Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Wilaya ya Tanganyika haina Mahakama ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya sanjari na kuboresha Mahakama za Mwanzo?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Wilaya ya Tanganyika ni Wilaya kubwa na tarafa zake zimekaa kwa mtawanyiko. Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuharakisha kujenga jengo la mahakama katika wilaya hiyo? Ili kuweza kuwasaidia wananchi ambao wanapata tabu sana kutoka eneo lingine kwenda lingine kwenda kutafuta huduma za mahakama?

Swali la pili, kwa kuwa Mahakama za Mwanzo zimekuwa katika mazingira mabaya na hayana kivutio cha aina yoyote kwa watumishi wanaofanya kazi kwenye maeneo hayo. Serikali iko tayari kwenda kukarabati jengo la Mahakama ya Mwanzo eneo la Karema na maeneo ya Mishamo ili waweze kupata huduma iliyo sahihi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kwamba huduma ya kimahakama ni huduma ambayo kila mwananchi anastahili. Ni kweli katika mazingira ambayo ameyasema ya Wilaya ya Tanganyika wananchi wanatembea umbali mrefu. Lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba katika mpango huu kama nilivyosema hapo awali katika jibu langu la msingi kwamba kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama ya Wilaya ya Tanganyika ili wananchi wengi zaidi waweze kupata fursa ya kupata huduma za kimahakama.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Wizara yetu ya Katiba na Sheria tumeingia makubaliano na Chuo cha Ardhi pamoja na Taasisi ya masuala ya nyumba tunajenga mahakama hizi kwa teknolojia ya kisasa ya moladi ambayo inatumia muda mfupi sana. Kwa hiyo, imani yangu ni kwamba na zile Mahakama za Mwanzo alizozisema, kutokana na bajeti ilivyo basi tutaanza Mahakama ya Wilaya na hizi zingine pia na kutokana na mfuko wa bajeti ulivyo. Lakini nimhakikishie kwamba Serikali inatambua kilio hicho na tutayafanyia kazi kadri bajeti inavyoendelea kupatikana.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Wilaya ya Tanganyika haina Mahakama ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama ya Wilaya sanjari na kuboresha Mahakama za Mwanzo?

Supplementary Question 2

MHE. JAMES F. MBATIA: Ahsante sana, Mahakama za Mwanzo za Kilema lile jengo limebomoka kabisa na haifanyi kazi na Marangu inayofanya kazi hali ni mbaya sana na inahatarisha Hakimu na watendaji wote. Serikali inaji-commit itafanya lini ukarabati wa mahakama hizi na kujenga hii nyingine upya kwa sababu utoaji wa haki unakuwa ni mgumu sana katika Jimbo la Vunjo na Wilaya ya Moshi Vijijini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Spika, swali hili la Mheshimiwa Mbatia litajibu pia maswali ya Wabunge wengi ambao walitaka kusimama. Serikali inatambua upungufu wa Mahakama za Mwanzo nchi nzima na ndiyo maana katika mpango wa miaka mitano tuliyojiwekea katika Wizara wa uboreshaji wa miundombinu, tunakwenda kuyafikia maeneo yote kadri ya bajeti itakavyopatikana.

Mheshimiwa Spika, lakini pia niwaombe Waheshimiwa Wabunge katika Wizara ya Katiba na Sheria tumetengeneza majedwali ambayo yanaonesha Mahakama ya Wilaya, Mahakama ya Mkoa lakini na vilevile ukarabati na ujenzi wa Mahakama Kuu. Kwa hiyo niwaombe Waheshimiwa Wabunge watakaopata nafasi basi waweze kupitia jedwali lile waangalie katika eneo lake ni lini wamepangiwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo, ya Wilaya na Mkoa.