Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali imeweka mikakati ya kuhamasisha uvunaji wa maji ya mvua ili kupunguza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi hasa ikizingatiwa kuwa Tanzania kijiografia ipo katika ukanda wenye mvua za kutosha?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini nilikuwa nadhani kuna haja ya Serikali kuwa mfano katika ujenzi wa majengo yake kwa kuweka miundombinu ya uvunaji wa maji kwa mfano kwenye majengo ya hospitali, shule, zahanati na kadhalika. Aidha, nina swali moja la nyongeza. Pamoja na jitihada hizi za kubuni mbinu mbalimbali za uvunaji maji ya mvua, bado kuna uhitaji wa maji katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kigoma, yakiwemo maeneo ya Mwandiga:-

Je, Serikali inatuambia nini au inawaambia nini wananchi wa Mwandiga kuhusiana na upatikanaji wa maji safi na salama?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokitaka kuwahakikishia wananchi wa Mwandiga, mimi nimekwishafika pale na Mheshimiwa Waziri amefika, tumetuma fedha kiasi cha shilingi milioni 400. Tumeagiza wataalamu wetu wa ndani wafanye ile kazi. Mpaka sasa uchimbaji wa mabomba wameshachimba, lakini pia mabomba yameshafika pale na tutajenga tenki zaidi ya lita 150,000 katika eneo la Bigabilo katika kuhakikisha wananchi wa Mwandiga wanapata safi, salama na yenye kuwatosheleza. (Makofi)

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali imeweka mikakati ya kuhamasisha uvunaji wa maji ya mvua ili kupunguza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi hasa ikizingatiwa kuwa Tanzania kijiografia ipo katika ukanda wenye mvua za kutosha?

Supplementary Question 2

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mvua kubwa zilizonyesha hivi karibuni Wilaya ya Korogwe zimeathiri kwa kiasi kikubwa miundombinu ya maji na kusababisha shida ya upatikanaji wa maji.

Je, Mheshimiwa Waziri anasema ni upi mkakati maalum na wa dharura wa Serikali kurekebisha miundombinu hii na kurudisha miundombinu hii na kurudisha huduma ya maji kwa wananchi wa Korogwe Vijijini kama wanavyofanya wenzenu kwenye upande wa barabara?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, maji ni uhai. Namwomba Mheshimiwa Mbunge tukutane leo saa 7.00 ili tujue namna ya kuweza kuwasaidia wananchi wa Korogwe.

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Je, ni kwa kiasi gani Serikali imeweka mikakati ya kuhamasisha uvunaji wa maji ya mvua ili kupunguza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi hasa ikizingatiwa kuwa Tanzania kijiografia ipo katika ukanda wenye mvua za kutosha?

Supplementary Question 3

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kama tunavyojua, maji ni uhai na maji safi na salama yanapunguza sana maambukizi ya magonjwa ya matumbo kama vile kipindupindu. Nataka Mheshimiwa Naibu Waziri aniambie:-

Je, ni lini Serikali itajenga visima vya maji safi na salama katika Jimbo la Musoma Vijijini?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ambacho nachotaka kumhakikishia, pamoja na uchimbaji wa visima, mpaka sasa tumeshasaini mradi mkubwa sana wa Mugango Kyabakari katika kuhakikisha wananchi wa Musoma wanaenda kupata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza. Ahsante sana.