Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Jimbo la Kalenga lina vivutio vya utalii vinavyoweza kuingiza nchi yetu pesa za kigeni kama vile Isimila Stone Age na Makumbusho na Mtwa Mkwawa Mkwavinyika:- Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Iringa Vijijini kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza Pato la Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, ingawa katika maeneo aliyozungumza kuhudu REGROW hajaeleza kiuwazi kwamba itakuwa ni lini makumbusho yatakuwa yameanza. Nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ni kwamba, wananchi wa Jimbo la Kalenga hasa katika Kata husika ya Kalenga hawanufaiki na chochote kupitia Makumbusho haya ya Mkwawa Mkwavinyika, zaidi wanapata zile fedha ndogo ndogo kupitia watalii ambao wanakuja kununua bagia, maandazi na mbogamboga. Sasa sijui Serikali ina utaratibu gani kuhakikisha kwamba wananchi wa Kalenga hasa katika Kata husika ya Kalenga wananufaika na Makumbusho haya ya Mkwawa Mkwavinyika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni kwamba, kutokana na utaratibu ambao umeanzishwa na Serikali kuhakikisha kwamba tunajenga au kuboresha barabara ya Iringa Mjini kuelekea Ruaha ambayo iko katika utaratibu wa REGROW ningependa kufahamu kupitia Mheshimiwa Waziri kwa sababu Ruaha National Park ni mbuga kubwa katika Bara la Afrika na Tanzania kwa ujumla. Ningependa sasa kufahamu, je, utaratibu wa ujenzi wa barabara hii ambayo inaenda Ruaha National Park ukoje ukizingatia kwamba Wizara ya Ujenzi imeshaeleza kwamba itaijenga barabara hii, lakini vile vile kwa sababu inakidhi mahitaji ya Wizara ya Maliasili, je, kuna mawasiliano yoyote kati ya Wizara hizi mbili kujua barabara hii itaanza kujengwa lini?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu maswali mawili ya Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa kwanza niwape salamu Wanayanga wote, kamwene, mnogage.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya salamu hizo kwa Wanayanga, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Mgimwa kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ni kwamba, Mtwa Mkwavinyika Mnyigumba Mwamuyenga ni shujaa wa Taifa, ni alama ya Utanzania wetu na ni miongoni mwa watu mashuhuri ambao sisi watoto wa Tanzania tunajinasibu nao. Pia hawezi kuwa mtu ambaye anaweza kutupa historia inayoleta faida kwa watu wa Kalenga peke yake, kwa hivyo mafanikio yatakayopatikana kutokana na Mtwa Mkwavinyika Mnyigumba kuwa ni Mtwa wa Wahehe na ngome yake kuwa pale Kalenga ni kuvutia watalii kuja katika eneo lile na hiyo multiplier effect anayoizungumza kwamba watalii watalala, watatembelea maeneo mbalimbali, watajifunza historia ya Wahehe, wataacha pesa pale, lakini sio lazima moja kwa moja kwa kuwa Mtwa Mkwavinyika alikuwa wa eneo lile, basi iwe tu ni kwa faida ya watu wa pale, huyu ameshakuwa alama ya Taifa. Kwa hivyo, kinachopatikana kutokana na utalii kinaingia kwenye taasisi za Serikali na wananchi wanafaidika na kodi inayotokana na Sekta ya Utalii kwa ujumla wake na pia wananchi wanafaidika kwa kufanya shughuli mbalimbali ambazo zinaendana na mnyororo mzima wa kazi au shughuli za utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusu barabara ya kutoka Iringa kwenda Msembe, ni barabara muhimu sana kiutalii na ni barabara ambayo tunaipa kipaumbele cha hali ya juu katika kuifungua circuit ya Kusini hususan kuitumia Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa faida zaidi kiutalii. Pia ni barabara ambayo Serikali katika bajeti hii tutakapokuwa tukitoka hapa tuna uhakika itakuwa imepitishwa na katika mikakati yetu ni kwamba tutaanza sisi wenyewe kuijenga barabara hii japokuwa tayari tuna fedha kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya barabara hii kuunganisha pia na Mradi wa Kuboresha Uwanja wa Ndege wa Nduli. Kwenye uwanja wa ndege wa Nduli uliopo pale Iringa tayari Mkandarasi atatangazwa muda si mrefu, tunabaki na hii barabara ya kuunganisha Iringa Mjini na Hifadhi ya Taifa Ruaha kwenye eneo la Msembe. Kwa hivyo, hii barabara naijua vizuri japokuwa mimi sio Waziri wa uchukuzi wala wa Ujenzi kwa sababu ni barabara muhimu sana kiutalii kama anavyosema Mheshimiwa Godfrey Mgimwa.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Jimbo la Kalenga lina vivutio vya utalii vinavyoweza kuingiza nchi yetu pesa za kigeni kama vile Isimila Stone Age na Makumbusho na Mtwa Mkwawa Mkwavinyika:- Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Iringa Vijijini kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza Pato la Taifa?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Wananchi wa Urambo wanaoishi karibu na hifadhi za misitu wamekuwa na migogoro ya muda mrefu sana na hata kusababisha kuchomewa nyumba zao na mali zao hasa katika sehemu ya Kata ya Nsenga, Lunyeta, Ukondamoyo na Uyumbu. Je, Serikali inawaambia nini wananchi kuhusu lini watakwenda kutatua na hasa kwa vile ninavyokuwa na imani na Waziri husika. Lini anamaliza matatizo haya ili wananchi wafanye shughuli zao kwa raha?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margareth Simwanza Sitta, Mbunge wa Jimbo la Urambo, mama yangu, kwa ufupi tu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia maelekezo ya Mheshimiwa Rais aliyoyatoa Januari 15, 2019 kwa Mawaziri wa Wizara nane ambazo ni wadau wa migogoro ya ardhi, tumefanyia kazi jambo hilo kuhusiana na Lunyeta na maeneo mengine ya Mkoa wa Tabora na mikoa mingine hapa nchini na kwa sasa siwezi kusema nini itakuwa hatma yake, lakini kazi ya Mawaziri imekamilika na tumepeleka mbele ya meza ya Mheshimiwa Rais, tunasubiri mwongozo. Baada ya hapo Waheshimiwa Wabunge na wananchi wote kwa ujumla watapata kujua ni nini itakuwa hatma ya ufumbuzi wa migogoro ambayo imedumu kwa muda mrefu kwenye Sekta ya Ardhi na Maliasili.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:- Jimbo la Kalenga lina vivutio vya utalii vinavyoweza kuingiza nchi yetu pesa za kigeni kama vile Isimila Stone Age na Makumbusho na Mtwa Mkwawa Mkwavinyika:- Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Iringa Vijijini kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza Pato la Taifa?

Supplementary Question 3

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba nimuulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, katika historia ya Wahehe, moja ya sifa ni kumpiga Mjerumani na Mjerumani alipigwa katika Kijiji cha Lugalo Iringa na ikasababisha kiongozi wao Zelewisky kupigwa na kaburi lake liko pale. Je, Serikali sasa haioni kwamba kile kilikuwa ni kivutio kizuri tosha mpaka sasa hivi kimetelekezwa kwa miaka yote na Waziri yuko tayari kufika pale?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venance Mwamoto, kamwene bwana!

Mheshimiwa Mwenyekiti, niko tayari kufika katika eneo hili na wakati wowote muda ukipatikana tunaweza tukachomoka na Mheshimiwa Mwamoto tukaenda kuona eneo hili, lakini kwa ujumla wake tu maeneo yote ya malikale na maeneo ya makumbusho kwa kweli tumeyafanyia mkakati mzuri sana wa kuyaboresha kwa sababu Idara ya Malikale ambayo iko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii ilikuwa ina uwezo mdogo sana wa kuyasimamia maeneo haya kifedha, kwa hivyo ilikuwa inayaendeleza kidogo kidogo. Kwa kuzingatia umuhimu wa maeneo haya, kihistoria lakini pia kama urithi kwa nchi yetu ambao unapaswa kudumu kwa vizazi na vizazi, tumeamua kuyakabidhi baadhi ya maeneo nyeti ikiwemo eneo la Kalenga na eneo la Isimila kwa taasisi za uhifadhi ambazo zina msuli mkubwa kidogo kifedha kwa mfano TANAPA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano eneo la Kalenga na eneo la Isimila na vivutio vyote vilivyoko Mkoa wa Iringa vya Malikale tumewakabidhi Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ili waweze kuviendeleza na kuvisimamia.

Kwa hivyo tumegawa maeneo haya kutokana na shirika lipi ambalo lina msuli mkubwa kifedha, liko jirani na maeneo haya. Kwa hivyo, maeneo mengi kwa kweli kwa sasa yataendelezwa yatakuwa na hadhi ya kisasa na yatatoa huduma nzuri zaidi kwa watalii wa ndani na wa nje.