Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Katika Bajeti ya mwaka 2018/2019 Mkoa wa Katavi ulitengewa kiasi kidogo cha fedha kuliko mikoa yote. Je, Serikali iko tayari kuongeza mgao wa fedha kwa Mkoa wa Katavi kwa kuzingatia jiografia na kilomita za mtandao wa barabara?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIANA S. KAFUPI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru pamoja na majibu mazuri ya Serikali Mkoa wa Katavi ni kati ya mkoa ambayo haijafunguka kwa maana ya kuunganishwa na mikoa mingine. Kitendo cha kupewa kilomita hizo chache kinafanya mkoa huu uendelee kujifunga. Serikali inasema nini katika hilo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo kama haitoshi kigezo cha idadi ya magari yanayopita katika barabara ni tunda la uzuri wa barabara. Serikali inasema nini kwenda kuboresha barabara ili baadaye idadi ya magari iongezeke?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nami ni shahidi kwa sababu nimefika Mkoa wa Katavi mara kadha na Mheshimiwa Kapufi anafahamu, na ndio maana Serikali hata katika Manispaa yake pale tunawekeza fedha nyingi sana kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu wa barabara za lami. Lakini hata hivyo ni kweli vigezo hivi vimewekwa kwa mujibu wa utaratibu kama pale itakapobidi tutaangalia nini kifanyike kuhakikisha kwamba Mkoa wa Katavi unapatiwa fedha za kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo naomba nikuhakikishie kwamba jukumu la wizara yetu yale maeneo yenye changamoto kubwa tutahakikisha kwamba kama maoni yako ulivyotoa hayo tutahakikisha jinsi gani tunaipa nguvu. Na ndio maana hata katika addition finance ya sasa hivi ambayo bado hatua disclose tumeweka kipaumbe kwa ajili ya kuongeza katavi kupata fedha nyingi za ziada nini kifanyike katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hata hivyo katika suala nzima la traffic ya magari kama ulivyosema ni jukumu la Serikali sisi tunahakikisha kwamba tunaimarisha miundombinu ya barabara hizo lengo kubwa ni kwamba barabara zikifunguka magari mengi yatapita. Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kwa hiyo Mheshimiwa Kapufi usihofu Serikali ipo kwa ajili yakuwahudumia wananchi.

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Katika Bajeti ya mwaka 2018/2019 Mkoa wa Katavi ulitengewa kiasi kidogo cha fedha kuliko mikoa yote. Je, Serikali iko tayari kuongeza mgao wa fedha kwa Mkoa wa Katavi kwa kuzingatia jiografia na kilomita za mtandao wa barabara?

Supplementary Question 2

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Halmashuri ya Uvinza ni halmashauri ambyao kijiografia na kimuundo imekaa katika mazingira magumu sana. Lakini kwenye mgao wa bajeti Halmashauri ya Uvinza imekuwa ikipata pesa dogo, na huku inashindwa kutekeleza miradi ya kimaendeleo katika halmashauri yake. Mheshimiwa Waziri ni shahidi aliona ukubwa wa jimbo na mazingira jinsi yalivyo na alituahidi kutuongezea fedha katika mgao wa bajeti.

Je, Mheshimiwa Waziri katika bajeti ya 2019/2020 umezingatia kuongeza pesa za maendeleo katika Halmashauri ya Uvinza?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nami nilikuwepo Uvinza mara kadhaa na juzi juzi nilikuwanae Mheshimiwa Mbunge. Na ni kweli ukitoka makao Makuu ya uvinza mpaka unafika kule kalya karibu kilomita 300 na jimbo kweli ni kubwa, kwa hiyo, jukumu la Serikali tutafanya kila liwezekanalo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio maana katika bajeti ya mwaka huu kuna fedha kidogo tumeiongeza Mheshimiwa Mbunge na hata katika kipaumbele tukaona hata pale mjini kidogo japo angalau tuongeze na tabaka la lami.

Kwa hiyo, kuna bajeti ya kuweka tabaka lami pale mjini lakini hata hivyo tunajua kwamba changamoto kubwa ipo katika Uvinza kwa siku za usoni tutaendelea kwa kuifanyia kazi eneo hili kwa sababu kasungura kenyewe kadogo tutajitahidi kufanya kila liwezekano lengo kubwa ni kuimarisha Uvinza iende vizuri.

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Katika Bajeti ya mwaka 2018/2019 Mkoa wa Katavi ulitengewa kiasi kidogo cha fedha kuliko mikoa yote. Je, Serikali iko tayari kuongeza mgao wa fedha kwa Mkoa wa Katavi kwa kuzingatia jiografia na kilomita za mtandao wa barabara?

Supplementary Question 3

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri pale Mtwara Mjini Manispaa ya Mtwara mjini nimekuwa naulizia barabara kwa muda mrefu barabara ya kutoka Mikindani, Lwelu mpaka Dimbuzi lakini barabara ya kutoka kata ya ufukoni, Mbaye mpaka Mbawala chini. Lakini barabara ya kutoka Mtawanya mpaka Namayanga. Barabara hizi nimekuwa nikizungumza ndani ya Mbunge hapa kwa muda mrefu na hivi sasa TARURA imekuwa inasuasua kuzitengeneza barabara hizi ambazo ni muhimu kwa wananchi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuzitengeneza barabara hizi kwa kiwango cha lami?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuchukue jambo hili kama ulivyosema Mheshimiwa Mbunge. Lakini naomba kuweka takwimu sawa kwamba katika maeneo ambayo tumeyapa kipaumbele sana ni Mtwara Mikindani. Katika mpango wetu wa miji mikakati, miji ile ambayo nane ambayo inahusisha Tanga, Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Ujiji lakini vilevile Mikindani ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndio maana leo ukiangalia ya miaka mitano iliyopita na Mtwara ya leo ni vitu tofauti. Lakini huwezi ukafanya mambo yote kwa siku moja, imani yangu Serikali tutaendelea kupambana lengo kubwa ni kuwahudumiwa wananchi hasa wa Mtwara mikindani na maeneo mengine waweze kuhakikisha barabara zao zinapitika kwa wakati wote.