanazosababisha kama ajali za mara kwa mara pamoja na wizi. (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo hilo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutofautisha adhabu ya waendesha bodaboda na ile ya magari makubwa kulingana na vipato vyao?

Supplementary Question 6

MHE. KEMILEMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Spika, ahsante nakushukuru kwa kuweza kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, suala la ajali za bodaboda siyo kwa Mkoa wa Mara tu, ni Tanzania nzima kwa ujumla wake. Bodaboda hawa wengi wao wanakata third part insurance ambayo kimsingi inatakiwa iwasaidie pale wanapopata matatizo lakini kiuhalisia insurance hii haiwasaidii chochote bodaboda hawa wanapopata matatizo.

Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kukaa na hawa watu wa insurance ili baadhi ya fedha inayotozwa/ wanayolipa hawa watu wa bodaboda iweze kwenda kwenye Halmashauri zetu ili waweze kupata msaada kwenye hospitali ambapo hospitali hizi ndiyo zinawapokea na kuwatibu watu hawa? Nashukuru. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, wazo lake linafikirika na kwa hiyo basi tunalichukua, tulitafakari.