Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:- Serikali ina mpango wa kufikia uzalishaji wa zaidi ya megawatts 5,000 za umeme ifikapo 2020. Je, ni mkakati gani umewekwa ili kufikia lengo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali na natambua jitihada kubwa sana zinazofanywa na Serikali katika kuongeza uzalishaji wa umeme lakini nina swali moja tu la nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhamasisha na kuwezesha kisera uwekezaji wa miradi midogo midogo ya uzalishaji wa umeme hususan katika maeneo ambayo hayajafikiwa na gridi ya Taifa kama vile Mkoa wa Kigoma?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri katika swali la msingi la Mheshimiwa Katimba. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia wazalishaji wadogo wadogo katika nishati kwa upande wa maeneo ambayo hayana gridi ya Taifa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kama ambavyo tumeeleza katika jibu la msingi, pamoja na kuzalisha umeme mkubwa katika maeneo mbalimbali yenye gridi ya Taifa, bado Serikali inahamaisha sana uzalishaji wa umeme mdogo mdogo katika maeneo ambayo hayajafikiwa na gridi ya Taifa. Katika maeneo ya Kigoma mathalani; wazalishaji wadogo wameshajitokeza, Kampuni ya Nexgen Solar White imeanza kuzalisha megawatts tano ambazo sasa wanafanya majadiliano na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kuingiza kwenye gridi ya Taifa. Kwa hiyo ni matumaini yetu maeneo mbalimbali ya Ujiji ambayo yameshafanyiwa utafiti kwenda mpaka Kaliua kuja mpaka Mkoa wa Tabora wazalishaji wataongezeka zaidi.

Mheshimiwa Spika, katika kuongeza maelezo ya upana zaidi kwenye suala la nyongeza la Mheshimiwa Katimba ni kwamba katika maeneo ya Mkoa wa Kigoma na Uvinza ambayo hayajapitiwa na umeme wa gridi ya Taifa, hivi sasa Serikali imeanza kujenga njia ya kusafirisha umeme mkubwa wa gridi ya Taifa ili Mikoa ya Kigoma na Katavi nayo ifikiwe na gridi ya Taifa. Sasa hivi ujenzi unaanzia Tabora kupitia Jionee Mwenyewe-Juhudi-Nguruka mpaka Kidawe Mchini-Kigoma, kwa hiyo, hata wazalishaji wadogo wa umeme mdogo mdogo nao wataingizwa kwenye gridi ya Taifa.