Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. DKT. TULIA ACKSON (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Umeme wa REA umepita katika vijiji vya Unyamwanga, Kisonidzela na Mpuga lakini wananchi wa maeneo hayo hawajaunganishiwa huduma ya umeme. Je, ni lini wananchi hao wataunganishiwa huduma ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. TULIA ACKSON: Mheshimiwa Spika, nakushuru kwa fursa pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza Kata ya Lupepo haina umeme kabisa na hivyo shule ya Sekondari Lupepo haina huduma hiyo na pia zahanati ya Lupepo watu wanajifungulia gizani, ni lini kwenye Kata hii tutaletewa umeme wa REA? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri alipokuja Jiji la Mbeya alitoa ahadi kwa Kata ya Usalaga na Kata ya Iduda kwamba wananchi wa maeneo haya watawekewa umeme kwa shilingi 27,000. Lakini kuna Kata zingine za Jiji la Mbeya ambazo pia hazina umeme na ningependa kusikia msimamo wa Serikali kuhusu bei ya umeme kwenye kata hizi, na kata hizi ni Kata ya Itende, Kata ya Iziwa, Kata ya Nsoho, Kata ya Iwambi, Kata ya Mwasanga, Kata ya Itezi, Kata ya Mwansekwa, Kata ya Nsalaga na Kata ya Idunda na Kata ya Itagala? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri katika swali la msingi la msingi la Mheshimiwa Naibu Spika kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge wa Rungwe.

Mheshimiwa Spika, napenda nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Naibu Spika kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge wa Rungwe kama ifuatavyo;-

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli kabisa katika shule ya sekondari katika Kata la Lupepo pamoja na kituo cha afya havijapatiwa umeme, lakini nilipotembelea Rungwe niliwaomba sana Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Halmashauri waweze kulipia ili shule pamoja na zahanati zipelekewe umeme. Niombe tu Mkurugenzi wakandarasi wetu wako site na wamemfuatilia mpaka wiki iliyopita alipe ili shule ya sekondari na zahanati zote zipatiwe umeme ikiwezekano wiki ijayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kweli nilitembelea Mbeya Mjini na maeneo mengine na katika maeneo ambayo nilitembelea nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Spika kwa niaba ya Mbunge na Wabunge wengine wa Mbeya kwa kufuatilia ipasavyo sana katika kupeleka umeme katika vijiji vya Mbeya Mjini.

Mheshimiwa Spika, nilipotembea Mbeya Mjini kwanza aliomba maeneo saba yapelekewe umeme ikiwemo eneo la Kitunda, Msalaga na maeneo mengine yote yameshapelekewa umeme nakupongeza Mheshimiwa Naibu Spika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ameendelea kuomba maeneo mengine14 katika Jiji la Mbeya ili nayo yapelekewe umeme kwa shilingi 27,000, tumeanza kuyapelekea kuanzia mwezi huu Kata zote za Nsalaga mpaka Relini zitapelekewa umeme wa 27,000, nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Spika. (Makofi/ vigelegele)

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DKT. TULIA ACKSON (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Umeme wa REA umepita katika vijiji vya Unyamwanga, Kisonidzela na Mpuga lakini wananchi wa maeneo hayo hawajaunganishiwa huduma ya umeme. Je, ni lini wananchi hao wataunganishiwa huduma ya umeme?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Nataka nipate tu maelezo ya Serikali ni lini mtapeleka umeme katika vile vijiji ambavyo vilishapitishwa kwenye mradi wa REA II vijiji vya Ruvu na Dimba katika Jimbo la Mchinga?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameulizia vijiji vyake viwili ambavyo viko kwenye mpango wa kupelekewa umeme katika REA III mzungunguko wa kwanza, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na tulikutana Lindi nikamuahidi baada ya Bunge hili la Bajeti tutatembelea Jimbo lake na Mkandarasi State Grid kupitia ziara ambayo alifanya Mheshimiwa Waziri katika Wilaya ya Luwangwa, Wilaya ya Nachingwea na Jimbo la Mtama Lindi vijijini ameonesha kupata kasi zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nilitaka nimtaarifu tu kwamba kazi inaendelea katika vijiji alivyovitaja na baada ya Bunge hili kwa ruksa ya Mheshimiwa Waziri tutaambatana naye tukague na tuwashe umeme katika vijiji vyake asiwe na wasiwasi ahsante sana. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. TULIA ACKSON (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:- Umeme wa REA umepita katika vijiji vya Unyamwanga, Kisonidzela na Mpuga lakini wananchi wa maeneo hayo hawajaunganishiwa huduma ya umeme. Je, ni lini wananchi hao wataunganishiwa huduma ya umeme?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona niweze kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa kabla ya kuuliza swali naomba kutoa pole nyingi kwa Wananchi wa Mkoa wa Kagera kwa mafuriko kwa ajili ya mvua nyingi zinazoendelea kunyesha. Mimi Mbunge wao na Serikali tuko pamoja, nawapa pole sana Ndugu zangu wa Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Spika, sasa swali la nyongeza, changamoto iliyopo Rungwe inafanana kabisa na changamoto iliyopo Wilaya ya Ngara katika Kata ya Mlusagamba, Kata ya Bukiriro na Mganza. Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika kata hizo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge Oliver na kumpongeza, hii ni mara yake ya tatu anasimama ndani ya Bunge hili kuulizia masuala ya nishati katika Jimbo la Ngara. Hizo kata alizozitaja ikiwemo Msagamba, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwa miradi ya REA inayoendelea kata hizi zimeingia kwenye REA Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili, ambao unaanza tarehe 01Julai, 2019, tuko katika hatua za kuandaa makabrasha ya zabuni. Kwa hiyo, nimtoe hofu tu kwamba, na Wananchi wakazi wa Ngara kwamba, Serikali yetu ya Awamu ya Tano imedhamiria ifikapo 2020/21 maeneo yote, vijiji vyote vikiwemo vijiji vya Wilaya ya Ngara viwe vimewaka umeme. Kwa hiyo, nimtoe tu wasi Mheshimiwa Mbunge aendelee kushirikiana na sisi katika kufuatilia hayo maeneo yake, asante sana.