Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa Gridi ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwanza tunaishukuru sana Serikali wananchi wa Mkoa wa Katavi kwa kutuletea mradi mkubwa sana huu ambao utatusaidia katika Mkoa wetu wa Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mradi huu wa Mkoa wa Katavi ni mradi wa mkakati, Mkoa wa Katavi tunataka kujenga bandari na vilevile tunataka standard gauge inafika katika Mkoa wetu wa Katavi. Na mradi huu unaenda kwa kusuasua sana ninavyoongea sasa hivi nilikuwa naongea na Meneja wa TANESCO wa Mkoa wangu wa Katavi mradi unaenda kwa kusuasua, tunaomba tupate majibu mazuri lini mradi huu utaanza na utaisha lini ili kwa manufaa ya wananchi wa Katavi kwa sababu tuna malengo ya kupata viwanda ndani ya Mkoa wa Katavi tumechelewa sana tunataka viwanda ili tuweze kufaidika na Serikali yetu ya Awamu ya Tano? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na vilevile swali langu la pili kwa kuwa Mkoa wa Katavi kuna vijiji vingi sana na umeme wa REA bado haujawafika, ni lini umeme wa REA utatufikia katika vijiji vyetu? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri katika eneo hili napenda pia nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia mradi huu mahususi wa North West Grid. Kwanza ni lini mradi utaanza mradi umeshaanza kupeleka Grid ya Taifa katka maeneo ya Katavi na kwa hatua ya kwanza tumeanza na utekelezaji wa kuutoa umeme wa Grid kutoka Mjini Tabora kama ilivyosoma katika swali la msingi kupitia Ipole, Inyonga na hatimaye Mpanda. Umbali wa takribani kilomita 381 na utekelezaji umeanza na tunatarajia mradi kukamilika kabla ya mwezi Mei mwakani, kwa hiyo wananchi wa Katavi watakuwa wameshapatiwa umeme wa Grid kabla ya mwezi Mei Mwakani huo ni Awamu ya I ya utekelezaji wa mradi huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Awamu ya II, mradi utaanza kutekelezwa kuanzia mwakani mradi ambao unatokea kimsingi Iringa, Mbeya, Sumbawanga na baadaye kutoka Sumbawanga, Mpanda na hatimaye Kigoma umbali wa takribani kilomita 1384 kwa ujumla wake mpaka Nyakanazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika awamu hii eneo hili litaanzwa kutekelezwa kwa maana nyingine mwanzo mwa mwaka lakini utaisha mwaka 2022. Mradi huu ni muhimu sana kwa sababu unaunganisha kati yetu na nchi ya Zambia kwa umeme wa kilovoti 400 na umeme utakapopatikana maeneo ya Katavi wananchi wa Katavi wataweza sasa kufanya shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa viwanda. Kwa hiyo, nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya wananchi wa Katavi wavute subira mradi wakati unatekelezwa na utakamilika kama nilivyotaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali la pili kuhusu vijiji ambavyo havijapata umeme katika Mkoa mzima wa Katavi. Mkoa wa Katavi bado vijiji 132 havijapata umeme na vijiji vyote tumeviingiza kwenye mpango wa REA Awamu ya II unaoanza mwezi Februali hata hivyo vile vijiji ambavyo vinatekelezwa na mkandarasi kwa sasa vitakamilishwa vyote ifikapo mwezi Aprili mwaka huu 2020.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa Gridi ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kumekuwa na tatizo kubwa sana la kukatika kwa umeme wakati mwingine kwa siku nzima au hata zaidi ya siku kwenye visiwa vya UKerewe kila wakati mvua inaponyesha. Ningeomba Mheshimiwa Waziri awaambie wananchi wa Ukerewe ni lini tatizo hili litakoma ili wafurahie huduma ya umeme kama yalivyo maeneo mengine nashukuru sana?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli eneo la Ukerewe kwa mwezi mmoja uliopita umeme ulikuwa umekatika sana umesababishwa na sababu moja tu, wavuvi wanaovua kutoka eneo la Kisolia ambapo ni mwanzo wa kuingilia kutoka Bunda kuelekea Lugenzi wamekuwa mara nyingi sana wakikata nyaya wakati wa uvuvi. Lakini nyaya zile zimekuwa zikitikiswa pia wakati wa mvua inapoambatana na upepo, kwa hiyo, ni kweli maeneo ya Ukerewe yamekuwa yakipata changamoto kwa kukatika kwa umeme kipindi hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hatua tulizochukua kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge na wananzegwa wananchi wa Ukerewe ni kwamba kwanza tumeanza kujenga kebo ya kutoka Kisolia kwenda Lugenzi ambapo ni kilomita nne na tume-commit shilingi bilioni 375 na ujenzi umeanza tutafunga kebo tutaipitisha juu ili wavuvi waache kuzigusa na hivyo kutakuwa na umeme muhimu sana kwa maeneo hili. Kwa hiyo, wananchi wa Ukerewe wavumilie kipindi cha wiki mbili zinazofuata mradi utakamilika ili umeme uwe ni uhakika zaidi kwa maeneo ya UKerewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipe nafasi kidogo kwa sababu ni suala la Ukerewe nitoe tangazo kwa wananchi sio wa Ukerewe peke yake ingawa Mheshimiwa Mbunge hajaliuliza, kumekuwa na changamoto kwa wananchi wa Ukerewe hasa watumiaji wadogo wa umeme kutozwa shilingi 2500 kwa unit kinyume na utaratibu na sheria ya umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nitoe tangazo kwa wananchi wa Ukerewe wasikubali kutoa shilingi 1000 kwa unit kwa sababu wananchi wote wa Ukerewe ni sawa na Watanzania wengine ambao wanatumia unit 75 ambao wanatakiwa walipe shilingi 100 per unit badala ya 2500 per unit.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe tangazo hili Mheshimiwa Mbunge anifikishie, lakini nimuombe Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe alisimamie na Meneja wa TANESCO alisimamie ili mwananchi yoyote atakayepatikana akitozwa hivyo kupitia kwa mkandarasi basi atoe taarifa mara moja na Serikali ichukue hatua dhidi ya watu ambao sio wazalendo kwa kitendo hicho ahsante. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa Gridi ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 3

MHE. WILLY Q. QAMBALO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, mkandarasi Nipol group anayefanya usambazaji wa umeme katika Mkoa wa Rushu hususani Wilaya ya Karatu kazi yake ya usambazaji ni ndogo sana, hivi sasa pamoja na kwamba muda wake wa ukandarasi unakaribia kuisha lakini bado vijiji vingi vya Kata za Bugeri, Kansai Endamarieki havijafikiwa na umeme. Nini kauli ya Serikali juu ya mkandari huyo ambaye anasuasua?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za ujenzi wa mradi wa REA Awamu ya III mzunguko wa kwanza zinaendelea na mkandarasi Nipol anafahamu kabisa hivi karibuni tulifanya kikao cha wakandarasi wote na kwamba tumewaambia kwamba ifikapo tarehe 30 Juni, 2020 mradi utakuwa umekamilika na watakabidhi vijiji vyote vitakuwa vimejengewa miundombinu ya umeme na kazi ya kuwasambazia wateja itaendelea.

Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge baada ya kipindi cha maswali na majibu tuonane ili tuweze kuzungumza zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimthibitishie tu usimamizi umeimarishwa na ni muagize mkandarasi Nipol kwa niaba ya Waziri wa Nishati kwamba azingatie dead line iko pale pale na aitaongezwa muda wowote kwa wakandarasi wote nchini lazima wakamilishe tarehe 30 Juni, 2020 ili uunganishaji pamoja na miundombinu. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa Gridi ya Taifa Mkoani Katavi?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niipongeze Serikali kwa kusambaza umeme maeneo mengi katika nchi yetu lakini najua kipaumbele moja wapo cha Serikali ni kulenga zile Taasisi zenye kutoa huduma za jamii kama shule, zahanati nakadhalika. Shule ya sekondari ya Bama iliyoko Kata ya Nangwa Wilayani Hanang licha ya kuomba kwa muda mrefu hadi leo juhudi za kuomba huo umeme haujazaa matunda. Ni nini tatizo ambalo linasababisha sekondari hiyo isipate umeme hadi leo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake la nyongeza Mheshimiwa Martha. Kwanza nimpongeze kwa sababu amefuatilia sana kuhusu shule hii, lakini nieleze tu shule hii ipo karibu sana na umeme takribani nusu ya kilomita na tumekuwa tukifuatilia sana halmashauri ile iweze kulipia ili umeme uweze kuingia kwenye hiyo shule ya sekondari. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nashukuru sana kwa kukumbushia hili lakini na mimi nitoe maelekezo wa Mkurugenzi wako na Mwenyekiti wa Halmashauri alipe gharama za kuunganishiwa umeme ili shule hiyo ipate umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie nafasi hii kwa Waheshimiwa Wabunge kwa niaba ya Wakurugenzi na Wenyeviti wa Halmashauri zote nchini wahakikishe wanatenga fedha mahususi kwa ajili ya kuingiza umeme kwenye Taasisi za Umma, hapa tuna maana shule, vituo vya afya, zahanati na Taasisi nyingine. Imekuwa ni changamoto kubwa sana tunapokwenda maeneo yale unakuta shule ipo karibu umeme lakini halmashauri haijalipia. Basi nitoe rai hiyo ili wafanye hivyo ziweze kuunganishiwa umeme na shule ambazo ziko mbali hata kama kijijini hatujapeleka umeme sisi tutapeleka umeme mahususi kwa ajili ya hizo shule za sekondari na vituo vya afya. (Makofi)