Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia Wananchi wa Kiluvya, Madukani, Mwanalugali na Mikongeni ambao wamepisha ujenzi wa njia ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, swali la kwanza kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Pwani especially sehemu hizo zilizotajwa, walisitishiwa tangu 2014 wakati wa Awamu ya Nne, na anasema kwamba watalipa fidia kwa uthamini wa 2018 watu hawa walikuwa wanajenga wakaacha ujenzi na gharama zimepanda.

Je, Serikali iko tayari kulipa hasara ambayo maongezeko ya gharama za ujenzi watakapokuwa wanalipa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa Serikali imekaa kimya muda wote huu. Je Waziri yuko tayari kufuatana na mimi baada ya Bunge ili akaweze kuongea hayo ambayo ameyaeleza hapa wananchi waweze kumuelewa kwa urahisi?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru kwa kufuatilia ili suala hili ni swali lake la pili, lakini pamoja naye niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo ya Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini na Chalinze kwa kufuatilia hili swali kwa karibu.

Mheshimiwa Spika, lakini nataka nimueleze Mheshimiwa Mbunge na na wananchi wa Mkoa wa Pwani wakati wa mwaka 2014/2015 Serikali ilipo design mradi huu wa Kinyerezi, Chalinze, Segera Tanga ulikuwa kabla haujafanywa maamuzi ya ujenzi wa mradi mkubwa wa Rufiji Hydro Power.

Kwa hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani na kuamua kutekeleza mradi huu kwa nia ya kufanya nchi iwe na umeme wa kutosha ilibidi ifanye utaratibu wa kuuisha upembuzi yakinifu kwa sababu mradi huu sasa wa Rufuji Hydro Power kuna njia mpya ambayo itajengwa ya KV 400 kutoka Rufiji, Chalinze ambayo inaelekea Dodoma.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndiyo suala ambalo limepelekea fidia hii kuchelewa kwa sababu lazima iuishwe, lakini tunatambua fidia inalipwa kwa mujibu Sheria na Kanuni. Kwa hiyo, malipo ya fidia hii kwa wananchi wa Mkoa wa Pwani yatazingatia Sheria na Kanuni za nchi ambazo zinapeleka malipo haya ya fidia.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili amesema je, nipo tayari?, nataka nimualifu Mheshimwa Mbunge na mimi pia ni mdau ni Mbunge wa Mkoa wa Pwani hivi karibuni tu nilifanya ziara Kata ya Pera Jimbo la Chalinze na niliongea na wananchi suala hili.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo namkubalia kwamba baada ya Bunge hili au wakati wowote tunaweza tukafanya ziara katika maeneo ya Kibaha, maeneo ya Jimbo la Segerea, maeneo ya Kibaha Vijijini, maeneo ya Chalinze kuzungumza na wananchi na kwamba kwa kweli kama nilivyosema wakati wa bajeti yetu wataona tumedhamilia kabisa kulipa hii fidia kwa sababu mradi huu unaanza mapema Julai, 2020 na kukamilika Desemba, 2022, ahsante sana.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia Wananchi wa Kiluvya, Madukani, Mwanalugali na Mikongeni ambao wamepisha ujenzi wa njia ya umeme?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, mradi wa kuchakata gesi wa LNG Likong’o Lindi. Ni muda mrefu sana wananchi wa eneo la Likong’o hawafanyi shughuli zao za kilimo ili kujipatia mahitaji yao ya msingi na kuongeza uchumi wao binafsi na mradi huu ni muhimu sana kwa wananchi wa Lindi kwa ajili ya kuongeza uchumi wao, lakini si hilo tu bali ni Taifa kwa ujumla kwa sababu ni mradi mkubwa sana, Mheshimiwa Waziri.

Je, ni lini wananchi hawa wa Lindi hasa Likong’o watalipwa fidia zao kwa ajili ya kuinua vipato vyao na kuacha eneo hilo liendelee na kazi iliyokusudiwa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la Mheshimiwa mama Salma Kikwete Mbunge wa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais juu ya suala la fidia la eneo la Likong’o ambalo tunatarajia kutekeleza mradi mkubwa wa kujenga kiwanga cha kuchakata gesi asilia ambayo imegundulika kwa wingi katika Mikoa ya Mtwara kwa kiasi cha trilioni cubic feet 55.

Mheshimiwa Spika, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge mama Salma na wananchi wa Mkoa wa Lindi Serikali inatambua umuhimu wa mradi huu na ndiyo maana Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo ya kukwamua mkwamo ambao uliokuwepo kwa Wabia wale wa mradi wa kutaka kila mmoja tuzungumze naye kwa wakati tofauti na mazungumzo hayo yameanza kati ya kampuni ya BP SHELL pamoja na STATOIL ambayo kwa sasa hivi inajulikana kama equinor.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mazungumzo haya yameanza kwa kwa kuwa sasa hivi kuna kila dalili ya mradi huu kufanyika na taratibu zinaendelea na Kamati ya Wataalam wameshakaa suala la fidia kwa eneo hili limeshafanyiwa kazi na naomba nimualike Mheshimiwa Mama Salma Kikwete na Wabunge wote wa Mkoa wa Lindi kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati kwenye mkutano wa tarehe 21 mwezi huu wa 5 wa ku-raise awareness ya mradi huu na ambapo pia taarifa na uhakika wa ulipaji wafidia baada ya tathimini kukamilika itatolewa.

Mheshimiwa Spika, tunawashukuru wananchi wa Mkoa wa Lindi kwa uvumilivu wao tunakuja tarehe 21 na kwamba kila kitu Serikali imekiweka vizuri, ahsante sana.