Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. RUTH H. MOLLEL) aliuliza:- Migogoro ya wakulima na wafugaji imekuwa tatizo sugu katika maeneo mengi nchini pamoja na kazi kubwa ambayo imefanywa na Serikali:- (a) Je, Serikali imetenga kiasi gani cha bajeti kwa ajili ya kupanga matumizi ya ardhi nchi nzima? (b) Kijiji cha Matenzi Kata ya Beta Wilayani Mkuranga kina wafugaji takribani 10,000: Je, Serikali ina mkakati gani wa kupima eneo hilo kabla migogoro haijaanza?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwa niaba ya Mheshimiwa Ruth Mollel, bado ana maswali amwili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali ni moja na Serikali Kuu alikasimu baadhi ya madaraka yake katika Serikali za Mitaa, basi Serikali Kuu haina budi kusimamia na kuratibu shughuli mbalimbali za Serikali za Mitaa. Serikali haioni ni vyema sasa kusimamia na kutoa maelekezo mahususi katika Serikali za Mitaa katika kujikita kupanga ili tujue kwamba matumizi ya ardhi ni nani anatumia nini kwa ajili ya shughuli za kiuchumi?

Mheshimiwa Spika, vilevile kwa kuwa Serikali Kuu imechukua vyanzo vikuu vya mapato katika Serikali za Mitaa, Serikali Kuu haioni sasa ni muhimu ku-ring fence fedha fulani kwa ajili ya shughuli mahususi za kuratibu shughuli za upangaji wa matumizi ya ardhi? (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli Wizara ya Ardhi ina wajibu ya kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Ardhi Na. 5 na utekelezaji wa Sheria ya Mipango Miji zote zinahusiana na mambo ya ardhi.

Mheshimiwa Spika, tumekuwa tunafanya hivyo, tunatoa mwongozo wa kusimamia na kupitia wataalam wetu waliopo kila Halmashauri wanashiriki, kwa sababu kazi hii inasimamiwa na wataalam wa Sekta ya Ardhi ambao wako katika kila wilaya. Ndiyo maana imewezesha leo hii Wilaya hiyo ya Mkuranga anayoiulizia swali, Mheshimiwa Ulega, Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, ni shahidi, vijiji 21 tayari vimeshafanyiwa mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Mheshimiwa Spika, kutokana na mafunzo ambayo Wizara tumeyatoa na uwezeshaji tulioufanya katika Wilaya ya Mkuranga, wale viongozi, Madiwani pamoja na watendahi wa Sekta ya Ardhi wa Mkuranga wameweza kujiongeza wenyewe kutekeleza wajibu wao na kwenda kufanya sasa mipango ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji 21. Kwa hiyo, kazi hiyo ndiyo tunayofanya.

Mheshimiwa Spika, la pili ni fedha. Sisi kama Wizara, hata kwenye bajeti yangu kesho mtaona, tumekuwa tunapanga fedha kusaidia kazi hii tunayofanya. Leo kwa mfano tunapanga matumizi bora ya ardhi na kupanga na kupima kila kipande cha ardhi. Tumeanza Mkoa wa Morogoro katika wilaya tatu. Namwalika mwuliza swali siku moja katika Wilaya za Kilombero, Malinyi na Ifakara ili aje uone kazi inayofanywa.

Mheshimiwa Spika, tumeanza mpango mwingine ambao tunakamilisha sasa wa kutaka kupanga na kupima kila kipande cha ardhi nchi nzima. Sasa huo ndiyo mpango wa Serikali Kuu kwa uwezo wa Serikali Kuu. Kwa hiyo, yote mawili tunafanya; hatuwezi kuwaacha wenye jukumu lao wasifanye, lakini Serikali Kuu nayo imekuwa ikishiriki katika kufanya kazi hii tukijua kwamba tuna wajibu wa kufanya hivyo.

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. RUTH H. MOLLEL) aliuliza:- Migogoro ya wakulima na wafugaji imekuwa tatizo sugu katika maeneo mengi nchini pamoja na kazi kubwa ambayo imefanywa na Serikali:- (a) Je, Serikali imetenga kiasi gani cha bajeti kwa ajili ya kupanga matumizi ya ardhi nchi nzima? (b) Kijiji cha Matenzi Kata ya Beta Wilayani Mkuranga kina wafugaji takribani 10,000: Je, Serikali ina mkakati gani wa kupima eneo hilo kabla migogoro haijaanza?

Supplementary Question 2

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa tatizo la migogoro ya ardhi Mkoa wa Pwani inasababishwa na makundi makubwa ya mifugo inayotoka sehemu mbalimbali: Je, Serikali ina mpango gani kukaa Wizara ya Mifugo na Wizara ya Ardhi kupanga na kuzuia makundi hayo ya mifugo?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, anasema ng’ombe.

Mheshimiwa Spika, dawa siyo kuzuia. Tunashirikiana kama Serikali moja na Wizara zote zinazohusika na matumizi ya ardhi ambao ni wadau kupanga matumizi bora ya ardhi, kupanga maeneo ya malisho na kuweka miundombinu. Hiyo ndiyo dawa ya kuwawezesha wafugaji watulie, wafanye shughuli zao za ufugaji kwa tija zaidi. Dawa siyo kuwaondoa wala kuwafukuza.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali kwa ujumla kwa pamoja tunafanya hiyo mikakati na katika kazi ambayo alitutuma Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, katika ile timu ya Mawaziri wanane tumeandaa utaratibu ambao tunapendekeza utakuwa ndiyo mwarobaini ambao utawezesha kuainisha maeneo, kuyatambua, kuyapanga na kupanga miundombinu katika maeneo hayo ili wafugaji na wakulima waweze kukaa mahali salama ili waweze kuzalisha na kuongeza tija katika nchi hii.

Kwa hiyo Serikali kwa ujumla kwa pamoja tunafanya hiyo mikakati na katika kazi ambayo alitutuma Dkt. John Pombe Magufuli, katika ile timu ya Mawaziri nane tumeandaa utaratibu ambao tunapendekeza utakuwa ndiyo muarobaini ambao utawawezesha kuainisha maeneo kuyatambua, kuyapanga na kupanga miundombinu katika maeneo hayo ili wafugaji nao na wakulima waweze kukaa mahali salama ili waweze kuzalisha na kuongeza tija katika nchi hii.