Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wafanyakazi 545 wa KILTEX – Arusha ambao bado wanadai pensheni toka kiwanda hicho kilipofungwa baada ya Mwajiri wao kutowasilisha michango yao kwenye Mfuko wa Kijamii wa PPF?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wafanyakazi hawa hawakulipwa kama ambavyo jibu linasema lakini walikuwa wakikatwa mishahara yao kila mwezi na pesa hazikuwasilishwa kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kinyume na utaratibu wa kisheria na ni wajibu wa Serikali kuhakikisha makato ya wafanyakazi yanawasilishwa kwenye mifuko na si wajibu wa wafanyakazi. Je, Serikali inatoa tamko gani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa madai ya wafanyakazi ambao wamekuwa wakidai mafao yao yamekuwa mengi sana ikiwepo hata iliyokuwa Hoteli ya Sabasaba ya Mkoani Arusha mpaka leo hawajaliwa mafao yao na nimekuwa nikifuatilia kwa mrefu sana. Je, nini tamko la Serikali?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya swali hilo lakini naomba nichukue nafasi hii kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Catherine Magige katika maswali yote mawili ya nyongeza amelihakikishia Bunge hili kwamba bado lipo tatizo kwanza la kulipwa kwa pensheni kwa wafanyakazi hao lakini lipo tatizo la mwajiri kutopeleka michango ya wafanyakazi katika mifuko iliyokuwa inachangiwa na hao wafanyakazi. Naomba nitumie nafasi hii kuagiza viongozi watendaji wa Mifuko iliyokuwa inahusika na wafanyakazi wa taasisi zote hizi mbili na kwa mujibu sheria mpya tuliyonayo ni wajibu wa Mfuko wenyewe kuhakiksha michango ya mwajiri inapelekwa kwenye mifuko husika, hivyo basi mifuko hiyo ifanye haraka kukutana na wafanyakazi hao na zilizokuwa taasisi zinazosimamia mafao ya wafanyakazi hao ili tuweze kujua nini kilichojiri na kama wanazo stahili zao kwa mujibu wa sheria waweze kulipwa mapema sana na kuweza kuondoa adha kwa wafanyakazi wote katika Taifa letu.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wafanyakazi 545 wa KILTEX – Arusha ambao bado wanadai pensheni toka kiwanda hicho kilipofungwa baada ya Mwajiri wao kutowasilisha michango yao kwenye Mfuko wa Kijamii wa PPF?

Supplementary Question 2

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nadhani Mheshimiwa Naibu Waziri analifahamu vizuri suala hili la Kiwanda cha Nguo cha MUTEX, wale watumishi ajira yao ilikoma toka mwaka 1984 na baadhi yao mafao waliyopaswa kulipwa ilikuwa ni zaidi ya Sh.400,000 ambazo wao walizikaa kwamba hayo mafao yalikuwa ni madogo. Tumehangaika na suala hilo kwa kusaidiana na Mheshimiwa Waziri na hatimaye Desemba mafao yao yakatoka badala ya kulipwa zaidi ya Sh.400,000 wamelipwa chini ya Sh.100,000. Kwa sababu suala hili limechukua muda mrefu sasa, je, Mheshimiwa Naibu Waziri sasa yupo tayari kufuatana nami twende tukakae na hawa watumishi ili hilo suala liweze kuisha?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Manyinyi, Mbunge wa Musoma Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ameomba kuogozana nami kwenda Musoma Mjini, naomba nimwambie baada ya Bunge hili kuahirishwa ziara yangu ya kwanza ni kwenda Msoma Mjini kukutana na wastaafu hawa.

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa wafanyakazi 545 wa KILTEX – Arusha ambao bado wanadai pensheni toka kiwanda hicho kilipofungwa baada ya Mwajiri wao kutowasilisha michango yao kwenye Mfuko wa Kijamii wa PPF?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Swali langu linafafana na yaliyopita, kwa kuwa waliokuwa wafanyakazi wa TAZARA mwaka 2005 na mwaka 2009 wa miaka 55 walistaafishwa kwa lazima idadi yao ni 11,075. Ni lini wastaafu hao wa TAZARA watapewa mafao yao kwani mpaka sasa bado wanahangaika hapa Tanzania?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Susan Kiwanga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze nimeongea naye kuhusiana na jambo hili siku mbili zilizopita na baada ya kuongea naye nimelifuatilia jambo hili na naomba kuweka takwimu sahihi. Kwa takwimu tulizonazo ndani ya Ofisi ya
Msajili wa Hazina, wastaafu waliostaafishwa kwa lazima miaka 55 ni 271 na wala siyo 11,075 kama Mheshimiwa alivyosema. Hao ndiyo wastaafu tunaowajua ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango na sasa hivi faili lao liko mezani kwangu Mheshimiwa Mbunge tangu nimeongea nawe tumeanza kufuatilia ili malipo yao yaweze kulipwa kwa wakati.