Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Primary Question

MHE. ANDREW J. CHENGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi yake ya kujenga barabara za Mji wa Bariadi kwa Kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa majibu yake mazuri. Napenda nithibitishe kabisa kwamba jibu lake ni sahihi na nimshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, alikuja Bariadi na kuzindua barabara hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya shukrani hizo nina swali moja tula nyongeza.

Mheshimiwa Spika, chini ya mradi huu halmashauri ya Mji wa Bariadi imenunua vifaa mbalimbali kwa kuendeleza maboresho hayo ikiwemo magari ya maji taka, grader na vifaa vingine. Vifaa hivi viko bandarini kwa muda mrefu sana; na hili siyo kwa Bariadi tu lakini kwa vifaa kama hivyo kwa miji mingine ambayo iko chini ya mradi huu ambao unafadhiliwa na World Bank.

Mheshimiwa Spika, napenda nifahamu suala la VAT kwa miradi inayotekelezwa na Serikali ambayo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alishalitolea maelekezo, ni lini sintofahamu hii kati ya TAMISEMI na Wizara ya Fedha itamalizika ili vifaa hivi vitoke bandarini viende vikafanye kazi iliyokusudiwa chini ya mradi huu? Naomba majibu.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa hii, na nimshukuru Mheshimiwa Andrew Chenge Mtemi kwa swali hili muhimu. Pia nimshukuru yeye kwa sababu ni mmoja wa wajumbe wa Kamati yetu ya Bajeti, Kamati inayofanya kazi kubwa katika kuishauri Serikali na kutoa maelekezo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo ni sahihi na tayari tulishaanza kuyafanyia kazi kupitia Sheria ya Fedha ya Mwaka 2018, Sheria ya Fedha ya mwaka 2019 na sasa tunaanza mchakato wa Sheria ya Fedha ya Mwaka 2020 ambapo nina uhakika tulikofika sasa tutaweza kushughulikia tatizo hili la miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia tutaweza kuikamilisha katika mwaka huu wa fedha. Ahsante sana. (Makofi)