Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID aliuliza:- Kwa muda mrefu kumekuwa na upungufu mkubwa wa Wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar hali inayopunguza ufanisi wa kazi katika Idara hiyo? (a) Je, ni lini Serikali itaajiri Wafanyakazi wa kutosha katika Idara hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itaimarisha Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi ili kupunguza msongamano katika Ofisi kuu ya Uhamiaji Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. MACHANO OTHMAN SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jibu lake lakini pamoja na majibu hayo nataka kumuuliza swali lifuatalo, kwa kuwa mwaka wa fedha 2018/ 2019 umebakisha kama mwezi mmoja kumalizika, na kwa kuwa ajira hizi bado hazijafanyika, na kwa kuwa upungufu huu wa wafanyakazi unasababisha wafanyakazi zaidi ya wale wa malindo kuingia kazini usiku na asubuhi kurejea tena kazini, Je, Mheshimiwa Waziri anatuhakikishia vipi kwamba ajira hizi 505 zitafanyika kwa wakati.

(b) lakini, Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi inafanya shughuli zake, wananchi wengi wa Zanzibar badala ya kwenda kwenye Mkoa wanakwenda Makao Makuu, Ofisi Kuu kwa sababu kule Mkoa hakuna nyenzo za kufanyia shughuli zao hasa passport. Ni hatua gani Serikali itachukua ili kupunguza mzigo Ofisi Kuu na wananchi kwenda katika Mkoa? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na ajira, kama ambavyo nimezungumza kwamba tunatarajia kuajiri na hivyo, basi pale ambapo kibali kitakuwa kimepatikana kutoka Utumishi vijana hao wataajiriwa, lakini swali lake la pili kuhusiana na kuboresha mazingira ya Ofisi ya Mjini Magharibi, ili kupunguza msongamano Makao Makuu nataka nimuhakikishie kwamba katika mwaka wa fedha tumetenga takribani shilingi milioni mia tatu kwa ajili ya kukamilisha matengenezo ili tuweze sasa kutumia vizuri zaidi, mara kazi hizo zitakapokamilika kwa mwaka huu, basi ni dhahiri kwamba sasa mazingira ya kazi katika Ofisi ya Mjini Magharibi yataboreka na msongamano utapungua.

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID aliuliza:- Kwa muda mrefu kumekuwa na upungufu mkubwa wa Wafanyakazi wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar hali inayopunguza ufanisi wa kazi katika Idara hiyo? (a) Je, ni lini Serikali itaajiri Wafanyakazi wa kutosha katika Idara hiyo? (b) Je, ni lini Serikali itaimarisha Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mjini Magharibi ili kupunguza msongamano katika Ofisi kuu ya Uhamiaji Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, licha ya juhudi kadhaa ambazo zimefanywa lakini bado unyanyasaji wa watu Maafisa Uhamiaji kwa wananchi wa Mkoa wa Kigoma, na hasa Manispaa ya Kigoma Ujiji kwenye masuala ya Uraia bado ni mkubwa, sasa Serikali haioni kwamba inge-priortise watu kupewa vitambulisho vya Uraia kwa haraka, ili kuweza kuhakikisha kwamba tunaondoa hili tatizo la watu kila wakati kukisiwa kwamba sio raia? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimuhakikishie Mheshimiwa Zitto, kwamba, malalamiko ambayo yeye pamoja na Waheshimiwa Wabunge wa Kigoma ambayo walikuwa wanayatoa kipindi cha nyuma kuhusiana na unyanyasaji wa wananchi tuliyafanyia kazi na kipindi ambacho tulikwenda kwenye ziara nikiwa nimeambatana na Mheshimiwa Waziri Mkuu na yeye alikuwepo nadhani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulilithibisha hilo kwamba sasa hali siyo kama ilivyokuwa, hata hivyo nimpongeze kwa rai yake na nimuhakikishie kwamba rai ambayo amezungumza ndio rai ya Serikali na ndiyo maana katika Bajeti yetu iliyopita tulieleza kwa mapana kuhusu malengo ya Serikali ya kuhakikisha kwamba tunafikia yale malengo tuliyoyapanga ili wananchi waweze kupata Vitambulisho hivi na hatimaye iweze kurahisisha mambo mbalimbali ikiwemo hayo ambayo yamezungumzwa, lakini na mambo mengine mengi ambayo yanatokana na faida za kuwa na kitambulisho hiki cha uraia.