Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Joel Makanyaga Mwaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chilonwa

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha Kata ya Haneti na Kata ya Segala kupitia Kata ya Zajilwa ni muhimu sana kwa kufungua mawasiliano katika kata hizo tatu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa barabara hiyo, inatengenezwa kwa kiwango cha kupitika muda wote kwa mwaka?

Supplementary Question 1

MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nichukue nafasi hii kushukuru kwa jibu zuri, fupi, linaloeleweka la Mheshimiwa Naibu Waziri. Hata hivyo, kwa maana ya uelewa wa pamoja nimwombe Mheshimiwa Naibu Waziri tuondoke pamoja twende tukatembelee hii barabara kutoka Zajilwa – Gongolo – Umoja hadi Izava, lakini pia na barabara kutoka Zajilwa hadi Itiso tuone, tushauriane tuone jinsi barabara ilivyo. Ahsante sana.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba, ombi alilotoa Mheshimiwa Joel Mwaka Makanyaga tutalitekeleza.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha Kata ya Haneti na Kata ya Segala kupitia Kata ya Zajilwa ni muhimu sana kwa kufungua mawasiliano katika kata hizo tatu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa barabara hiyo, inatengenezwa kwa kiwango cha kupitika muda wote kwa mwaka?

Supplementary Question 2

MHE. RITA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi, ili niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa katika Manispaa yetu ya Iringa kuna Daraja la Igumbiro, daraja ambalo limekuwa likileta maafa kila mwaka na ambalo limechukua muda mrefu sana kumalizika. Je, ni lini sasa Serikali itatoa pesa ili Daraja lile la Tagamenda liweze kukamilika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo ambayo tunafanya uwekezaji mkubwa wa miundombinu ni pamoja na Manispaa ya Iringa. Serikali ya Chama cha Mapinduzi imeamua kuboresha miundombinu katika Manispaa hiyo ya Iringa na hivi sasa tumekamilisha barabara kadhaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ritta Kabati kwamba wataalam wangu wataenda kufanya tathmini katika eneo hilo ambalo limebakia linaonekana lina changamoto. Lengo letu kubwa ni ili tuhakikishe kama hiyo kazi ina upungufu wa aina yoyote tuweze kuurekebisha ili wananchi wa Iringa wawe katika mazingira mazuri ya kuweza kusafiri.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha Kata ya Haneti na Kata ya Segala kupitia Kata ya Zajilwa ni muhimu sana kwa kufungua mawasiliano katika kata hizo tatu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa barabara hiyo, inatengenezwa kwa kiwango cha kupitika muda wote kwa mwaka?

Supplementary Question 3

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Suala la kupitika barabara ni suala muhimu sana kwa ajili ya uchumi na maendeleo ya wananchi; na kwa kuwa, Madaraja ya Mipande, Mtengula, Chawara hadi kule Buyuni, lakini pia Daraja la Mwitika Maparawe ni madaraja ambayo yamezolewa na mafuriko kutokana na mvua kubwa. Je, nini kauli ya Wizara ya TAMISEMI katika kuhakikisha madaraja haya yanarudishwa ili kuwe na mawasiliano ya usafiri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Bwanausi, kwanza kwa kufuatilia madaraja hayo, kwa sababu nikiri wazi kwamba alifika ofisini kwangu na nilimwelekeza aende akakutane na Mkurugenzi wetu wa Barabara Vijijini, Ndugu Digaga na amefanya hivyo. Ofisi yangu sasa hivi wanakwenda kufanya tathmini ya kina ya nini kifanyike kwa sababu wananchi wa eneo hilo wamekwama sana katika suala la usafiri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama alivyofika kwangu na kama nilivyomwelekeza kufika TARURA, ofisi yetu italifanyia kazi kwa nguvu zote eno hilo.

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha Kata ya Haneti na Kata ya Segala kupitia Kata ya Zajilwa ni muhimu sana kwa kufungua mawasiliano katika kata hizo tatu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa barabara hiyo, inatengenezwa kwa kiwango cha kupitika muda wote kwa mwaka?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Ni azma ya Serikali kuunganisha Makao Makuu ya Mikoa na Wilaya mbalimbali. Mkoa wetu wa Manyara ambao una Makao Makuu Babati hakuna barabara ya lami inayounganisha Wilaya za Kiteto na Simanjiro na nyakati zingine hazipitiki kutokana na hali mbaya ya barabara hizo kuwa za vumbi na kwa kuwa iko kwenye Ilani kwa muda mrefu. Je, ni lini Serikali sasa itaunganisha barabara kutoka Simanjiro na Kibaya kuja Babati kwa kiwango cha lami?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nilihakikishie Bunge Tukufu kwamba utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi unaendelea ambayo imeelekeza ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha lami; na hasa hasa nikitaja barabara ambayo inatoka Kilindi inapita Kiteto inakuja mpaka Dodoma huku Kondoa ambayo ni barabara kumbwa sana itaanza kutengenezwa hivi karibuni chini ya usimamizi wa Wizara ya Ujenzi. Hii barabara ya kutoka Babati kwenda mpaka Simanjiro na ile aliyoitaja nyingine tunaziangalia kwa karibu sana na ndiyo maana matengenezo yake huwa ni ya uangalizi wa juu kabisa chini ya usimamizi ya Mkuu wa Mkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, usimamizi wake umepelekea barabara hizo kuimarika na kwa sasa zinapitika muda wote wa mwaka isipokuwa matengenezo madogo madogo kama kuna mvua kubwa sana. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba utekelezaji utafanyika, naomba tu wananchi wawe na subira.

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha Kata ya Haneti na Kata ya Segala kupitia Kata ya Zajilwa ni muhimu sana kwa kufungua mawasiliano katika kata hizo tatu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa barabara hiyo, inatengenezwa kwa kiwango cha kupitika muda wote kwa mwaka?

Supplementary Question 5

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kata za Rhotia na Mbulumbulu Wilayani Karatu ni maarufu sana kwa uzalishaji wa mazao ya chakula. Hata hivyo barabara za kuelekea kwenye kata hizo zinazounganisha Makao Makuu ya Wilaya ya Karatu zina hali mbaya sana kwa kukosa matangenezo ya mara kwa mara lakini pia kutokana na mvua zilizonyesha mwaka huu; je, ni nini kauli za Serikali kwa Meneja wa TARURA Mkoa ili barabara hizo ziweze kutengenezwa ili wananchi waweze kufika kwenye masoko?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze kaka yangu Mbunge wa Karatu. Kubwa zaidi ni kwamba maelekezo yetu si kwa Meneja wa TARURA wa Mkoa wa Arusha peke yake, isipokuwa ni maelekezo yetu kwa Mameneja wa TARURA wote katika mikoa yote 26, kwamba wafanye needs assessment ya barabara zetu zote zilizoharibika. Lengo letu kubwa ni kwamba kile kichache tutakachokuwa nacho kwa ajili ya ukarabati tuweze kurekebisha maeneo hayo. Kwa hiyo ni maelekezo yangu kwa meneja wa TARURA wa Mkoa wa Arusha na hali kadhalika Mkoa wa Babati, Wilaya ya Karatu wafanye hivyo haraka iwezekanavyo watupe taarifa.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha Kata ya Haneti na Kata ya Segala kupitia Kata ya Zajilwa ni muhimu sana kwa kufungua mawasiliano katika kata hizo tatu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa barabara hiyo, inatengenezwa kwa kiwango cha kupitika muda wote kwa mwaka?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Barabara zote zilizozunguka Mlima Hanang kutokana na mvua kutoka Gendabi, Hatgabadau, Katesh, Gitting, Gerodom na Gendabi zote zimeharibika. Naamini kwamba zitakuwa zimeoneshwa kwenye needs assessment. Je, Mheshimiwa Waziri anasemaje kwa sababu kuna makorongo makubwa yanayozuia akinamama kwenda hospitali na watoto kwenda shuleni?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, mazingira ya Mikoa hii ya Manyara na Arusha yanafahamika, hasa maji yanapoporomoka kutoka kwenye milima yana tabia ya kuharibu barabara kwa haraka sana. Kwa hali hiyo, kama ambavyo Mheshimiwa Waziri wangu amewaagiza Mameneja wa TARURA wote kufanya tathmini ya kina ili maeneo yale yaweze kupata uhakikisho maalum wa matengenezo ambayo yatahakikisha kwamba hayo maji hayaharibu kwa haraka barabara zetu katika maeneo hayo kama ambavyo imekuwa ikitokea. Napenda kumwahidi Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu kwamba tutalifuatilia utekelezaji wa agizo hilo kikamilifu ili maeneo hayo ili tuweze kuyapa kipaumbele kinachotakiwa. (Makofi)

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. JOEL M. MAKANYAGA aliuliza:- Barabara inayounganisha Kata ya Haneti na Kata ya Segala kupitia Kata ya Zajilwa ni muhimu sana kwa kufungua mawasiliano katika kata hizo tatu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa barabara hiyo, inatengenezwa kwa kiwango cha kupitika muda wote kwa mwaka?

Supplementary Question 7

MHE. SUSAN A. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Barabara ya Kimara - Bahama Mama - Msewe kwenda Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilijengwa ili kuondoa msongamano katika Barabara ya Morogoro. Sasa magari haya yanapita Chuo Kikuu na Chuo Kikuu barabara imeharibika sana. Je, ni lini Serikali itajenga barabara ile ya Chuo Kikuu kutoka Msewe kuelekea jengo la Utawala ili kufanya mandhari ya Chuo Kikuu iwe nzuri kwa sababu kwa kweli barabara hiyo imeharibu sana barabara za Chuo Kikuu?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara aliyoitaja ni muhimu sana katika kupunguza msongamano wa magari katika Barabara ya Morogoro hasa kwa watu wanaokwenda maeneo ya City Centre. Hata hivyo, barabara ile ina changamoto ya ufinyu wake. Kama inatakiwa kutengenezwa vizuri basi inatakiwa fidia kubwa sana ilipwe kwa wananchi ambao wamejenga mpaka karibu na barabara, hasa kuanzia Kimara kuja kupita maeneo ya milima ya Golani, kuja kuteremsha chini kwenye daraja hapo kuna uvamizi mkubwa sana ambao ulifanywa na wananchi, barabara ile ni finyu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo matengenezo yake yanahitaji tathimini ya kina ambayo itaishauri Serikali namna ya kuiendeleza hiyo barabara. Naomba sana kwa sasa hivi matengenezo madogo madogo ambayo yanafanyika wananchi watuvumilie yaendelee hiyo hivyo mpaka ambapo tathmini ya kina itakapokamilika.