Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Gesi asilia iliyogundulika nchini ni takribani ujazo wa trilioni feet 56:- (a) Je, uwekezaji wa viwanda vinavyotumia gesi asilia kwa ukanda wa Kusini umefikia wapi na ni wa kiwango gani? (b) Je, mpango wa kujenga kiwanda cha kuchakata gesi asilia bado upo?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni wiki iliyopita tu tumepta taarifa ya kuvuja kwa bomba la gesi, suala ambalo ni la hatari lakini ni kudra za Mwenyezi Mungu hakuna madhara yaliyojitokeza. Sasa licha ya juhudi za Serikali kuunganisha viwanda na gesi, nini hatua wanazochukua kunusuru hali ya namna hiyo isijitokeze kwa ajili ya kunusuru maisha ya wat? Swali la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika utawala wa Awamu ya Nne kazi kubwa ilifanyika ya kuhakikisha gesi inazalishwa na kusambazwa viwandani kama njia au nishati mbadala, lakini kwa sasa tunaona nguvu kubwa imewekwa kwenye Stiegler’s na miradi mingine ya umeme wa maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali; Kwa kuwa mradi wa gesi ulikuwa haujatumika kwa asilimia mia moja na tunaona tumehamia mradi mwingine, ni nini mkakati uliopo kuhakikisha mradi wa gesi unazalishwa na unatumika kwanza katika full capacity kabla ya kuhamia miradi mingine? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Anatropia katika swali lake la kwanza ameeleza namna ambavyo taarifa ilitolewa rasmi na TPDC kuhusu kuvuja kwa gesi kwenye maeneo ya Somanga Fungu. Kama anavyofahamu tangu imeanza kujengwa miundombinu ya gesi, tangu gesi imeanza kutumika kwa mara ya kwanza 2004 mpaka sasa ni tukio la kwanza. Kwa hiyo, ni wazi kabisa miundombinu iliyojenga taratibu zote za precaution juu ya masuala ya bomba yalizingatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, taarifa rasmi imetolewa, wataalam wa SONGAs wakishirikiana na TPDC na Wizara ya Nishati walikuwa eneo la tukio na kila kitu kilifanyiwa kazi na kwa sasa kwa kweli hali imetengamaa na tutaendelea kuchukua hatua stahiki kuhakikisha kwamba matukio kama haya hayajitokezi na kama ambavyo inaonesha ni mara ya kwanza. Kwa hiyo, nataka nimtaarifu kwamba hatua zote zitachukuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameulizia namna gani tutaendelea kuwekeza katika miradi ya gesi na amehusisha kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imejielekeza kwenye mradi wa Mwalimu Nyerere Hydro Power. Naomba nimtaarifu Mheshimiwa Anatropia kwamba katika suala zima la uwekezaji wa masuala ya nishati hususan ya umeme, vipo vyanzo mbalimbali; Serikali yoyote lazima itumie vyanzo mbalimbali mbadala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaposema masuala ya gesi, umeme wa maji, umeme wa makaa ya mawe, umeme wa upepo na umeme wa nishati mbadala pia. Kwa hiyo, Serikali ilipoamua kujielekeza kwenye mradi huu wa Mwalimu Nyerere Hydro Power, ni kuhakikisha kwamba lengo la uzalishaji wa megawatt 10,000 ifikapo 2025 linafikiwa kwa mradi huu mkubwa ambao utazalisha megawatt 2,115.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumepata kusema ndani ya Bunge chanzo hiki cha kuzalisha umeme wa maji kina nafuu, kinagharimu shilingi 36 tu kwa unit, lakini pia Serikali inaendelea na uwekezaji wa miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi. Kwa mfano, hata sasa hivi kuna mradi wa kuzalisha umeme wa gesi Mtwara wa Megawatt 300 lakini pia upo Mradi wa Somanga Fungu Megawatt 330.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara nchini Japan, aliambatana na Maafisa kutoka TPDC akiwepo Mkurugenzi Mtendaji lakini pia hivi karibuni ametoka Urusi, kote kule wamezungumza na wawekezaji mbalimbali na amewaalika kwa niaba ya Serikali kuja nchini Tanzania hapa kuwekeza katika miradi ya gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kujielekeza kwenye miradi ya gesi na miradi mingine yoyote ili kupata energy mix ya uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Gesi asilia iliyogundulika nchini ni takribani ujazo wa trilioni feet 56:- (a) Je, uwekezaji wa viwanda vinavyotumia gesi asilia kwa ukanda wa Kusini umefikia wapi na ni wa kiwango gani? (b) Je, mpango wa kujenga kiwanda cha kuchakata gesi asilia bado upo?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa matumizi ya gesi asilia siyo kwa viwandani tu, bali hata majumbani:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba unapeleka gesi asilia kwenye majumba katika maeneo ya Ubungo, Manzese, Vingunguti, Mbagala, Gongolamboto, Tandika, Mwananyamala na Tandale; maeneo ambayo yana wakazi wengi ili kuwasaidia akina mama kupata nishati ya gesi kwa bei nafuu; pia katika kupunguza gharama za mkaa na uhifadhi wa mazingira?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Mariam Kisangi anapozungumzia masuala ya usambazaji wa gesi majumbani, anamzungumzia mwanamke ambaye ndio mtumiaji mkubwa wa rasilimali ya gesi majumbani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimtaarifu kwamba ni mkakati wa Serikali kwamba kwanza mpaka sasa zaidi ya kaya 500 zimeshasambaziwa gesi asilia katika Mikoa ya Dar es Salaam na Mtwara. Kazi inayoendelea sasa kwa mwaka 2019/2020 tuna matarajio ya kaya zaidi ya 1,000 kuzifikia na kazi inaendelea na mpaka sasa vifaa vyote vya kuunganishia yakiwemo mabomba, mita za matumizi ya gesi vimeshafika na vimeshafungwa na vipo katika nyakati za majaribio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, maeneo aliyoyataja ikiwemo Tandale, Mwananyamala, Mbagala na maeneo ambayo Mbunge anawakilisha, nataka nimthibitishie kwamba Serikali imedhamiria na ndiyo maana imetenga katika mpango mzima matumizi ya gesi, kiasi cha futi za ujazo trilioni 0.7 kwa ajili ya matumizi ya majumbani ili kuokoa mazingira pia. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST (K.n.y. MHE. SAED A. KUBENEA) aliuliza:- Gesi asilia iliyogundulika nchini ni takribani ujazo wa trilioni feet 56:- (a) Je, uwekezaji wa viwanda vinavyotumia gesi asilia kwa ukanda wa Kusini umefikia wapi na ni wa kiwango gani? (b) Je, mpango wa kujenga kiwanda cha kuchakata gesi asilia bado upo?

Supplementary Question 3

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Swali la msingi lilikuwa linaulizia mradi wa LNG wa Lindi. Napenda kufahamu kutoka Serikalini, ni lini Serikali italipa fidia wakazi wa Likong’o, Mto Mkavu na Mchinga ambao wapo tayari kupisha mradi huu?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bobali, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza lini fidia italipwa kwa wakazi wa maeneo ya Likong’o, Mchinga na Mitwelo Mkoani Lindi ambao wamepisha eneo kwa ajili ya Mradi huu mkubwa wa LNG. Napenda nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba mwezi uliopita wataalamu wa TPDC na Wizara ya Fedha na Mipango walikuwa ziara katika Mkoa wa Lindi kuhitimisha zoezi zima la tathmini. Matarajio yetu ifikapo Disemba 2019 zoezi la kuanza kulipa fidia kwa wakazi wa maeneo hayo litaanza na litaendelea na hatimaye kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwathibitishie wakazi wa Mkoa wa Lindi ambao kwa kweli kwa muda mrefu wamekuwa wakiulizia fidia hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano sasa iko tayari kuwalipa. Fidia iliyotengwa ni kiasi cha shilingi bilioni 56 na mambo yote yamekamilika na itaanza kulipwa na wakati huo sisi Serikali na wawekezaji tunaendelea na mazungumzo. Ahsante.