Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Mafuriko yaliyotokea Mlalo mwaka 1993 yalisababisha uharibifu mkubwa kwa barabara inayounganisha Tarafa za Umba na Mtae:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kukarabati barabara hiyo muhimu?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu hayo, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

(a) Kwa kuwa barabara hii ya Mtii – Mtae – Mnazi, kilometa 12.7 pamoja na Kwekanda – Hekcho – Rugulu hadi Mkomazi kilometa 17.5, zote hizi tumeziweka katika bajeti ya Mwaka wa Fedha 2019/2020 na bajeti tayari tumeshapitisha. Je, Serikali inatoa tamko gani kwa wananchi wa Mlalo?

(b) Kwa kuwa, barabara hizi siyo tu kwamba zinaunganisha Tarafa za Umba – Mlalo na Mtae, lakini pia zinaunganisha wilaya jirani za Korogwe na Same: Je, Serikali haioni kwamba kwa kutofanya wepesi wa kurekebisha barabara hizi inakuwa ni kikwazo kwa fursa za kiuchumi kwa wananchi wa Mlalo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kipekee kwanza naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Shangazi, amekuwa akipigia kelele sana kuhusu barabara hii ya kwenda Mtae na mara nyingi sana amefika ofisini kwetu. Naomba nimpongeze katika hilo.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake anaulizia kwamba tayari bajeti imeshapitishwa, nini tamko la Serikali kuhusiana na ujenzi wa barabara hiyo? Bajeti ambayo imepitishwa kwa ajili ya Wilaya ya Lushoto ni jumla ya shilingi bilioni 1.8. Kama katika bajeti yao na barabara hii ipo, ni vizuri wakahakikisha kwamba barabara hii ni muhimu ikaanza kutengenezwa mapema.

Mheshimiwa Spika, kwa vile bajeti inahusu shilingi bilioni 2.5 ambayo siyo rahisi, Bajeti ambayo imepitishwa ni
1.4 na wao wanahitaji shilingi bilioni 2.5; na kilometa katika Wilaya ya Lushoto ni jumla ya 935. Naomba Meneja wa TARURA ahakikishe katika vipaumbele vya barabara za kutengenezwa iwe pamoja na barabara hii.

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, anaulizia je, Serikali haioni umuhimu wa kutengeneza barabara ya kuunganisha kwenda Lushoto na wilaya nyingine kwa maana ya fursa ya kiuchumi? Ni ukweli usiopingika kwamba maeneo ambayo barabara haipitiki tunakuwa tunawanyima wananchi fursa ya kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiopingika pia kwamba bajeti yetu haiwezi ikakidhi kwa mara moja maeneo yote. Naomba Mheshimiwa Mbunge aendelee kuvuta subira na yeye mwenyewe ni shuhuda, tangu tumeanzisha chombo cha TARURA kazi inayofanyika ni nzuri na hakika na barabara hii itawekwa kipaumbele ili iweze kutengenezwa.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Mafuriko yaliyotokea Mlalo mwaka 1993 yalisababisha uharibifu mkubwa kwa barabara inayounganisha Tarafa za Umba na Mtae:- Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kukarabati barabara hiyo muhimu?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Ikola – Kasangantongwe imeharibika sana na mvua zilizonyesha na kusababisha wananchi kushindwa kutumia barabara hiyo na kuanza kutumia njia ya majini ambayo siyo salama.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha kuijenga barabara hiyo ya Kasangantongwe?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) Mheshimiwa Spika, nimepata fursa ya kutembelea Jimbo la Mheshimiwa Kakoso na katika maeneo ambayo barabara zinajengwa unaona thamani ya pesa ni pamoja na Jimboni kwake. Yeye mwenyewe anakiri kwamba barabara hii ambayo anaitaja imeharibika kutokana na mvua ambazo zinanyesha na ni ukweli usiopingika kwamba katika maeneo ambayo mvua ni za uhakika ni pamoja na Jimboni kwake.

Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kumwagiza Meneja wa TARURA ili akaangalie uharibifu wa hiyo barabara namna aone namna ambavyo anaweza angalau akafanya maboresho katika maeneo korofi sana ili barabara hii iweze kuendelea kupitika na wananchi waendelee kufaidi matunda ya CCM.