Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI (K.n.y. MHE. ENG. RAMO M. MAKANI) aliuliza:- Utekelezaji wa Mpango wa Kaya Maskini katika Jimbo la Tunduru Kaskazini una changamoto nyingi sana zinazolalamikiwa na Wananchi:- Je, Serikali itachukua hatua zipi za makusudi kurekebisha kasoro hizo ili wananchi wapate kunufaika vema zaidi na huduma za Mfuko huo?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza maswali ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Eng. Makani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, nimpongeze Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana na Naibu wake kwa utendaji mzuri wa kazi. Pamoja na majibu hayo naomba maswali madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ni lini Serikali itashughulikia changamoto katika kaya za vijiji kwenye Tarafa za Nakapanya, Matemanga, Nampungu na Mlingoti? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini Serikali itapitia upya utaratibu wake na kuhakikisha kwamba wanufaika wanakuwa ni wale wenye kaya maskini na siyo wale wenye uwezo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba nimjibu maswali madogo mawili ya nyongeza wifi yangu Mheshimiwa Jacqueline Msongozi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kama mwanamke naomba nimpongeze kwa sababu walengwa wengi ambao ni wanufaika wa kaya maskini ni wanawake kwa sababu wameonyesha uaminifu mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika swali kuhusu Tarafa za Napakanya, Matemanga, Nampungu na Mlingoti, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba sasa hivi TASAF tumekuwa katika Awamu ya Tatu na mwezi ujao Oktoba tunategemea kuzindua rasmi sehemu ile ya pili ambapo tumemaliza sehemu ya kwanza. Hizi Tarafa zote nne ambazo amezisema basi walengwa wote wale ambao hawajafikiwa watafikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili, naomba niseme kwamba Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Mpango huu wa Kunusuru Kaya Maskini tumejipanga kuboresha zaidi kuhakikisha kwamba walengwa wote ambao tulikuwa tunawawezesha na sasa hivi wameweza kusimama wenyewe, tutakuwa na mpango mkakati kuhakikisha kwamba wamefuzu tunaita graduation ili sasa waweze ku- phaseout ili tuweze kusaidia wale wengine ambao hawajiwezi kwa sababu wasiojiweza, maskini sana, wazee, walemavu wapo kila siku basi tuendelee kuwahudumia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo, tumeboresha mfumo kuhakikisha kwamba kuanzia sasa hivi tutakwenda kielektroniki ili kuondokana na suala zima la kaya hewa. Niwatake Wabunge wote na Watanzania wote kuhakikisha kwamba wanaendelea kuunga mkono juhudi hizi za Serikali ya Awamu ya Tano kuhakikisha kwamba walengwa wote wanaotokana na kaya maskini ndiyo hao wanaostahili kupewa misaada yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI (K.n.y. MHE. ENG. RAMO M. MAKANI) aliuliza:- Utekelezaji wa Mpango wa Kaya Maskini katika Jimbo la Tunduru Kaskazini una changamoto nyingi sana zinazolalamikiwa na Wananchi:- Je, Serikali itachukua hatua zipi za makusudi kurekebisha kasoro hizo ili wananchi wapate kunufaika vema zaidi na huduma za Mfuko huo?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mpango huu wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) umefanikiwa kwa kiwango kikubwa na umenufaisha nchi na sisi Wabunge tukiwa wamojawapo. Je, Serikali itakuwa sasa tayari kutoa takwimu ni Wilaya, Mkoa na Kijiji gani mpango huu umefanyika vizuri ili iwe mfano kwa Wilaya au Mikoa mingine ambayo imeshindwa kufanya vizuri?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja dogo la nyongeza la Mheshimiwa kaka yangu Mheshimiwa Mwamoto, kama ifauatvyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango mzima huu wa TASAF, takwimu zipo na muda wowote anapozihitaji tutampatia kwa sababu ni zoezi endelevu. Sisi kama TASAF tumejipanga kuonyesha kwamba sasa hivi tutakuwa tunaonyesha zaidi multiply effect ya walengwa wote na mpango mzima mpaka leo hii tumetumia shilingi ngapi ili kuonyesha kwamba impact yake inaonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI (K.n.y. MHE. ENG. RAMO M. MAKANI) aliuliza:- Utekelezaji wa Mpango wa Kaya Maskini katika Jimbo la Tunduru Kaskazini una changamoto nyingi sana zinazolalamikiwa na Wananchi:- Je, Serikali itachukua hatua zipi za makusudi kurekebisha kasoro hizo ili wananchi wapate kunufaika vema zaidi na huduma za Mfuko huo?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Kamati yetu ya Utawala na Serikali za Mitaa tulipotembelea Mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu, tulikuta madaftari mengi wameorodheshwa watu ambao siyo walengwa, ni vijana ambao ni matajiri, wana mali na nyumba nzuri. Tulikwishatoa ushauri kwenye Wizara hii hawa vijana wote waondolewe. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, orodha ile mlihakiki na kuondoa majina hayo?

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba nimjibu swali dogo la nyongeza Mzee wangu Mheshimiwa Lubeleje, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli siku za nyuma kulikuwa na walengwa wengine ambao wana uwezo lakini walikuwa kwenye mpango. Serikali ya Awamu ya Tano hilo tumelidhibiti na hao wote tuliwaondoa. Ndiyo maana pia katika jibu langu la nyongeza nimesema katika sehemu yetu hii ya pili tunakwenda kielektroniki kudhibiti wale wote ambao wanasema wanatokana na kaya maskini lakini kumbe ni kaya maskini hewa. Hilo tumelidhibiti na tumeboresha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.