Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- TBC ni Shirika la Umma na hutangaza habari na vipindi mbalimbali ili Watanzania wasikie kwa Lugha ya Kiswahili; Tanzania pia ina wageni kutoka nchi mbalimbali duniani waishio nchini. Lakini TBC limekuwa likitangaza taarifa za habari na vipindi vyake vingine kwa lugha ya Kiswahili tu; zamani kulikuwa na kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangazwa kwa Lugha ya Kiingereza ili wageni waishio nchini wasikie lakini sasa hivi hakipo. (a) Je, ni kwa nini TBC ilifuta kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangaza taarifa ya habari kwa Lugha ya Kiingereza? (b) Je, kwa kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili tu hatuoni kwamba tunawanyima wageni fursa ya kujua kinachoendelea nchini?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili y nyongeza, swali la kwanza natambua juhudi za Serikali zinazofanywa kuitangaza Kiswahili ili kiweze kutumika duniani mpaka kufikia kwamba Kiswahili sasa ni lugha rasmi inayotumiwa SADC, hatua hizo zinazofanya Serikali ni nzuri lakini ninalo swali moja.

Je, kwa kipindi hiki TBC kama TBC ina mkakati gani wa kuwa na translate kwenye vipindi vyake anaye translate Kiswahili kwenda kingereza, na kingerez akwenda Kiswahili wakati anatangaza taarifa zake za habari?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni ukweli usiopingika kwamba kuna television na redio za TBC. Je, TBC kama TBC ina mkakati gani wa kukuza lugha hii duniani kwa kuongeza masafa yake nikiwa na maana frequency ziweze kusikika kwenye nchin mbalimbali duniani?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza kwa maswali mazuri ya nyongeza, lakini nikianza na swali lake la kwanza ametaka kujua kwamba TBC tuna mkakati gani kwa kuwa na mtafusiri kutoka kwenye lugha ya Kiswahili kwenda kwenye lugha ya kingereza. Kama ambavyo nimejibu kwenye jibu kangu la msingi kwamba kwa sasa hivi tunavyo vipindi mbalimbali ambavyo vinatangazwa kwa lugha. Kwa hiyo, naamini kwamba kupitia hivyo vipindi watu wa mataifa mengine kwa maana ya nchi za nje wanaweza kupata kila kitu ambacho kinaendelea ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija pia kwenye swali lake la pili anataka kujua kwamba tuna mkakati gani wa kukuza lugha ya ksiwahili duniani. Mimi niseme kwamba Mheshimiwa Taska Mbogo anatambua namna gani ambavyo Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa mstari wa mbele katika kukuza Kiswahili, vilevile tunamshukuru sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa sababu ndiye ambaye amewezesha sasa hivi kiswahili kinatumika kwenye mikutano ya SADC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme kwamba sisi kama Shirika la Utangazaji la Taifa mkakati wetu kuhakikisha ya kwamba tunakuza kiswahili na ndiyo maana tumekipa kiswahili kipaumbele katika vipindi vyetu, vilevile tumetengeneza apps mbalimbali ambazo zinapatikana ndani pamoja na nje ya nchi. Kwa hiyo, vipindi vyote ambavyo vinatangazwa ndani ya Tanzania, vilevile kwa kupitia app mbalimbali kwa maana ya mtandao wanapata taarifa mbalimbali ambazo zinatokea katika nchi yetu ya Tanzania, ahsante.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- TBC ni Shirika la Umma na hutangaza habari na vipindi mbalimbali ili Watanzania wasikie kwa Lugha ya Kiswahili; Tanzania pia ina wageni kutoka nchi mbalimbali duniani waishio nchini. Lakini TBC limekuwa likitangaza taarifa za habari na vipindi vyake vingine kwa lugha ya Kiswahili tu; zamani kulikuwa na kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangazwa kwa Lugha ya Kiingereza ili wageni waishio nchini wasikie lakini sasa hivi hakipo. (a) Je, ni kwa nini TBC ilifuta kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangaza taarifa ya habari kwa Lugha ya Kiingereza? (b) Je, kwa kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili tu hatuoni kwamba tunawanyima wageni fursa ya kujua kinachoendelea nchini?

Supplementary Question 2

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri na kazi nzuri ambayo inafanyika na Wizara hii. Pamoja na pongezi hizo naomba niulize swali la nyongeza, yako maeneo mpaka hivi tunavyozungumza yana tatizo la usikivu kwa upande wa TBC, yakiwemo maeneo ya Nyasa kule mipakani, baadhi ya maeneo katika halmashauri ya Wilaya ya Tunduru na hasa yale ya mipakani, badala ya kuwa na usikivu mzuri wa TBC sasa wanasikiliza redio za nje kama kule Nyasa.

Je, Serikali ina mkakati gani kupitia Wizara kuhakikisha maeneo yote sasa yanakuwa na usikivu mzuri ili wananchi waweze kuitumia fursa hii kupitia Shirika la TBC, ahsante sana.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa maswali yake mazuri ya nyongeza, lakini kama ambavyo amezungumza sisi kama wizara tunatambua ni kweli kwamba tatizo la usikivu kwa baadhi imekuwa ni changamoto. Lakini Mheshimiwa Mbunge atakubaliana na mimi kwamba kwa kipindi cha hii miaka minne ya utekelezaji wa Serikali ya Awamu ya Tano kazi kubwa sana imefanyika katika kuhakikisha kwamba tunaboresha masuala ya usikivu wa TBC katika nchi nzima ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi tumeweza kufikia Wilaya 102, lakini wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani tulikuwa tuna Wilaya 52 tu ambazo zilikuwa zinapata usikivu wa TBC. Lakini malengo ambayo tunayo kwa mwaka huu 2019/2020 kwa bajeti ambayo tayari tumeshaipitisha ni kuhakikisha ya kwamba tunaongeza Wilaya 15 kwa maana utoke Wilaya 102 tuweze kuwa na usikivu katika Wilaya 117.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitumie fursa hii kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge pamoja na watanzania nzima kwamba sisi kama Serikali tumejipanga katika kuhakikisha kwamba tatizo la usikivu wa TBC katika nchi nzima ya Tanzania linaboreshwa na niwahakikishie kwamba kwa sasa hivi TBC iko vizuri na tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa sababu imekuwa ikiongeza bajeti kila mwaka lakini lengo kuhakikisha ya kwamba tunaboresha usikivu TBC, ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- TBC ni Shirika la Umma na hutangaza habari na vipindi mbalimbali ili Watanzania wasikie kwa Lugha ya Kiswahili; Tanzania pia ina wageni kutoka nchi mbalimbali duniani waishio nchini. Lakini TBC limekuwa likitangaza taarifa za habari na vipindi vyake vingine kwa lugha ya Kiswahili tu; zamani kulikuwa na kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangazwa kwa Lugha ya Kiingereza ili wageni waishio nchini wasikie lakini sasa hivi hakipo. (a) Je, ni kwa nini TBC ilifuta kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangaza taarifa ya habari kwa Lugha ya Kiingereza? (b) Je, kwa kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili tu hatuoni kwamba tunawanyima wageni fursa ya kujua kinachoendelea nchini?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza, maeneo yote ya mipakani mwa nchi, Mkoa wa Rukwa, Katavi, Kigoma ni Mikoa ambayo haina usikivu wa TBC redio a wananchi wengi wanasikia redio jirani mfano ukienda Kasanga wanasikiliza redio Zambia, ukija Kirando wanasikiliza redio ya kutoka nchi ya DRC na Kigoma wanasikiliza redio za nchi jirani ya Burundi.

Ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya karibu ya redio ili kuwafanya wananchi wasikie taarifa za kutoka kwenye Taifa lao?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri kwa maswali yaliyotangulia, napenda kulijibu swali la Mheshimiwa Kakoso kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu swali hili limejitokeza mara nyingi sana hapa Bungeni naomba tu nisisitize kwamba nchi yetu imekuwa ikitegemea vituo vinane vya kurushia matangazo miaka yote hii vituo vya masafa ya kati mid-wave ambavyo vilikuwa Dar es Salam, Arusha, Mwanza, Kigoma, Dodoma, Songea, Nachingwea na Mbeya. Vituo vyote hivi vya midwave vimechakaa na vingi kwa kweli vimeharibika kabisa haviwezekaniki kutengenezwa kwa sababu vinatumia teknolojia ya kizamani. Ndiyo maana ni karibu miaka kumi ilioyopita tumeanzisha mradi wa kuweza kuboresha usikivu wa redio yetu hii ya Taifa kwa kutumia mitambo ya FM.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Bunge hili linaanza tulianza na vituo vitano vya mpakani, tulianza na Longido, Rombo, Tarime, Kibondo na Nyasa, hali ni nzuri; tukafatia Lushoto na baadhi ya maeneo ya Mtwara. Sasa hivi katika bajeti ya mwaka huu tunahangaika na Pemba, Unguja, Simiyu, Songwe na Njombe. Vilevile tumeingia mkataba na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ambapo tutashambulia maeneo ya Kilwa, Kilombero, Kyela, Itigi na Rungwa na kufanya ongezeko la Wilaya 33 katika kipindi hiki kuweza kusikika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea, tumefika Wilayani kwa Mheshimiwa Kakoso, tayari tumepeleka wataalamu wanaangalia ni maeneo yapi upande wa Ziwa Tanganyika tuweze kuyapelekea mitambo ya FM.

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- TBC ni Shirika la Umma na hutangaza habari na vipindi mbalimbali ili Watanzania wasikie kwa Lugha ya Kiswahili; Tanzania pia ina wageni kutoka nchi mbalimbali duniani waishio nchini. Lakini TBC limekuwa likitangaza taarifa za habari na vipindi vyake vingine kwa lugha ya Kiswahili tu; zamani kulikuwa na kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangazwa kwa Lugha ya Kiingereza ili wageni waishio nchini wasikie lakini sasa hivi hakipo. (a) Je, ni kwa nini TBC ilifuta kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangaza taarifa ya habari kwa Lugha ya Kiingereza? (b) Je, kwa kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili tu hatuoni kwamba tunawanyima wageni fursa ya kujua kinachoendelea nchini?

Supplementary Question 4

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja dogo tu la nyongeza. Shirika la Utangazaji (TBC) ni Shirika la Taifa na linaendeshwa kwa kodi za wananchi wote wakiwepo Wana- CHADEMA, CCM na hata wale ambao hawana chama; lakini ukifungua TBC kila mara utakuta ni shughuli za chama tawala tu ndiyo zinaonyeshwa. Hata kama kwa mfano CHADEMA wamefanya Press Release fulani au chama kingine cha Upinzani huwezi kuona wakiirusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nauliza, kama hili ni Shirika letu la Taifa nasi tunalipia kodi zetu kuliendesha: ni lini sasa TBC itakuwa inarusha vipindi vyake kwa usawa bila upendeleo? (Makofi)

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, TBC haiendeshi kwa upendeleo wowote kwa vyama, ili mradi kwanza ukubali kama kuna vipindi vya kulipia, kama wewe ni mkono wa birika, hatuwezi tukarusha vipindi wakati unatakiwa kulipia. Kwa hiyo, kuna gharama yake pale.

Pili, tukiletewa vipindi tunatangaza. Watuambie lini wametuletea vipindi tumeshindwa kutangaza? Haya malalamiko ya jumla jumla hayatatusaidia hata kidogo. (Kicheko)

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:- TBC ni Shirika la Umma na hutangaza habari na vipindi mbalimbali ili Watanzania wasikie kwa Lugha ya Kiswahili; Tanzania pia ina wageni kutoka nchi mbalimbali duniani waishio nchini. Lakini TBC limekuwa likitangaza taarifa za habari na vipindi vyake vingine kwa lugha ya Kiswahili tu; zamani kulikuwa na kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangazwa kwa Lugha ya Kiingereza ili wageni waishio nchini wasikie lakini sasa hivi hakipo. (a) Je, ni kwa nini TBC ilifuta kipindi cha External Service kilichokuwa kikitangaza taarifa ya habari kwa Lugha ya Kiingereza? (b) Je, kwa kutangaza taarifa ya habari kwa Kiswahili tu hatuoni kwamba tunawanyima wageni fursa ya kujua kinachoendelea nchini?

Supplementary Question 5

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza. TBC imekuwa ikisikika kwenye baadhi ya maeneo ya nchi hii lakini katika Jimbo la Ludewa TBC haisikiki kabisa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba Jimbo la Ludewa na maeneo yake TBC inasikika?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Deogratias Ngalawa naomba niongezee kidogo. Ni kwamba juzi TBC imerusha Mkutano Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi. Kwa hiyo, kusema kwamba TBC ina ubaguzi siyo kweli. Tumekuwa tunafanya kazi na vyama vyote na TBC ni chombo cha Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye jibu la Mheshimiwa Deogratias Ngalawa, ametaka kujua ni lini sasa tatizo la usikivu wa TBC litaboreshwa kwenye Wilaya yake ya Ludewa? Niseme kwamba kwa sasa hivi kwenye mipango yetu ya bajeti ya mwaka 2019/2020 tumejipanga kuboresha mikoa mbalimbali ikiwepo Mkoa wa Njombe, Songwe, Simiyu pamoja na mikoa mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitumie fursa hii kuweza kumhakikishia Mheshimiwa Deogratias Ngalawa kwamba tatizo la usikivu wa TBC kwenye Wilaya yake na vilevile Mkoa mzima wa Njombe litaboreshwa muda siyo mrefu. Ahsante sana.