Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza:- Moja kati ya maombi yaliyowasilishwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati wa ziara yake Mkoani Ruvuma, katika Wilaya ya Songea ni zahanati za Mbangamawe na Magingo zilizoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba zitakapokamilika zipandishwe hadhi kuwa Vituo vya Afya kutokana na ukubwa wake na mahitaji kwa Wananchi:- Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza jukumu hilo muhimu?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kupata nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Awali ya yote naomba kwa niaba ya wananchi wa Madaba niishukuru sana Serikali pamoja na kutoa milioni 900 imetenga tayari milioni 500 kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Wilaya ya Madaba.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile Halmashauri ya Madaba inachangamoto ya wauguzi kwa maana ya wataalam katika eneo la afya na kwa vile Mganga Mkuu sasa tangu amehama ni zaidi ya miezi 3 hatujapata Mganga Mkuu mwingine kwa ajili ya kutoa huduma. Na katika Kituo cha Afya cha Madaba ambacho kinatoa huduma tuna mganga mmoja tu ambaye yuko active. Ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba Madaba inapata Mganga Mkuu na inapata waganga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa vile katika zahanati hizi mbili ya Mbangamawe na Magingo wananchi wapo tayari kuendelea kutoa ushirikiano wa nguvu kazi na baadhi ya vitendea kazi. Ni lini sasa Serikali itatuhakikishia kwamba hizi fedha ambazo Serikali imekusudia kutupa zitapatikana ili wananchi waendelee kutoa nguvu kazi zao na kuhakikisha zahanati hizi zinakamilika na zinageuka kuwa vituo vya afya, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kipekee naomba nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mhagama pamoja na wananchi wa Jimbo lake na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla. Kama kuna sehemu ambayo wananchi wamekuwa wakijitoa katika kuhakikisha kwamba wanatoa nguvu yao ni pamoja na Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza anaulizia suala la mganga ambaye alikuwa amepangiwa na nilikuwa nateta naye kabla sijaja kujibu swali hapa. Kuna mganga alikuwa amepangiwa sasa hivi yapata miezi miwili hajaenda kuripoti naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada tu ya kumaliza shughuli za Bunge leo nitafatilia nijue nini ambacho kimetokea ili nafasi ile kama mganga hajaenda kuripoti basi tumpeleke mganga mwingine kwa ajili ya kwenda kuziba pengo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ameongelea suala zima la upungufu wa watumishi naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo kuna upungufu tunategemea kuajiri hivi karibuni na tutazingatia ikama ili maeneo ambayo yana upungufu mkubwa yaweze kupelekewa waganga.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili anaongelea suala zima la wananchi kujitolea, jambo ambalo limekuwa likifanywa ndani ya Mkoa mzima wa Ruvuma na nini jitihada za Serikali kuhakikisha kwamba pesa zinapelekwa. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge maeneo yote ambayo wananchi wanajitoa kama ilivyo katika Mkoa wa Ruvuma, Serikali itakuwa tayari fedha ikipatikana kuwaunga mkono wananchi.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza:- Moja kati ya maombi yaliyowasilishwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati wa ziara yake Mkoani Ruvuma, katika Wilaya ya Songea ni zahanati za Mbangamawe na Magingo zilizoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba zitakapokamilika zipandishwe hadhi kuwa Vituo vya Afya kutokana na ukubwa wake na mahitaji kwa Wananchi:- Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza jukumu hilo muhimu?

Supplementary Question 2

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina vituo vinne ambavyo vinafanya kazi lakini vichakavu. Pia wananchi kupitia mapato ya ndani na wananchi wenyewe tumejenga kituo cha afya cha Ikuna. Sasa katika hivi vituo vya zamani Kituo cha Kichiwa, Sovi, Matembwe na Lupembe ni lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya kukarabati na kuongeza majengo ili wananchi wa Lupembe waweze kupata huduma kama ilivyo maeneo mengine?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimetangulia kutoa majibu katika swali la msingi. Katika maeneo ambayo tumetenga fedha ili kuhakikisha kwamba huduma ya afya inaboreshwa ni pamoja na jimbo la Mheshimiwa Mbunge na atakumbuka kwamba katika vituo vya afya vya kuboreshwa ni pamoja na Kichiwa ambacho ametaja. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kadri fedha ya kwanza itakavyopatikana eneo la kwanza kupangiwa fedha itakuwa na kituo chake kwa sababu yeye amekuwa mstaarabu sana na amekuwa akifuatilia sana suala hili.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza:- Moja kati ya maombi yaliyowasilishwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati wa ziara yake Mkoani Ruvuma, katika Wilaya ya Songea ni zahanati za Mbangamawe na Magingo zilizoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba zitakapokamilika zipandishwe hadhi kuwa Vituo vya Afya kutokana na ukubwa wake na mahitaji kwa Wananchi:- Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza jukumu hilo muhimu?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtama niishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutupa bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga Hospitali ya Wilaya. Pamoja na shukrani hizi mwaka 2017 Waziri Mkuu alifanya ziara jimboni Mtama katika Kata ya Mtama na majengo ambayo ina idadi ya watu wengi sana na mpaka sasa tuna zahanati alitoa ahadi ya kujenga kituo cha afya. Sasa je, Serikali haioni umefika wakati wa ahadi hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu itekelezwe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Nape Nnauye na wananchi wake wa Mtama kwa kazi kubwa waliyoifanya ya uimarishaji wa kituo cha Afya cha Mnazi Mmoja na hali kadhalika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambayo tumewapelekea fedha. Lakini tukijua wazi kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa ahadi sehemu hii ni jukumu letu la Serikali kwamba tutafanya kila liwezekanalo maeneo yote ambayo viongozi wetu wa kitaifa wametoa ahadi tutaweza kuyashughulikia. Sambamba na hilo hata kule mkoani Kigoma kwa Peter Serukamba kuna scenario kama hiyo zote tunaenda kufanyia kazi kwa kadri tutakavyokuwa tumejipanga, hakuna shaka.

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza:- Moja kati ya maombi yaliyowasilishwa kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu wakati wa ziara yake Mkoani Ruvuma, katika Wilaya ya Songea ni zahanati za Mbangamawe na Magingo zilizoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Madaba zitakapokamilika zipandishwe hadhi kuwa Vituo vya Afya kutokana na ukubwa wake na mahitaji kwa Wananchi:- Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza jukumu hilo muhimu?

Supplementary Question 4

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana ni kwa nini Kituo cha Afya Nemba ambacho ni kipya na ujenzi umekamilika hakianzi kutoa huduma?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba kule kwake kulikuwa na changamoto kubwa sana na ndio maana tulianza na ujenzi wa kituo kile cha afya cha Yakanazi lakini kazi kubwa inaendelea ujenzi wa hospitali sasa wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo tumejenga vituo vya afya 352 na vituo hivi tumeshaanza kuwakilisha kwamba vingine vinapata vifaa na hivi sasa tunawasiliana na wenzetu MSD katika vile vituo vyote ambavyo vimekamilisha vifaa viweze kupatikana na kupeleka wataalam wetu, na lengo kubwa ni vituo hivi viweze kufunguliwa. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Oscar wala usiwe na hofu kituo kile kitafanya kazi vizuri kama ulivyopigania humu Bungeni na wananchi wako watapata huduma vizuri bila mashaka ahsante sana.