Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA) aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kuwasadia wananchi walioweka amana zao katika Benki ya FBME.

Supplementary Question 1

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa tatizo hili sio mara ya kwanza kutokea hapa nchini, je, Serikali ina mkakati gani wa makusudi kuzuia jambo hili lisitokee tena kupunguza usumbufu kwa wananchi wetu?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, Serikali mikakati iliyonayo ni kusimamia sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 kama inavyoelekeza kuhusu unazishwa na usimamiaji wa uanziswaji wa taasisi za kifedha ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, na Serikali mmeona kwa sasa imekuwa, imeweka udhibiti wa hali ya juu kuhakikisha taasisi zote za kifedha zinafanya kazi kulingana na sheria ili kuzuia changamoto hizi wanazozipata wateja wetu.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA) aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kuwasadia wananchi walioweka amana zao katika Benki ya FBME.

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na majibu ya Serikali, kuna mkanganyiko mkubwa na mlolongo mrefu kwa watu hawa kupata haki zao.

Sasa kwa kuwa Benki Kuu ndiyo guarantor wa hizi benki, kwa nini Serikali isimalizane na hawa wateja kwa niaba ya hii benki halafu Serikali sasa ibaki ikishughulika na benki hii wakati wananchi wakiwa wanaendelea na shughuli zao, hasa ikizingatiwa kuwa ziko taarifa kwamba, wamiliki wa benki hii wametushitaki, wameishitaki Serikali kutokana na hatua walizochukua?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, benki inapofilisika, benki inaponyang’anywa leseni yake ya kufanya kazi, hatua zote za ulipaji wa wateja wa beki hiyo au taasisi hiyo ya kifedha, imetajwa katika sheria ya mabeki na taasisi za fedha kifungu cha 39(2) na (3), ambako kuna maeneo mawili.

Mheshimiwa Spika, kwa wale ambao wana amana zilizo chini ya 1,500,000 hulipwa fedha zao zote, kwa wale ambao amana zao ni zaidi ya hiyo, hulipwa kwa kutumia sasa sheria ya ufilisi baada ya kujiridhisha na madeni na mali halisi ya benki hiyo au taasisi ya kifedha kama ilivyoelezwa.

Mheshimiwa Spika, lakini naomba niliambia Bunge lako Tukufu kwamba, siyo kwamba wamiliki wa benki ndiyo walioishitaki Serikali, hapana, waliostopisha mchakato huu ni Central Bank ya Cyprus, ambayo wao wanaona wana mandate ya kuweza kulipa wateja wote wa benki hii, wakisahau kwamba kulingana na sheria ya uanzishwaji wa mabenki, wanaotakiwa kulipa ni kule ambako benki hiyo ilikuwa na makao makuu, na makao makuu ya benki hii ya FBME yalikuwa Dar es Salaam lakini shughuli zake nyingi zilikuwa zinafanyika nchini Cyprus.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, mwezi wa nne tarehe 5 mwaka 2019, Serikali mbili zimekutana nchini Cyprus na tayari makubaliano yamefikiwa ya jinsi gani ya kuhakikisha wateja wote wa iliyokuwa benki ya FBME Tanzania na FBME Cyprus wanapata haki zao bila kupoteza chochote katika mchakato huu.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA) aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kuwasadia wananchi walioweka amana zao katika Benki ya FBME.

Supplementary Question 3

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, wananchi wengi wameathirika kwa kukosa fedha zao ambazo waliziweka katika benki hii na Benki Kuu inapotoa leseni au kibali kwa ajili ya kufungua benki, wao wanakuwa ndiyo dhamana.

Mheshimiwa Spika, na kuna methali inasema dhamana ndiyo mlipaji, lakini hata mahakamani unapomchukulia mtu dhamana, akikimbia wewe ndiyo unakamatwa unahusika na suala lile. Kwa nini Benki Kuu isiwalipe hawa watu fedha zao, halafu wao wakaendelea na huo, kwa sababu watanzania wanaathirika na hili.

Sasa maana ya ninyi kuwa dhamana ni nini?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nimesema kwenye majibu yangu ya msingi, uendeshaji wa taasisi za kifedha yakiwemo mabenki imeelezwa wazi kwenye sheria ya mabenki na taasisi za kifedha ya mwaka 2006. Benki Kuu haiwezi kuwa dhamana na kuchukua jukumu la kulipa wateja wote ndiyo maana ikaanzishwa Bodi ya Amana, kama nilivyoeleza, ambayo ina dhamana kubwa ya kuwalipa wateja ambao wanamiliki amana chini ya 1,500,000.

Mheshimiwa Spika, na niseme kwamba, asema wateja wengi wamepoteza, kwa experience tuliyonayo ndani ya Taifa letu, iknapofungiwa benki yoyote au taasisi yoyote ya kifedha, zaidi ya asilimia 90 ya wateja wa benki au taasisi husika ya kifedha, huwa ni wale wenye amana ya 1,500,000 kurudi chini.

Kwa hiyo, hawa asilimia 10 iliyobaki, ndiyo nimesema kwamba, Serikali mbili zimeshakutana, mwezi Aprili, tarehe 5, 2019 na tayari tumeshakubaliana jinsi ya kuliendea jambo hili ili wateja wateja wote sasa waliobaki ambao ni zaidi, waliokuwa na amana ya zaidi ya 1,500,000, waweze kulipwa amana zao.

Name

Salim Hassan Turky

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpendae

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA) aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kuwasadia wananchi walioweka amana zao katika Benki ya FBME.

Supplementary Question 4

MHE. SALIM HASSAN ABDULLAH TURKY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Ukiangalia juhudi za Serikali ya kukuza uchumi huu, sasa hivi jinsi hizi benki zinavyokwenda tunaanza kupata mshituko kidogo. FBME imezama, M Bank nayo imezama, M Bank kama ninafahamu ni benki ya Tanzania hatuwahitaji Ma-Cyprus kuja kutujibu, lakini bado zile dhamana ambazo ni za Serikali, naomba sana kwamba Serikali itoe tamko rasmi kwa sababu wateja ni wengi ambao wanahangaika na Serikali iko hapahapa na hii benki iko hapahapa, na sasa hivi imechukuliwa na benki nyingine ya Serikali yetu.

Kwa hiyo, tunaomba sana tujulishwe hii hatma ya kudai fedha za M Bank, tunazipata vipi kwa uharaka wake? Ili watu waamini kuweka fedha benki maana sasa hivi sasa watu kuweka fedha benki tunaanza kuogopa, tunaona hizooo, zinazama.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kuna usalama mkubwa sana ndani ya Taifa letu, kwenye taasisi zetu za kifedha kwa sababu Benki Kuuu ya Tanzania iko macho na iko makini kusimamia sheria ya kuazisha benki hizi na taasisi za kifedha.

Mheshimiwa Spika, na niliombe sana Bunge lako Tukufu, tunapokuja na sheria ya kusimamaia hizi taasisi za kifedha, muwe mnatuunga mkono, ni kwa sababu tunaona wengi wa wateja wetu wanapoteza fedha kwa kuingia katika mifumo ambayo siyo sahihi na nilishukuru Bunge lako Tukufu kwa kuturuhusu kwenye Bunge letu la mwezi wa 11 kupitisha sheria ya huduma ndogo za fedha na sasa tunawafikia wote kule walipo ili kuhakikisha wateja wetu wote wanakuwa salama.

Mheshimiwa Spika, na niseme, hili la M Bank, kama alivyosema muuliza swali, M Bank imechukuliwa na benki nyingine. Kwa maana hiyo, M Bank siyo kwanza wataja wake wanatakiwa kusubiri mchakato kwa sheria ya ufilisi, hapana. Benki iliyoichukua M Bank, ina jukumu na dhamana kubwa ya kuhakikisha wateja wote wanalipwa na wanalipwa amana zao zote pale wanapozihitaji.

Mheshimiwa Spika, lakini niwaambie watanzania kwamba, kuweka fedha zao kwenye benki zetu ni salama na benki ambayo M Bank imeunganishwa inafanya vizuri na niwaombe waendelee kuacha amana zao huko kwa sababu faida ni kubwa ya kuacha fedha zao kwenyeakaunti zao.