Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Tunapoelekea kujenga uchumi wa viwanda ni wazi kuwa fursa za kibiashara zinazojitokeza nyingi zitafanywa na wajasiriamali wadogo; hata hivyo muundo wa kazi kwa kada ya Maafisa Biashara katika Halmashauri zetu umefichwa ndani ya Idara ya Fedha, pamoja na kazi na uzito wa majukumu ya biashara siyo idara wala kitengo:- Je, ni lini Wizara kwa kushirikiana na Utumishi itafanya kada hii kutambulika kwa uzito wake ili wanufaike na uwepo wa Maafisa Biashara kuliko ilivyo hivi sasa?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali na pia kwa kukiri kwamba inaufanyia mapitio muundo na kwamba itazingatia mawazo ambayo nimeyatoa kutokana na swali langu, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, wakati huu ambapo tunaelekea uchumi wa viwanda, ni matarajio kwamba Maafisa Biashara tulionao watakuwa na wajibu zaidi ya wajibu walionao sasa ambao kimsingi umejielekeza zaidi katika kufanya kazi ya kutoa leseni na kukagua leseni. Maafisa hawa wengi wao ni watu ambao wana elimu zao, wamesoma mambo ya international trade, international business na kadhalika, kwa hiyo, tunakuwa kama tuna wa- under utilize. Je, lini mipango hiyo ya kukamilisha muundo itakamilika? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Serikali iko tayari wakati inaendelea kukamilisha suala hilo la muundo kuwa- task na kuwawezesha Maafisa Biashara ili waweze kuwasaidia wajasiriamali wetu kuibua miradi, kuwasaidia kuandika maandiko lakini pia kung’amua fursa mbalimbali za mikopo ya riba nafuu. Kwa mfano, kule kwetu Mafinga kuna wafanyabiashara na wajasiriamali wa mazao ya misitu kama mbao, mirunda na nguzo na majirani zangu Njombe wanalima maparachichi. Je, Serikali wakati inaendelea kukamilisha muundo huo iko tayari kuwa-task na kuwawezesha ili wafanye shughuli hizo za kuibua miradi? (Makofi). Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nirejee katika swali langu la msingi nimemshukuru sana kwa mchango wake. Hata haya maswali yake mawili ya nyongeza bado ameendelea kuweka mchango mzuri wa mawazo ambao utakuja kusaidia sana Serikali. Yeye ana uzoefu mkubwa, amefanya kazi katika Serikali za Mitaa sehemu nyingi sana, kwa hiyo, uzoefu wake tutautumia. Hata baada ya leo hapa namkaribisha ofisini kwangu ili tujadiliane kwa kina zaidi haya masuala ya Serikali za Mitaa kwa sababu wote tuna uzoefu nayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu wajibu wa Maafisa Biashara, muundo utakapokamilika wataongezewa wajibu zaidi, kwa sababu sasa kama tunawatoa kwenye ile Idara ya Fedha tunawapeleka kwenye Idara nyingine ambavyo sipendi kuitaja kwa sababu haijawa rasmi watashirikiana huko na Maafisa Maendeleo ya Jamii na Wachumi katika kutekeleza yale ambayo Mheshimiwa Mbunge anayependekeza.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Tunapoelekea kujenga uchumi wa viwanda ni wazi kuwa fursa za kibiashara zinazojitokeza nyingi zitafanywa na wajasiriamali wadogo; hata hivyo muundo wa kazi kwa kada ya Maafisa Biashara katika Halmashauri zetu umefichwa ndani ya Idara ya Fedha, pamoja na kazi na uzito wa majukumu ya biashara siyo idara wala kitengo:- Je, ni lini Wizara kwa kushirikiana na Utumishi itafanya kada hii kutambulika kwa uzito wake ili wanufaike na uwepo wa Maafisa Biashara kuliko ilivyo hivi sasa?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kutokana na mwamko uliopo wa wananchi kujiunga na vikundi vya ujasiriamali pamoja na VICOBA lakini wananchi wamekabiliwa na kutokuwa na uwezo wa uzalishaji. Tatizo hili linachangiwa na kutokuwepo na Maafisa Biashara wa kutosha katika Halmashauri zetu na kuwajengea uwezo wananchi. Halmashauri zote nchini zina Afisa Biashara mmoja au wawili au hakuna kabisa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwaajiri Maafisa Biashara wa kutosha? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama alivyosema katika mazingira ya sasa kuna vikundi vingi vya uzalishaji mali, kuna VICOBA na shughuli nyingi za kiuchumi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kutokana na kazi nzuri inayofanywa na Mheshimiwa Dkt. Kalemani na timu yake kueneza umeme vijijini na kazi nzuri inayofanywa na Mheshimiwa Profesa Mbarawa na timu yake kujenga barabara na sisi kupitia TARURA kujenga barabara za vijijini, fursa nyingi sana zinajitokeza. Kwa hiyo, kuna kazi kubwa sana iliyoko mbele yetu ambayo tunahitaji kuifanya kupitia kada hizi za Afisa Biashara, Maafisa Maendeleo ya Jamii na Wachumi. Serikali itahakikisha kwamba wanapatikana wa kutosha ili kusudi wananchi wahudumiwe vizuri. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Tunapoelekea kujenga uchumi wa viwanda ni wazi kuwa fursa za kibiashara zinazojitokeza nyingi zitafanywa na wajasiriamali wadogo; hata hivyo muundo wa kazi kwa kada ya Maafisa Biashara katika Halmashauri zetu umefichwa ndani ya Idara ya Fedha, pamoja na kazi na uzito wa majukumu ya biashara siyo idara wala kitengo:- Je, ni lini Wizara kwa kushirikiana na Utumishi itafanya kada hii kutambulika kwa uzito wake ili wanufaike na uwepo wa Maafisa Biashara kuliko ilivyo hivi sasa?

Supplementary Question 3

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa ukataji wa leseni unaenda sambamba na uwasilishaji wa tax clearence katika Halmashauri zetu na uwasilishaji wa tax clearance unaamaanisha kwamba watu wamelipa kodi, kwa maana hiyo watu wanalazimika kulipa kodi kabla hata ya kufanya biashara. Je, hatuoni kwamba ni muhimu kuondoa kigezo cha tax clearance katika baadhi ya biashara ili watu waweze kukata leseni na kuanza biashara kabla ya kulipa kodi na kabla ya biashara zenyewe kuanza? (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake linalenga kujaribu kutetea wafanyabiashara wale wanaoanza na utetezi wa aina hiyo siyo mbaya, ni mzuri. Hata hivyo, kwa sababu kuna kanuni, sheria na taratibu ambazo zimewekwa, nalichukulia swali lake kama mchango wa maoni ambao unahitaji kufanyiwa kazi baadaye lakini kwa leo hatuwezi kutoa tamko kwamba sasa tunafuta taratibu hizo. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Tunapoelekea kujenga uchumi wa viwanda ni wazi kuwa fursa za kibiashara zinazojitokeza nyingi zitafanywa na wajasiriamali wadogo; hata hivyo muundo wa kazi kwa kada ya Maafisa Biashara katika Halmashauri zetu umefichwa ndani ya Idara ya Fedha, pamoja na kazi na uzito wa majukumu ya biashara siyo idara wala kitengo:- Je, ni lini Wizara kwa kushirikiana na Utumishi itafanya kada hii kutambulika kwa uzito wake ili wanufaike na uwepo wa Maafisa Biashara kuliko ilivyo hivi sasa?

Supplementary Question 4

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa jitihada za kutoa mitaji kwa vijana na wanawake inabidi ziende sambamba na kuwajengea uwezo wa kuanzisha na kuendeleza biashara. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwatumia hawa Maafisa Biashara katika kuwajengea uwezo vijana wanaokuwa katika vikundi ambao wananufaika na asilimia 10 inayotengwa kutoka kwenye mapato ya ndani ya Halmashauri? Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kwa dhati kabisa nimshukuru na kumsifu sana Mheshimiwa Zainab Katimba kwa sababu yeye amekuwa anashughulikia sana sana maslahi ya vijana katika Bunge hili Tukufu. Aliwahi kuleta mpaka mapendekezo ya hoja kutaka kutetea vijana wanaomaliza shule ili kusudi waajiriwe bila kuwa na experience. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimhakikishie kwamba vijana katika nchi hii wana idara nyingi sana za kuweza kuwasaidia mawazo ya kujikwamua kutoka pale walipo kwenda mbele. Katika Halmashauri kuna Idara ya Vijana, Idara ya Maendeleo ya Jamii na Idara ya Mipango sasa Maafisa Biashara tunawongezea sehemu nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda sana nitumie nafasi hii kuwaomba vijana wa nchi hii ambao hata fursa ambayo ziko katika Halmashauri hawazitumii ipasavyo, ukienda katika Halmashauri unakuta maombi ya vijana yako asilimia 10 ya maombi yote yaliyowasilishwa. Kwa kweli, naomba sana Waheshimiwa Wabunge tujitahidi kuwaelimisha na kuwaomba vijana wajitokeze na wajiunge katika vikundi na watumie fursa zilizopo kwa ajili ya kujiendeleza na Serikali tuko macho katika kuangalia suala hilo linatekelezwa vizuri. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:- Tunapoelekea kujenga uchumi wa viwanda ni wazi kuwa fursa za kibiashara zinazojitokeza nyingi zitafanywa na wajasiriamali wadogo; hata hivyo muundo wa kazi kwa kada ya Maafisa Biashara katika Halmashauri zetu umefichwa ndani ya Idara ya Fedha, pamoja na kazi na uzito wa majukumu ya biashara siyo idara wala kitengo:- Je, ni lini Wizara kwa kushirikiana na Utumishi itafanya kada hii kutambulika kwa uzito wake ili wanufaike na uwepo wa Maafisa Biashara kuliko ilivyo hivi sasa?

Supplementary Question 5

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na Serikali kuendelea kutenga maeneo ya kibiashara kwa ajili ya wajasiriamali wadogo, lakini bado kumekuwa na changamoto kubwa kwa wajasiriamali hawa wadogo hususani katika Manispaa ya Mpanda Mjini kwamba wamepelekwa kwenye maeneo ambayo miundombinu ya kibiashara pamoja masoko imekuwa na changamoto kubwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wajasiriamali hawa katika Manispaa ya Mpanda Mjini? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzia mwaka juzi Serikali imetoa maelekezo kila Halmashari, Wilaya na mkoa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya uwekezaji. Uwekezaji ni kuanzia uwekezaji mdogo, wa kati na mkubwa hususani maeneo ya viwanda, viwanda vidogo, viwanda vya kati na vikubwa na yawepo maeneo maalum kwa ajili ya biashara katika kila mji na kila Halmashauri. Kwa hiyo, hayo ni maelekezo ambayo yanakwenda kuboresha maeneo yetu ya Miji, Halmashauri na minada.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hayo maelekezo ya Serikali yatakapokamilika kutekelezwa vizuri, miundombinu ni sehemu ya mahitaji kwenye maeneo hayo mapya. Kwa hiyo, tunazidi kusisitiza kila halmashauri inapotenga eneo jipya lazima liambatane na miundombinu inayohitajika, ikiwemo umeme, maji na vyoo. Kwa hiyo, masuala yote ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyazungumza, kama ni Mpanda basi tutafuatilia tuhakikishe kwamba hiyo miundombinu inayokosekana inakuwepo. Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.