Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:- Serikali imetumia zaidi ya shilingi milioni 350 kuimarisha barabara ya Namanyere – Ninde yenye urefu wa kilomita 67, lakini fedha hazikutosha kukamilisha barabara hiyo:- Je, Serikali itatenga fedha zaidi kukamilisha barabara hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kufuatia majibu ya Serikali tayari barabara hii imetumia zaidi ya milioni 439.8 katika jitihada ya kutaka kuifungua. hata hivyo, mwaka huu haijatengewa fedha na wanasema itaendelea kuitengea fedha kadri fedha itakavyozidi kupatikana. Je, Serikali haioni kwamba kwa kufanya hivi inachelewa na fedha ambazo tayari imesha-invest kwenye barabara hizi zitakosa thamani?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kufuatia mvua nyingi zilizonyesha katika Mkoa wa Rukwa kuna barabara katika Jimbo la Nkasi Kusini zimefunga kabisa. Barabara hizo ni pamoja na Kisula - Malongo Junction - Katongolo- Namasi- Ninde - Kanakala na tayari TARURA imeleta taarifa ya orodha ya barabara hii. Je, ni lini fedha sasa zitatolewa kwa ajili ya kwenda kurudisha miundombinu ili iweze kutumika?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, naomba kwanza uniruhusu kipekee nimpongeze sana Mheshimiwa Mipata barabara hii amekuwa akiipigania kwa nguvu zake zote na ndiyo maana Serikali imesikia kilio chake na hicho kiasi cha pesa kikaanza kutumika.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie kama ambavyo yeye mwenyewe amesema itakuwa si busara kwa Serikali kuweza pesa bila kupata matunda kwa sababu matunda yanayotarajiwa ni barabara kufunguka. Hata hivyo, naye atakubaliana nami kwamba barabara hii haikuwepo kabisa na kazi kubwa ambayo imekwishafanya kuhusiana na ujenzi wa madaraja pamoja na yale makalvati hakika pesa ikipatikana kipande ambacho kimebaki kitaweza kufunguliwa na wananchi waweze kupita kwenye hiyo barabara.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, anaongelea baada ya mvua kunyesha kumekuwa na uharibifu katika barabara hizo ambazo amezitaja na bahati nzuri TARURA walishaleta makisio ya nini ambacho kinatakiwa kutumika. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pesa ambazo zilitengwa kwa ajili ya emergence almost zote zilishakwisha na theluthi mbili ya pesa hizo zilitumika katika kurudishia miundombinu katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, pia naomba nimhakikishie kwa sababu bajeti ilishapitishwa naamini muda siyo mrefu pesa ikianza kupatikana na eneo la kwake litaweza kufunguliwa hizo barabara.