Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:- Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, Wilaya ya Mbogwe pamoja na Mikoa ya Kanda ya Ziwa tuna matatizo makubwa sana ya huduma za afya, matokeo yake wananchi walio wengi wanategemea sana huduma za waganga wa jadi na huko wakati mwingine wanapata uchonganishi na kuuana. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kuwajengea wananchi wa Mbogwe Hospitali yao ya Wilaya? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pamoja na kuipongeza Serikali kutupatia shilingi milioni 800 kwa ajili ya vituo vya Afya vya Iboya na Masumbwe. Je, Serikali iko tayari sasa kutupatia wataalam zaidi pamoja na vifaatiba? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiopingika kwamba Mikoa ya Kanda ya Ziwa pale ambapo huduma ya hospitali inakosekana wamekuwa wakitumia tiba mbadala na kwa Mheshimiwa Mbunge imekuwa ni jambo la kawaida. Hata hivyo, sasa hivi tangu Serikali kwa kushirikiana na wananchi wameanza zimeanza kujengwa zahanati pamoja na vituo vya afya, naamini mentality imeenda iki-change.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilienda Jimbo la Itilima kwa Mheshimiwa Silanga nikakuta kuna zahanati nyingi sana ambazo zimejengwa kwa kushirikisha wananchi na mwitikio ni mkubwa sana. Naomba hiyo kazi nzuri ambayo wameanza wenzetu wa kule ni vizuri na Mheshimiwa Mbogwe na yeye akaiga mfano mzuri ili wananchi wetu wahame katika tiba mbadala ambayo imekuwa ikisababisha mpaka watu kuuana kwa sababu ya masuala mazima ya kupiga ramli.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili juu ya suala zima la kupeleka wataalam, naomba nimhakikishie kwamba baada ya mchakato kukamilika wameajiriwa wataalam hakika na yeye mwenyewe anakiri kwamba tumempelekea vituo viwili vya afya. Ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba na wataalam wanapelekwa ili vituo vya afya vifanye kazi iliyokusudiwa.

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:- Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 2

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Tatizo la Hospitali ya Wilaya lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe ni sawa na tatizo la Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi. Tayari Hospitali ya Mawenzi imezidiwa na wagonjwa kama Hospitali ya Mkoa na Manispaa ya Moshi kwa muda mrefu imekuwa na ombi hilo la Hospitali ya Wilaya ambalo tayari Serikali imeonekana imelikubali. Je, ni lini Serikali sasa italeta fedha ili hiyo Hospitali ya Wilaya ya Manispaa ya Moshi iweze kujengwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo ambayo Hospitali za Wilaya hazipo zinaenda kujengwa na ndiyo maana tumeanza na hospitali 67. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya kwamba hizo 67 kukamilika hatutaishia hapo tutaenda maeneo mengine ambayo hakuna Hospitali za Wilaya ili tuweze kujenga.

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:- Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika juhudi za kuboresha huduma za afya katika Jimbo la Bagamoyo, wananchi katika Kata mbalimbali zikiwemo Nianjema, Fukayosi na Mapinga wameanza ujenzi wa zahanati katika vijiji vyao. Je, nini kauli ya Serikali kuhusu kuwaunga mkono kumalizia ujenzi wa zahanati hizi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kujibu naomba kwa dhati kabisa nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa maana katika vituo vya afya vilivyojengwa vya kupigiwa mfano ni pamoja na Kituo chake cha Afya cha Bagamoyo. Naomba na wengine wa mikoa ya jirani ambao vituo vya afya vinaendelea kujengwa wakatazame mfano mzuri jinsi ambavyo walivyosimamia na value for money ikaonekana katika Kituo cha Afya cha Bagamoyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya utangulizi huo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kama ambavyo Serikali imekuwa ikiwaunga mkono maeneo mengine katika Jimbo lake, tukimaliza hatua hii, kama ilivyo kwenye Ilani ya CCM kwamba tunahakikisha tunajenga zahanati kila kijiji na kituo cha afya kila kata, naomba tuvute subira hicho ndicho ambacho ni ahadi yetu sisi kwa wananchi, tutaenda kutekeleza.

Name

Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:- Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 4

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuulizwa swali la nyongeza. Kwa kuwa Hospitali nyingi za Wilaya kama Hospitali ya Sinza, Dar es Salaam ambayo ilikuwa Kituo cha Afya cha Sinza Palestina kimepandishwa hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, hospitali hiyo haipati fedha kama Hospitali ya Wilaya na kukosekana kwa fedha hizo kumesababisha hospitali kushindwa kukidhi mahitaji yake ikiwemo kuwa na chumba cha kuhifadhia maiti. Je, Serikali iko tayari kupeleka fedha za Hospitali ya Wilaya katika Hospitali ya Sinza Dar es Salaam?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kukumbusha kwamba swali hili limekuwa likiulizwa la Sinza Palestina, naomba nimjibu Mheshimiwa Said Kubenea kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nilishawahi kujibu hapa, Kituo cha Afya cha Sinza Palestina siyo Hospitali ya Wilaya. Katika jibu langu ambalo nililitoa siku ile nilitaka Halmashauri wahakikishe kwamba wanatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. Nikajibu pia kwamba katika kituo cha afya na hii ni changamoto katika vituo vya afya vingi ambavyo viko mijini tunakosa jina hasa ambalo tungeweza kusema kwa sababu viko juu ya vituo vya afya vya Kata za vijijini lakini pia havifikii hadhi ya Hospitali ya Wilaya. Ndiyo maana ukienda Sinza Palestina pale tumepeleka mpaka Madaktari Bingwa lakini bado hiyo haitoi mwanya kwamba tuseme ni Hospitali ya Wilaya. Kwa sababu Hospitali ya Wilaya inahitaji eneo la ukubwa usiopungua ekari 25.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulishawaambia Halmashauri yake watenge eneo hilo ili tujenge Hospitali ya Wilaya kama ambavyo tunafanya kule Kivule kwa Mheshimiwa Waitara ili tuwe na hospitali za Wilaya kupunguza msongamano katika hospitali zingine.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:- Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 5

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri ya Morogoro mpaka sasa haina hospitali ya Wilaya na kwa kuwa Tarafa ya Ngerengere na mahali ambapo panajengwa hospitali ya Wilaya kuna umbali wa zaidi ya kilometa 105.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Ngerengere kuna miradi mitatu mikubwa ya Kitaifa ambayo ni standard gauge pamoja na ujenzi wa kiwanda cha sukari pamoja na Bwawa la Kidunda ambao unasababisha wingi mkubwa wa watu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati Kituo cha Afya Ngerengere ili kiwe na hadhi ya kituo cha afya kuweze kuwa-accommodate watu hawa wote na kujenga Kituo kingine cha Afya katika Kata ya Mkulazi? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabla ya kujibu naomba nitangulize maneno yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ambayo tumekuwa tunapata taabu pale ambapo pesa za maendeleo zinapelekwa hazifanyiwi kazi kwa wakati ni pamoja na kwa Mkurugenzi wa Halmashauri anayotoka Mheshimiwa. Kuna pesa zimepelekwa kwa ajili ya kujenga kituo cha afya lakini kasi yake ni mbovu sana. Naomba nichukue fursa hii kwanza kumuagiza Mkurugenzi ahakikishe kwamba pesa iliyopelekwa inatumika kukamilisha ujenzi wa kituo cha afya ili wananchi waweze kupata huduma ya afya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya utangulizi huo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha maeneo yale yote ambayo iko haja na kama ambavyo ametaja umbali na ni ukweli usiopingika kwamba Ngerengere ina umuhimu wake. Naomba nimhakikishie kwamba baada ya hili zoezi kukamilika na mimi nikapata fursa ya kwenda, tutashauriana namna nzuri ya kuweza kuhakikisha ukarabati unafanyika na huko.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:- Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 6

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Napenda kuipongeza Serikali kwa kutenga shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Nyang’hwale. Napenda niiulize Serikali, huduma ya X-ray kwa Wilaya ya Nyang’hwale ni shida sana. Kuna ajali mbalimbali ambazo zinatokea na kuifuata huduma ya X-ray karibu kilomita 110. Je Serikali ina mpango gani wa kuleta mashine ya X-ray katika Hospitali ya Wilaya ya Nyang’hwale? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ambayo Waheshimiwa Wabunge wamefanya vizuri kwenye suala zima la afya kwa maana ya ujenzi wa vituo vya afya na zahanati ni pamoja na kwa Mheshimiwa Amar. Naomba nimpongeze kwa dhati kabisa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba X-ray zinakuwepo ndani ya vituo vyote vya afya na ndiyo maana katika maboresho ambayo yamefanyika hivi karibuni ni pamoja na kuongeza jengo la X-ray. Sasa kama X-ray zinakuwepo kwenye vituo vya afya sembuse hospitali ya wilaya! Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tukitoka hapa tuwasiliane tujue nini hasa ambacho kimetokea mpaka hospitali yake ya Wilaya ikose X-ray. (Makofi)

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe iliweka kiasi cha shilingi bilioni 1.5 katika bajeti yake ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya kuanza kujenga hospitali ya Wilaya. Hata hivyo, kutokana na ukomo wa bajeti uliowekwa, fedha hiyo iliondolewa katika bajeti:- Je, Serikali itakuwa tayari kutenga fungu maalumu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbogwe?

Supplementary Question 7

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wananchi wamekuwa wakishiriki huduma za afya kwa kujenga maboma. Kwenye Kata yangu ya Kimuri, wananchi wameweza kujenga vyumba zaidi ya 20 lakini vyumba hivi vimekaa zaidi ya miaka 10 Serikali haijaweza kukamilisha. Je, Mheshimiwa Waziri wako tayari kukamilisha hivyo vyumba ili wananchi waweze kupatiwa huduma bora ya afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ambayo Serikali tunaenda kujenga vituo vya afya pamoja na hospitali za Wilaya ni pamoja na Mkoa wa Kagera. Naamini Mheshimiwa Mbunge naye ni miongoni mwa Waheshimiwa Wabunge wanufaika katika Serikali ya Awamu ya Tano ambao wanaenda kupata huduma hii ambayo haikuwepo kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala zima la kukamilisha hivyo vyumba 20 ambavyo anavisema, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, wanasema kuona ni kusadiki. Ni vizuri pale ambapo tutapata nafasi ya kwenda kutazama ili tujue uhalisia na bajeti kiasi gani itahitajika kumalizia huo ujenzi ili nguvu ya wananchi isije ikapotea, kama Serikali tutakuwa tupo tayari.