Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati na Madini wamepungua sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita:- (a) Je, ni nini kimesababisha hali hiyo? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Wawekezaji wanaendelea kuja ili kukuza uwekezaji kutoka nje (Foreign Direct Investment] (FDI)?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pia namshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake. Hata hivyo, niseme tu kwamba swali langu la msingi ni nini kimesababisha kupungua kwa shughuli za utafutaji wa madini, mafuta na gesi kwenye nchi yetu halijajibiwa na hilo ndilo swali langu la kwanza la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la nyongeza ni kwamba, mwaka jana tulitunga sheria nzuri za kulinda rasilimali za uziduaji, yaani madini, gesi na mafuta ambazo ni “The Natural Wealth and Resources (Permanent Sovereignty) Act, 2017”; The Natural Wealth and Resources Contracts (Review and Re-Negotiation of Unconscionable Terms) Act, 2017; na ile Sheria ya Madini ilirekebishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu; sheria hizi ni nzuri sana, lakini zimesababisha changamoto kadhaa ambazo zimefanya kupungua kwa shughuli za uwekezaji, ikiwa ni pamoja na kuwekwa kwa asilimia 25 ya retention kwa wachimbaji wadogo wanapotaka kuuza madini. Kodi hiyo inawafanya wachimbaji wadogo washindwe kufanya biashara ya wazi. Je, ni lini Serikali itachukua hatua kurekebisha changamoto hizi ili kuhamasisha uwekezaji katika Sekta ya Madini na Mafuta? Ahsante.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya msingi nimejaribu kuelezea ni jinsi gani wawekezaji wanavyozidi kuongezeka kuomba leseni za kufanya tafiti pamoja na leseni za uchimbaji mkubwa na uchimbaji wa kati, vile vile wakiwepo wachimbaji wadogo. Ongezeko hili limezidi na hii inaonesha dhahiri kwamba bado wawekezaji wanazidi kuja kutaka kuwekeza kwenye nchi yetu. Hii ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya sheria ambayo tuliyopitisha katika Bunge lako Tukufu mwaka jana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile mabadiliko yale ya sheria yalikuwa ni kwa ajili ya kulinda rasilimali za nchi yetu. Hata hivyo, tunaendelea kuboresha na kuna kanuni ambazo tumezitoa mwaka huu wa 2018 ambazo kwa kweli wawekezaji wengi walisubiri kuangalia zile kanuni zinakwendaje. Baada ya kuzitoa zile kanuni wengi wamezipitia, wameziona na wengi wameona kwamba wana uwezo wa ku-comply, yaani wana uwezo wa kuendana na zile kanuni na sheria kadri tulivyoweza kuibadilisha. Kwa hiyo wawekezaji wanaendelea kuja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunaendelea kuwawezesha GST waweze kufanya tafiti za kina, waweze kufanya tafiti hadi kufanya zile resource estimation, kwa maana ya kuangalia resources tulizonazo ili baadaye tuwe na uwezo wa kuifanya GST iweze kuuza leseni kwa njia ya mnada. Ili wawekezaji wanapokuja wawe wanakuja kwa nia ya kuchimba tu, ili tuwaondoe katika ile nia ya kutaka kuja kukwekeza kwa maana ya utafutaji wa madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ule utafutaji wengine unawafanya wasite kuja. Hata ukiangalia dunia nzima siyo Tanzania tu uwekezaji katika kutafuta madini umepungua kidogo. Kwa hiyo sisi kama Serikali inabidi tujiongeze kuangalia namna ya kufanya resource estimation, kuangalia kwa kina ili mwekezaji anapokuja aje kuwekeza kwa maana ya kuchimba tu si kutafuta. (Makofi). Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati na Madini wamepungua sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita:- (a) Je, ni nini kimesababisha hali hiyo? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Wawekezaji wanaendelea kuja ili kukuza uwekezaji kutoka nje (Foreign Direct Investment] (FDI)?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza ambalo linaelekezwa kwenye Wizara ya Madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti na Mheshimiwa Naibu Waziri mtakumbuka kwamba miaka ya karibuni pamefanyika ugunduzi wa madini ya aina ya graphite kwenye Wilaya ya Masasi, Kijiji cha Chiwata, Kata ya Chiwata, vile vile Wilaya ya Ruangwa na vijiji vyake; ikiwemo baadhi ya maeneo ya Jimbo la Mtama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali langu, Kampuni ya Nachi Resources ndiyo ambao ilionesha nia ya kutaka kuwekeza, lakini mawasiliano ya mwisho tuliyoyafanya na wao yalionyesha kwamba hawawezi kuwekeza kwenye hayo maeneo kwa sababu pamekuwa na ucheleweshaji wa upatikanaji wa ripoti ya environmental assessment. Sasa Mheshimiwa Waziri, haoni haja ya kuwasaidia Nachi ili kuweza kukamilisha huu utaratibu ili waweze kuchimba hayo madini?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO) Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Nachi Resources ni kwamba wanasubiri kupata ripoti kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) ambayo iko chini ya Mheshimiwa Makamu wa Rais. Sisi hatuna shida kwa upande wa Wizara ya Madini, ni kwamba wale tunaendelea kuwasaidia ili waweze kuwekeza, kwa sababu tunafahamu uchimbaji wa graphite sasa hivi duniani ndiyo unahitajika kwa sababu madini ya graphite sasa hivi ndiyo yanayohitajika zaidi duniani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi kama Wizara ya Madini tunashirikiana nao kuhakikisha kwamba baada ya muda waweze kuanza kuwekeza na kuanza kuchimba. Kwa hiyo, nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba tunashirikiana nao na tunaendelea kuwasiliana na Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) ili iwawezeshe kupata environment impact assessment report ili kusudi waweze kuwekeza na waweze kuendeleza shughuli zao za uchimbaji kama kawaida. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati na Madini wamepungua sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita:- (a) Je, ni nini kimesababisha hali hiyo? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Wawekezaji wanaendelea kuja ili kukuza uwekezaji kutoka nje (Foreign Direct Investment] (FDI)?

Supplementary Question 3

MHE.SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Mkoani Kilimanjaro, Wilaya ya Same, Kata ya Makanya yanapatikana madini ya gypsum, madini hayo Tanzania nzima yanapatikana Manyoni, Pindilo na Makanya kwenyewe. Hata hivyo, miundombinu ya hapa ni mibaya sana na wachimbaji hao ni wachimbaji wakiwemo akinamama na akinababa. Je, Serikali ina mpango gani kuwasaidia wachimbaji hao wakati tunapoelekea kwenye Sera ya Viwanda na Biashara?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO) Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kama Serikali tunazidi kuhakikisha kwamba wachimbaji wadogo tunawawezesha kimiundombinu, kimitaji na kuwasaidia kiteknolojia ili waweze kuchimba na waweze kujipatia kipato chao. Ni kweli kabisa hayo madini ya gypsum ni madini ambayo ni muhimu na yahahitajika katika soko la dunia na baadhi ya nchi za jirani wanahitaji madini hayo na kwa ajili ya ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali pamoja na kupitisha sheria ile ya mwaka jana ya Marekebisho ya Sheria ya Madini tumetaka kwamba madini yote ya gypsum tuweze kuwasaidia wachimbaji waweze kuchimba na kuya-process ili kusudi wapeleke kwenye soko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi pamoja na Wizara nyingine tunasaidiana kupeleka miundombinu kwa maana ya maji, umeme, barabara kwa wachimbaji wadogo dogo ili waweze kuchimba vizuri na kwa gharama ndogo ili waweze kupata faida. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati na Madini wamepungua sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita:- (a) Je, ni nini kimesababisha hali hiyo? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Wawekezaji wanaendelea kuja ili kukuza uwekezaji kutoka nje (Foreign Direct Investment] (FDI)?

Supplementary Question 4

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa maeneo ya uchimbaji madini (mining sites) katika Mkoa wa Dodoma yako zaidi ya 700 na kuna baadhi ya maeneo hayajaanza kuchimbwa kabisa madini. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutangaza kwa wawekezaji ili kusudi waweze kuja kuchimba katika Mkoa wa Dodoma?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi, tuna maombi mengi sana ambayo wachimbaji wadogo na wakubwa wameomba katika Wizara yetu kupitia Tume ya Madini. Hapa Dodoma kuna wachimbaji wadogo wadogo wengi wameomba leseni hizo, kwa maana ya kwamba wanataka au wameonesha nia ya kuchimba. Sisi kama Serikali hivi karibuni ile Tume imeshaanza kufanya kazi na zile leseni tutazitoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema toka mwanzo kwamba tunataka tuwawezeshe wachimbaji wadogo. Mradi katika Wizara yetu ambao ni mradi unaopata fedha kutoka Word Bank, yaani Mradi wa SMRP; mradi huu tunaangalia namna bora sasa ya kuwawezesha wachimbaji wadogo, kwa maana ya kuwasaidia kuwapa teknolojia, elimu na mitaji ili waweze kuchimba. Pia wachimbaji wa Mkoa wa Dodoma na wao wamo kwa sababu sisi tunafanya kazi nchi nzima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwa wachimbaji wadogo ambao wako katika Mkoa wa Dodoma, nipende tu kusema, walioonesha nia au walioomba maombi ya leseni, leseni zitatoka na wachimbaji ambao wanataka kuomba leseni sasa hivi Tume imeanza kufanya kazi walete maombi hayo katika Wizara yetu, tuweze kuwapa leseni, na tuangalie namna ya kuwasaidia ili waweze kuchimba na Wizara iko tayari na tunaendelea na kazi hiyo. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati na Madini wamepungua sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita:- (a) Je, ni nini kimesababisha hali hiyo? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Wawekezaji wanaendelea kuja ili kukuza uwekezaji kutoka nje (Foreign Direct Investment] (FDI)?

Supplementary Question 5

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa mgodi wa Kiwira, umesimama kwa muda mrefu, je Serikali ina mpango gani ya kutafuta Wawekezaji ambao wanaweza kufufua mgodi ule ambao miundombinu yake inakufa?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, Mgodi wa Kiwira sisi kama Serikali tumejipanga kuangalia ni namna gani ya kuwezesha mgodi huo uweze kufanya kazi. Niseme tu kwamba tunashirikiana na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuangalia namna sasa ya kuzuia au kuangalia namna ya kuweza kuondoa zile changamoto zilizopo katika mradi wa Kiwira, ili uchimbaji ule wa Makaa uweze kufanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wawekezaji wengi wameonesha nia ya kutaka kushiriki katika kuchimba Mgodi huo wa Kiwira. Sisi kama Wizara, kwa kweli hatuna shida yoyote, tunahakikisha kwamba ikiwezekana mwaka huu, mgodi huo upate fedha na watu waweze kuchimba na vile vile tutafute wawekezaji wengine ambao wanaonesha nia ya kuwekeza pale, tushirikiane nao kuhakikisha kwamba Mgodi wa Kiwira unaanza kufanya kazi. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati na Madini wamepungua sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita:- (a) Je, ni nini kimesababisha hali hiyo? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Wawekezaji wanaendelea kuja ili kukuza uwekezaji kutoka nje (Foreign Direct Investment] (FDI)?

Supplementary Question 6

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Madini ya rubi yanayopatikana katika Wilaya ya Longido kule Mundarara, biashara yake imedorora kwa sababu mpaka sasa Serikali haikutoa utaratibu wa kuendesha biashara ya madini hayo. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuleta mchakato mzima wa kusimamia na kuendesha biashara ya madini yale?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli madini ya rubi yanapatikana kule Mundarara, Mkoani Arusha. Madini yale ni pamoja na madini mengine. Baada ya mabadiliko ya Sheria 2010, tulizuia kutoa madini ghafi nchini. Tunataka madini yote yapitie kwenye uongezwaji wa thamani ili yaongezwe thamani kwa ajili ya kutengeneza ajira kwa wananchi lakini na vile vile kuisaidia nchi kupata kipato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi ni kwamba madini yale, baada ya zuio hilo, imeonekana kwamba imeshindikana kwa wale waliokuwa wanatoa madini ghafi. Sasa hivi sisi kama Serikali tunaangalia utaratibu wa kuhakikisha kwamba tunawakaribisha wawekezaji, na wako wawekezaji ambao wameonesha nia, ya kuja kuyaongezea thamani madini ya rubi ili kusudi sasa yawe yanauzwa katika hali ambayo yameshaongezwa thamani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii itawasaidia watu wa Mundarara na wachimbaji wote wengine kwa maana kwamba watakuwa sasa wanapata soko la uhakika kuuza ndani lakini vile vile madini hayo tutayatoa nje, yakiwa tayari yameshaongezewa thamani. Hii itasaidia kwa wawekezaji wa ndani wenyewe, lakini vile vile kama Serikali, itazidi kupata kipato kwa maana kwamba tutapata kodi na mrabaha katika madini ambayo yameongezewa thamani. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge kuwa tayari tu kwamba tunaendelea …

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU aliuliza:- Wawekezaji wanaotaka kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati na Madini wamepungua sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita:- (a) Je, ni nini kimesababisha hali hiyo? (b) Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Wawekezaji wanaendelea kuja ili kukuza uwekezaji kutoka nje (Foreign Direct Investment] (FDI)?

Supplementary Question 7

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kuna malalamiko makubwa kutoka kwa utatu wa uwekezaji katika maeneo yote ya uwekezaji, kwa maana ya jamii, Serikali, pamoja na mwekezaji mwenyewe, kila mmoja akilalamikia kwamba hapati stahiki zake. Je, ni lini Serikali itakaa pamoja sasa kuuweka utatu huu, kwa maana ya Serikali, jamii na mwekezaji na kuweka mazingira sawia ambayo kila mmoja atampa haki yake kuwe hakuna malalamiko katika uwekezaji kabla ya mwekezaji hajapewa kibali cha kuwekeza?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais mwaka jana alivyoanzisha Wizara Maalum kwa ajili ya Madini, kwa sababu zamani ilikuwa ni Wizara ya Nishati na Madini, lakini mwaka jana mwezi wa Kumi Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alianzisha Wizara Maalum inayoshughulikia Madini baada ya kuona umuhimu wa kuanzishwa Wizara hii. Kwa kweli tangu Wizara imeanzishwa, sisi tumeanza pale, tumeanza kukaa na wawekezaji, wawekezaji wa kati, wawekezaji wadogo na wawekezaji wakubwa, kuangalia changamoto walizonazo, kuangalia namna bora ya kuweka mazingira ya uwekezaji ili kila mwekezaji aondoke katika kulalamika kutokana na vikwazo anavyovipata katika kuwekeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi kama Wizara tuna mikakati mizuri katika kuhakikisha kwamba wawekezaji wanaokuja wanawekeza vizuri na wanawekeza bila vikwazo. Sasa hivi kuna wengine wamelalamikia kuhusu kodi, nao tumewaambia walete malalamiko yao tuyaangalie. Kwa mfano wawekezaji wa chumvi, kulikuwa kuna kodi 16, katika Bajeti hii zimeondolewa kodi 10.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni moja au kiashiria kimoja cha kuona kwamba Wizara inafanya kazi ya kuwasikiliza wawekezaji na wachimbaji kwa nchi nzima na kuangalia namna bora ya kuwaondolea vikwazo ili waweze kuwekeza na waweze kuchimba kwa faida. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.