Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Mkoa wa Rukwa una wilaya nne na hakuna Hospitali ya Wilaya:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika wilaya hizo?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa, nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kazi kubwa ambayo imeifanya katika Mkoa wa Rukwa kutujengea Hospitali za Wilaya. Wakati nauliza swali hili tulikuwa hatujajengewa hospitali hata moja lakini ndani ya kipindi kifupi hospitali na vituo vya afya zimejengwa. Kwa hiyo, naipongeza Wizara na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, hakika kazi ameifanya, Mwenyezi Mungu ambariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo, sasa naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ni lini sasa hospitali hizi zitaanza kufanya kazi na kuletewa vifaa tiba ikiwemo X-ray, MRI na vifaa tiba vingine?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali sasa ina mpango gani wa kutuletea madaktari bingwa, manesi na wafanyakazi wa kada nyingine zote katika hospitali hizo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Bupe Nelson Mwakang’ata, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Serikali tunazipokea pongezi ambazo zinatoka kwa Mbunge na naamini na Wabunge wote wanatoa pongezi hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza anataka kujua ni lini sasa hospitali hizo ambazo zimejengwa zitafunguliwa ili zianze kutoa huduma kama zilivyokusudiwa. Naomba nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine, ni azma ya Serikali na ndiyo maana tulianza na majengo 7 yakamilike na yakishakamilika yaanze kutoa huduma wakati tunaongezea fedha zingine kwa sababu ili hospitali za wilaya zikamilike yanahitajika majengo yasiyopungua 22. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pale ambapo majengo yakishakuwa tayari, vifaa vikipelekwa tutapeleka watumishi ili wananchi wapunguziwe adha ya kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kufata huduma za afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na ujenzi, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba wanakuwepo watumishi wa kutosha. Ndiyo maana tunaenda kuajiri hao 550, ni njia ya kuanza kupeleka wengine sio kwamba 550 ndiyo mwisho, hapana, tutaajiri na wengine kwa kadri bajeti itakavyoruhusu. (Makofi)

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Mkoa wa Rukwa una wilaya nne na hakuna Hospitali ya Wilaya:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika wilaya hizo?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Sisi kwetu pale Kondoa hospitali tunayo lakini hospitali ile inahudumia zaidi ya Halmashauri tatu za Chemba, Kondoa Vijijini, Babati na wakati mwingine mpaka Hanang. Kwa hiyo, mahitaji ya huduma yamekuwa ni makubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, tunaipongeza Serikali kwa kukamilisha ile barabara ya kutoka Dodoma - Babati. Kunapokuwa na maendeleo na changamoto zinaongezeka sana. Kukamilika kwa barabara ile kumeongeza sana mahitaji ya huduma ya hospitali ikiwemo huduma za dharura. Nimelia sana kuhusiana na suala la ambulance, tuna tatizo kubwa sana la ambulance. Ni lini sasa Serikali itaipatia Hospitali ya Mji wa Kondoa ambulance mpya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Edwin Sannda, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea kwa niaba ya Serikali kupokea pongezi ambazo zimetolewa na Mheshimiwa Mbunge. Mheshimiwa Mbunge wakati anajenga hoja yake anaeleza jinsi ambavyo wananchi wengi wanalazimika kwenda kutibiwa kwenye Hospitali ya Kondoa Mji na hii tafsiri yake ni kwamba huduma inayotolewa pale ni nzuri ndiyo maana wananchi wanalazimika kutoka hata Chemba kwenda kupata huduma pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Serikali kuhakikisha kwamba inapunguza adha kwa wananchi kutembea umbali mrefu ndiyo maana hata Halmashauri ya Chemba inajengewa Hospitali ya Wilaya. Kwa hiyo, hiyo influx ambayo imekuwepo itapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la msingi ambalo anataka kujua lini Serikali itapeleka ambulance ili kupunguza adha, amesema mara nyingi sana na Serikali ni sikivu, katika mgao ambao utapatikana kwa siku za usoni hakika Kondoa hatutaisahau.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Mkoa wa Rukwa una wilaya nne na hakuna Hospitali ya Wilaya:- Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali za Wilaya katika wilaya hizo?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wilaya ya Nkasi ni miongoni mwa Wilaya ambazo ziko Mkoa wa Rukwa na mpakani, zinapakana na nchi ya Kongo na Burundi na kumekuwa na mlipuko wa magonjwa ikiwepo ugonjwa wa Ebola. Nataka kujua mkakati wa Serikali, haioni ni muhimu sasa kuipa Wilaya ya Nkasi kipaumbele cha kujenga Hospitali ya Wilaya ili kuepukana na matatizo ambayo yanaendelea kujitokeza?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya msingi ni kwamba kwenye orodha ya Hospitali za Wilaya zinazojengwa ndani ya Mkoa wa Rukwa na Nkasi nimeitaja. Inawezekana Mheshimiwa Mbunge alikuwa haijaingia lakini kama hiyo haitoshi hivi karibuni katika mgao wa gari kwa ajili ya chanjo na ameongelea suala la Ebola na Nkasi nayo ipo katika mgao. Kwa hiyo, ni namna ambavyo Serikali imekuwa ikitilia maanani mahitaji na imekuwa ikitekeleza.