Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Mkoa wa Dodoma una mahitaji ya walimu 11,676 kwa uwiano wa 1:40 kwa shule za msingi. Kwa sasa walimu waliopo ni 7,382 na hivyo kuwa na upungufu wa walimu 4,410 sawa na asilimia 38. Je, ni lini Serikali itaajiri mwalimu wa kutosha Mkoani Dodoma?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Spika, elimu ya msingi ni kumjengea mtoto uwezo wa kujua, wa kuelewa na wa kuendelea na maisha ya elimu na ujuzi katika siku za mbele; na unapoacha kumpa mwanafunzi wa shule ya msingi mwalimu wa kumsaidia hata huko sekondari hawezi kufanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, tuliomba walimu 4,410 lakini tumepewa walimu 699 hata nusu ya kiwango tulichoomba hatujapata; na hapo kuna walimu waliostaafu, waliotolewa kwa vyeti fake, kuna wanaougua ambao wamesafishwa kwa ajili ya kuugua. Walimu 699 hawakidhi mahitaji ya walimu wa shule za msingi na kutokana na ujio wa makao makuu kuna uhitaji mkubwa sana wa walimu wa shule za msingi.

Serikali ina mkakati gani sasa wakuongeza walimu wa kutosha katika mkoa wetu wa Dodoma?

Mheshimwa Spika, swali la pili, tuna walimu 203 ambao wamestaafu ambao mahitaji yao ya fedha wanazotakiwa kulipwa ni shilingi milioni 260. Walimu hawa tangu mwaka 2014 hajalipwa stahili zao na wamekwishastaafu wapo nyumbani.

Ni lini sasa Serikali itawalipa walimu hawa 203 ambao wamestaafu wameshindwa kurudi kwao kutokana na kutolipwa stahiki zao?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA W. WAITARA): Mheshimwa Spika, ni kweli kwamba tulipata kibali cha kuajiri walimu 4500 lakini uhitaji wa walimu wa shule za msingi ni zaidi 66,000; uhitaji wa walimu wa sekondari ni zaidi ya 14,000; walimu 3,088 tuliwapeleka shule za msingi na walimu waliobaki ndio tulipeleka sekondari. Kwa hiyo katika hesabu hiyo katika hali ya kawaida lazima kutaendelea kuwa na upungufu na kuna Halmashauri na shule nyingine hazikupata walimu kabisa, huo ndio ukweli.

Mheshimwa Spika, lakini kama nilivyosema kwenye swali lililotangulia tuliomba kibali cha kuajiri walimu tukipata kibali hicho tunaongeza walimu lakini tutapeleka maeneo ambayo wana uhitaji makubwa ikiwepo na Mkoa wa Dodoma.

Mheshimwa Spika, swali la pili anauliza walimu wastaafu; malipo ya stahiki za walimu ziko za aina mbili, kuna malipo yanayolipwa na Halmashauri zetu lakini pia kuna malipo ambayo yanatoka katika Serikali Kuu. Katika Mkoa wa Dodoma amezunguzumza walimu 203 lakini sisi tunajua kwamba tuna walimu hapa 599 katika Mkoa huu ambao wamestaafu na wadai fedha zaidi ya shilingi milioni 652. Lakini madi yalipokuja TAMISEMI yamerudishwa kule kwa mambo manne.

Moja, ni kwamba madai hayo pia yanabidi yahakikiwe kamati za ukaguzi za mikoa na halmashauri hazikufanya hivyo; lakini jambo la pili kwa mfano nauli za walimu inabidi Wakurugenzi walipe. Wakurugenzi hawakuwa wameonesha wana mkakati gani wa kulipa walimu wastaafu fedha kutoka kwenye mipango ambayo ni maelekezo ya Serikali; lakini jambo la tatu ni lazima fedha hizo baadhi ya watumishi waliomba wameletwa kwamba wadai wengine wanastaafu mwaka 2019 yaani mwaka Juni kimsingi walikuwa hawajastaafu. Sasa tulipoangalia namna ya ukokotoaji wa zile nauli kwamba nani analipwa nini kutoka wapi kwenda ilikuwa imekosewa.

Mheshimwa Spika, kwa hiyo tukarudisha madai hayo katika viongozi wetu wa Mikoa na Halmashauri wayafanyie kazi tutawasiliana na Wizara ya Fedha, ukweli ni kwamba wataafu wa Serikali wakiwemo na walimu baada ya kufanya kazi kubwa kutumikia taifa hili kwa unyenyekevu mkubwa na uaddilifu mkubwa ni lazima walipwe stahiki zao.

Kwa hiyo, naomba kwa Wakurugezi wahakikishe kabla ya kuleta madai ni lazima wahayahakiki ili kondoa usumbufu ambao walimu wetu na wastaafu wengine wanaupata, ahsante.